November 2007
no image
Bwana Michuzi,
Nimesoma kwa makini habari yenye kichwa cha habari noma kwenye blog yako. Nikiwa kada mwenye uchungu wa nchi hii nimeonelea nami niweke mambo sawa kwa kujibu kila lililosemwa, na ushahidi nnao. Ni kwamba, Bwana Michuzi, yote yalosemwa ni uongo wa mchana usiokuwa na kichwa wala miguu. Hao bwana asikudanganye mtu, ni wenzetu ambao sasa wamegundua matumaini waliokuwa nayo yametoeka baada ya nyota ya CCM kurudia kung'ara. Wamepoteza muelekeo hawana pa kushika.Hivyo wameamua njia hii ya uongo na kupakana matope.Bahati mbaya nayo haitasaidia kwa sababu ni uongo wa kitoto. Na wewe Bw. Michuzi usipoibandika hii kitu hapo chini nitajua kuwa na wewe ni hao hao kwani ilitoka kwenye mtandao huo huo ila mahasidi wakaminya na kukuletea ya upande mmoja tu, nawe ukaingia geji. Washindwe!
Si Mwingine ila ni mimi,
Mdau Nambari wani wa Nambari wani

1.Hadithi ya Bw.Gogo: JK hana swahiba Bagamoyo anayeitwa Gogo ambaye kanunuliwa gari ya Nissan na kuzunguka misikitini nchini kuhamasisha Waislamu kumuunga mkono JK wakati wa mchakato wa kutafuta uteuzi ndani ya CCM.Ama kweli njia ya muongo ni fupi.Mchakato ulikuwa ndani ya CCM hapakuwepo na haja ya kuzunguka misikitini.Kutafuta nini?Hakuna kura kule? Mwandishi amethibitisha asivyokuwa mwana CCM ingawaje anajifanya ni mmoja wao. Pia amethihbitisha asivyomfahamu JK.Yeye(JK) si mdini na hakuna wakati wo wote ametumia Uislamu wake kutafuta kura kabla, wakati na hata baada ya mchakato.Yuko hivyo hata sasa na atabaki hivyo kesho na kesho kutwa.
2.Kutekwa Anna Kilango: Anadai "ana ushahidi wa kuhusu Ana Kilango kutekwa ENEO LA GAIRO nje kidogo ya mji wa Morogoro,kuibiwa shilingi milioni mbili na kufanyiwa mambo mabaya." Mtu mwenye kudai kuwa na ushahidi anashangaza pale anaposhindwa kujua kuwa Gairo si nje kidogo ya mji wa Morogoro bali ni kilomita 125 kutoka Morogoro.Pia kwamba Ana Kilango hakutekwa Gairo. Kesi iliendeshwa hadharani Mahakamani asibabaishe watu kuwa anazo habari za siri za kutoa.Kama kweli anao ushahidi zaidi ya ule wa Polisi mbona hakuwapa Polisi wakati kesi inaendeshwa mpaka ikaisha zaidi ya mwaka mmoja na nusu sasa. Hata kama alishindwa kuwapata Polisi angempa habari hiyo Ana Kilango au Mzee Malecela ambao wangemshukuru sana kwani wangenufaika nayo sana kwa maana ya kesi na siasa wakati ule. Kutunga na hata kutoa uongo huo sasa hauna tija na wala hautambabaisha mtu ye yote.JK
hakuhusika na wala hakuna rafiki yake aliyehusika na tukio hilo la ujambazi.
3.Ngono na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uganda mwaka 2004: Huyu mtu anastahili kupuuzwa na kudharauliwa kwa uongo wa kijinga. Mwaka 2004 Uganda haikuwa na Waziri wa Mambo ya Nje mwanamke.Waziri alikuwa marehemu Wapakabulo na baada ya kufariki yeye akateuliwa Bw.Sam Kutesa anayeendelea mpaka sasa. Hili la JK kufanya ngono kwa siku mbili mfululizo na kushindwa kwenda mkutanoni halina msingi wowote. Rais Museveni hajaandika barua ya aina hiyo kwa sababu haikuwepo sababu ya kufanya
hivyo.
4.Fedha Chafu: CCM wala JK hawajapokea hata senti moja kutoka kwa Rais Joseph Kabila. Hapakuwa na haja ya kufanya hivyo. JK na CCM haijachangia hata senti tano kwenye uchaguzi wa Joseph Kabila na Chama chake. Hawajahi kuombwa na hivyo hawakuwa na sababu ya kufanya hivyo.Serikali ya Tanzania ilitoa mchango kwenye mpango wa SADC kuisaida Tume ya Uchaguzi ya DRC uliobuniwa na kuchangiwa na nchi wanachama wa SADC. Michango
iliratibiwa na ilitolewa kupitia Sekretariet ya SADC Gaborone, Botswana. Kamwe mchango huo haukupelekwa kwa mgombea ye yote binafsi, bali kwenye Tume tena kwa kuwapatia vifaa vilivyohitajika kufanikisha uchaguzi.
5.Millennium Towers Hotel: Madai ya JK kuwa na swahiba yake Jack Gotham katika hoteli hiyo na kufanya vitendo vya ngono na msichana wa UDSM ni uongo mtupu.Kwanza JK hana uswahiba na Jack Gotham. Ni watu wanaofahamiana lakini si watu waliowahi kuwa pamoja wakati wo wote katika hotel hiyo kwa ajili hiyo inayodaiwa.Hawako karibu kiasi cha kufikia kufanya hayo yanayosemwa.Ni maneno ya hasidi mwenye nia mbaya tu kwa JK. Lakini hapa amechemsha.
6.Klabu karibu na Red Cross: JK hajawahi kutembelea klabu hiyo maisha yake yote.Hata yeye haijui jina kama vile ambavyo hata mwandishi haijui.Isitoshe hajawi kukaa pamoja na vijana hao katika klabu au bar au mahali pengine po pote.Hivyo basi kuhusishwa na mkutano na vijana aliowataja mwandishi katika klabu hiyo na hadithi zote zinazodaiwa kutokea kwa ajili hiyo ni mambo
yasiyokuwa na hata chembe ya ukweli.Ni mambo ya kugushi tu.Hakika mwandishi hamfahamu JK ndiyo maana amesema mambo ambayo hata mtoto anajua uongo.JK hakuwa na matembezi ya klabu wala bar yo yote hapa jijini.
7.Kuoa mke kutoka Uarabuni: JK ana mke mmoja tu Salma. Hana mke mwingine, si kutoka Uarabuni wala kwingineko. Hadithi ya kuoa mke mpya ni upuuzi mtupu. Hii ni Bongoland kama mwandishi kakutana na tapeli shauri yake.Siku nyingine akikutana nae amtake ushahidi wa ndoa. Morogoro kuna kijana kawaibia watu wengi kwa kujiita mdogo wa JK aitwaye Yusufu. Alikamatwa na sasa anatumikia kifungo.
8.Hoteli ya Serengeti: Kwa kuwa suala la kuoa mke mpya ni jambo la uongo hivyo hadithi ya JK kuchukua eneo Serengeti la kujenga hoteli kwa ubia na mke huyo si jambo la kweli.JK hajengi hoteli po pote pale.


miss tz 2007 ni richa adhia ambaye hivi tunavyoongea yamebaki masaa machache kabla hajapanda jukwaani kwenye kinyang'anyiro cha miss world 2007 huko sanya, china. tumuombee ushindi binti yetu huyu anayetuwakilisha.
MUNGU MBARIKI RICHA
MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE
AMINA

hivi ndivyo mambo yalivyokuwa mwaka 1967 siku miss tz ya kwanza ilipofanyika hoteli ya kilimanjaro na mshindi akiwa bibie theresa shayo (5) ambapo baada ya hapo yakapigwa marufuku kabla ya kuibuliwa tena na kina lundenga mwaka 1994
no image
Michuzi,
Kila siku tunasema wewe ni kada wa CCM unaminya. Sasa kuna hii email inazagaa kila sehemu kuhusu swahiba'ako JK. Kama kweli wewe si kada na una ubavu ibandike kwenye globu yetu ya jamii. Hapo nitaamini wewe huna noma wala nini na ni mshikaji. Hakyanani tena we kama mwanaume ibandike hii
-Mdauz,
Ukerewe
Baada ya kusoma kwa makini kwa siku nne mfululizo, kwenye forum yetu hii tukufu, na baada ya kuona kuwa uongozi wa forum hii tukufu umeamua kuwa kila anayeona uovu wa viongozi wa kisiasa na haswa wenyeviti wa vyama vya siasa ana haki ya kuleta ujumbe wake hapa bila kubugudhiwa kitu ambacho nakiheshimu sana kwenye ujenzi wa demokrasia na pia haki ya kupata habarikwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya muungano ya Tanzania ibara ya 18.
Na pia nimeguswa kuandika ujumbe huu kutokana na kile nilichokiona kwenyegazeti la majira la jana (front page) na pia kauli iliyotolewa na katibumkuu wa CCM ndugu Makamba kuunga mkono hoja iliyowekwa hapa forum na wanachadema! Kama ilivyorushwa kwenye taarifa ya habari ya channel ten janasaa moja jioni .
Makamba alisema kuwa viongozi wa upinzani waache kurusha mawe ile hali waowako wakiishi kwenye nyumba za vioo!nimeshtuka na kuogopa kama huyu ndioanatakiwa kuonyesha njia ya kuweza kufikia maisha bora kwenye taifa hili , nashindwa kuamini kuwa huyu ndio dereva wa chama tawala !
Leo nimeona niweke ushahidi wangu hapa juu ya ufisadi wa ziada na au uovuuliotendwa na JK pamoja na timu yake wakati wa kuwania kuteuliwa na chamachake, na pia jinsi alivyotumia cheo chake cha waziri wa mambo ya nje kuendekeza ngono na kulisababishia taifa hili madhara makubwa ikiwa nipamoja na mahusiano ya kidiplomasia kuwa mabaya.

Naanza kuweka hoja zangu na ushahidi wake kama ifuatavyo

1.Kikwete wakati anagombea kuteuliwa kuwa mgombea wa CCM ,aliunda timu za aina mbalimbali ila kwa hapa nazungumzia timu yake ya uharamia ambayo aliiunda, aliunda timu ya kuwafanyia maasi wagombea wenzake na mojawapo ni hii iliyokuwa inaongozwa na mtu anayeitwa Gogo kutoka kule Bagamoyo.
Huyu alinunuliwa gari aina ya Nissan patrol ,na ndio mwanzo alitumika kupitakwenye misikiti mbalimbali na kutengeneza mtandao wa kiislamu,ila huyu Gogondio alihusika na aliongoza kikosi kilichohusika kumpora mke wa mzee Malecela fedha taslimu zaidi ya milioni mia mbili wakati anatoka dar kwendadodoma kwa ajili ya kampeni. ENEO LA GAIRO.

Gogo akiwa na vijana wenzake walimteka mama Kilango nje kidogo ya mji wamorogoro na kumpora fedha hizo na pia kumfanyia mambo ya ajabu ambayo kwamtu mzima kama mimi siwezi kuyaandika hapa.(ushahidi upo na nitautoa muda wowote kama utahitajika hapa ,niandikie kwenye PM yangu.)

2.Akiwa waziri wa mambo ya nje mwaka 2004 alipokwenda nchini marekanikuiwakilisha nchi kwenye kikao cha UN alifanya ngono na aliyekuwa waziri wamambo ya nje wa Uganda kitu kilichowafanya kutokuweza kuhudhuria mkutano kwa siku mbili mfululizo, na ndipo rais museven alimwandikia rais mkapa rasmimalalamiko yake na pia alimtimua kazi waziri huyo .

Hili linaifanya nchi yetu kutokuwa na mahusiano mazuri na serikali ya Ugandana haswa kati ya Kikwete na Museven na hili limechangia kwa kiasi kikubwahata kutokufikiwa kwa shirikisho kwani Museven anaamini kuwa hawawezi kujadili mambo serious na JK kutokana na kutokwenda kuwakilisha nchi nabadala yake ikawa ni kwenda kufanya ngono na waziri aliyetumwa na nchinyingine bila hata aibu.

3.Kikwete akiwa na swahiba wake wa karibu anayeitwa Jack Gotham,wakiwamaeneo ya millennium towers hotel kijitonyama ,walimchukua binti wamfanyibiashara mmoja wa jijini ambaye alikuwa anasoma shahada ya kwanza chuo kikuu cha DSM na kufanya naye ngono hapohapo hotelini na kumfanya kuchelewakwenda kwenye ziara za kampeni kwani kipindi hiki kilikuwa ni wakati wamchakato wa kampeni ukiwa unaendelea.

Huyu anaacha hata masuala ya maana na kwenda kumchukua binti wa rafiki yakeambaye amemchangia kiasi kikubwa cha fedha za kampeni zake na kufanya nayengono.

4.Fedha chafu.Kikwete aliingiza nchini kiasi kikubwa sana cha fedha chafu kutoka kwenyenchi za uarabuni na nyingine alizitoa Jamhuri wa Kidemokrasia ya Congo(DRC)kutoka kwa Joseph Kabila na fedha hizi ziliingizwa kupitia mkoani Kigoma na nyingine ziliingilia mkoani Mwanza .Ujumbe wa watu wa kongo uliongozwa na Luten Jenerali Peter Gessimba Gabonneakiwa na wasaidizi wake watatu ambao walikuwa ni viongozi wa jeshi tiifu kwaKabila.Fedha hizi zilitolewa kwa masharti kuwa endapo angeshinda ni lazimaahakikishe kuwa Kabila naye anashinda kule Congo kitu ambacho alikifanya nahata kutumia pesa za taifa hili kwa ajili ya uchaguzi wa congo kwa wale mnaokumbuka Asha Rose Migiro alisema kiasi cha pesa zilizotolewa na misaadamingine ……..

5.Ngono.JK akiwa na maswahiba wa mwanae wa karibu waitwao Benno (huyu kwa sasaanagombea ujumbe wa NEC ndani ya chama chetu),Said (huyu ni msaidizi maalumuwa kumsaidia mzee Makamba) ,Mussa (huyu alikuwa ni kiongozi mwandamizi wa mbio za mwenge mwaka huu), na Sisko (huyu ni chief protocol wa ikulu)wakiwakwenye club mojawapo jijini dar,(ipo mkabala na red cross-barabara yaAlhassan mwinyi) kabla ya mchakato wa kampeni kuanza rasmi walimchukua binti anayeitwa Hadija ……aliyekuwa anasoma UDSM na pia ni mfanyibiashara wa mjiniArusha, ila alikuwa pia ni mke wa aliyekuwa meneja msaidizi wa kituo kimojacha kimataifa nchini , na kufanya naye ngono .

Kitendo hiki kilimfanya Hadija kuachika /kuachwa na mumewe na kumnyanganyamagari pamoja na mtaji kitu kilichopelekea binti huyu kuishi kwa taabu hadiJK alipoweza kushinda urais wa nchi na kumpangishia nyumba maeneo ya Kijitonyama ambako anaishi hadi sasa.Pia JK alimwamuru Benno ambaye ni afisa mwajiri wa jumuiya ya UVCCMkumwajiri bint huyu makao makuu na kwa sasa ameajiriwa kama katibu wauhamasishaji wa taifa cheo ambacho hakipo hata kwenye katiba ya umoja huo, kwa toleo la 2003 ambalo ninalo hapa.

6. Ngono ,Alifanya ngono iliyoligharimu taifa hili zaidi ya shilingi milioni mia nneNa themanini, (480 milioni) akiwa kule Zanzibar Hotel Kempinski palealipokuja na mkewe mpya kutoka uarabuni na kukaa naye kwenye mapumziko hayo ambayo yaliliingizia taifa hasara hiyo kwa muda wa siku 9 tuu.Mkuu wetu wa nchi anatumia rasilimali zetu kwa ajili ya kujistarehesha yeyebinafsi na wanawake zake kutoka huko uarabuni.

7.Ubadhirifu.Aliweza kujichukulia eneo ndani ya mbuga za wanyama kule Serengeti na sasaanajenga hotel ya kisasa nah ii anaijenga yeye kwa ubia na mke wake huyo wauarabuni akishirikiana na mashemeji zake hao , swali la kujiuliza ni je?huu mkataba hautaishia kwenye kuliuza taifa hili? Mke anaenda kupewa mahari ya rasilimali zetu? Kama kila rais akioa ni shartiatoe sehemu ya mbuga zetu je? Mpaka lini tutakuwa tunachezea taifa kwa faidaza kuoa ama kupata ngono!

Huyu ndio mwenyekiti wa chama chetu na bado tunamwona kama malaika aliyetokambinguni kama sio kuzimu!

Nitakuja na taarifa pia za kina juu ya ndugu Nchimbi ambaye naambiwa kuwaanaweza kuwa ndio katibu mkuu wa chama chetu, jambo ambalo mimi nalipingakwa nguvu zote kwani huyu naye anaendelea kufanya mambo ya aibu na wanafunzi wa vyuo mbalimbali vya umma nchini.

Ni mimi mwanachama mtiifu na mpenda maendeleo ya chama chetu kitukufu. Mwanachama


novemba 18, 1995: siku moja kabla hatujamwapisha mh. benjamin mkapa kuwa rais wa awamu ya tatu uwanja wa taaifa wa neshno. kulia ni moshy kiyungi wa the guardian, kabendera shinani wa bbc (marehemu) na mie mbangaizaji. siku kama hii lazima mje siku moja kabla kula tizi na kuangalia namna ya kukaa kupata snepu nzuri

miss tz 1995 emmily adolph akivishwa taji na miss tz 1994 aina maeda baada ya kushinda. kesho huko china miss tz 2007 richa adhia anapanda jukwaani kutuwakilisha katika miss world. tumuombee heri ashinde na kuletea taifa sifa


januari 13, 1968: miss zanzibar wa kwanza hediye khamis mussa (kati) akipozi na wenzie baada ya kutwaa taji. mashindano hayo yaloandaliwa na chama cha hockey, kama ilivyokuwa kwa bara baada ya shindano la kwanza mwaka 1967, yalipigwa marufuku na hadi hii leo hayajafanyika tena huko visiwani

habari toka mwisho wa reli zinasema treni la abiria toka kigoma limekwama sehemu za kaliua siku ya nne leo na wadau wanasota ile mbaya. hii ni mara ya tatu kwa usafiri huu kuleta noma toka ulipoanza upya tokea stesheni ya dar kwenda bara siku ya novemba 1, 2007

Nakupa Hi sana tena sana Mr.Michuzi!!!!!

Habari za huko kwetu Bongo, ninapenda kutoa shuikrani zangu nyingi kwako Michuzi kwa kutupatia habari na picha mbalimbali zinazo tukumbusha nyumbani. Mimi nipo hapa Italy mji wa Cesena, mtanzania ni mimi peke yangu hapa mji wa Cesena, ni mpweke sana. Lakini kwa blog yako Michuzi inanifariji sana tena sana, yaani ninafuraha sana kwa hii blog. Hongera sana tena sana, ninakutakia mafanikio mema mengi, nikija Bongo nitakuja kukutembelea. Salamu nyingi sanaaaaaaa......!!!!!!!!

- Mdau Baraka Franco Chibiliti
no image
We are welcoming Tanzanians to our event, but they MUST register online or call us. They cannot just show up at the dinner because the room will be full!!! And we don’t want to turn anyone away!
they must either register online at
call us at 202.736.2239.

Nichet Smith Director,
Public Relations
Leon H. Sullivan Foundation
1800 K. Street NW Suite 1021 Washington,
DC 20006 202.736.2239 202.736.2226
Sullivan Summit VIII "The Summit of A Lifetime"
June 2-6, 2008
Arusha,
Tanzania
REGISTER NOW ONLINE!!
no image
KAKA MICHUZI SAMAHANI SANA MIMI KAMA MDAU WA BLOG YAKO NA MPENZI MKUBWA WA SOKA NAOMBA UWE UNATUEKEA MATOKEO YA BIG FOUR KILA WIKI ILI WADAU WAKO TUWEZE KUTOA MAONI YETU.
NIMECHOKA KUONA UNAJIPENDELEA MWENYEWE TU MATOKEO YA TIMU YAKO LIVERPOOL WAKATI UMESEMA BLOG YETU WOTE. MATOKEO YA ARSENAL,LIVERPOOL,MAN UNITED NA CHELSEA YAWEKWE NADHANI SIO KAZI NGUMU SANA.

asante sana muheshimiwa michuzi nitashukuru wazo langu ukilitekeleza.

Dear Friends and Colleagues

Music Mayday Tanzania is happily inviting you for a film launching on Thursday 13th December 2007 at Alliance Francaise

These are 4 films of 3 minutes each made by 4 young Tanzanians after a 6 weeks training

The function will start from 06:00 pm – 09:00pm.

This is under a Show Me Your World Project which is funded by Vipaji Project

This email is to alert you in making this time of your day free and come and support young Tanzanians creative work!

Invitation cards would be sent to you!


Many Thanks


Fatma Mussa
Program Assistant


Music Mayday Tanzania
P.O.Box 34747
Kijitonyama, Dar es Salaam
Tanzania
T. + 255 2771156
F. + 255 2771156
C. + 255 754 592643

www.musicmayday.org
www.b-connected.to


waziri mkuu mh. el akiwa na mkuu wa mkoa wa kagera na waheshimiwa wengine wa meza kuu wakiwapongeza wanakamati wa kagera dei kwa kazi nzuri. jumla ya milioni 100 keshi zilichangwa hapo hapo na pamoja na ahadi jumla ya shilingi bilioni 1.4 zilipatikana


waziri mkuu mh. el akiisifu kamati iliyoandaa kagera dei usiku kuamkia leo diamond jubilei. shoto ni profesa anna tibaijuka, akifuatiwa na waziri wa elimu mh. margareth sitta na kulia ni bosi wa kampuni ya simu ya nanihii na wa pili yake ni mkuu wa mkoa wa kagera

balozi wa ukerewe nchini mh. philip parham akiteta na waziri wa nchi ofisi ya makamu wa rais (mazingira) profesa mark james mwandosaya ofisini kwa waziri. mazungumzo yalihusu mkutano wa mabadiliko ya tabia ya nchi utaofanyika huko bali, indonesia, desemba 3, mwaka huu ambapo prof ataongoiza ujumbe wa bongo
no image
KAGERA DEI USIKU KUAMKIA LEO AMBAPO WAZIRI MKUU EL ALIKUWA MGENI RASMI ILIFANA SANA. MILIONI 100 ZILIKUSANYWA HAPO HAPO UKUMBINI DIAMOND JUBILEE NA PAMOJA AHADI ZILIKUSANYWA BILIONI 1.4 AMBAYO NI REKODI KATIKA MICHANGO YA KUSAIDIA MAENDELEO YA MIKOA. DAR ILIKUSANYA MILIONI 700 KWENYE MFUKO WA CHANGIA ELIMU

injinia juma hussein msonge ni mmoja wa wadau waliokula nondozz ya Masters in Engineering Management satadei ilopita chuo kikuu cha udsm. hongera sana mdau na asante kwa pongezi za bwawa la maini kwa kumpiga mkole porto jana. mambo ya yu neva woki aloni hayo, usikonde

Dully Sykes kaingia Holland kwa vishindo leo asubuhi tayari kwa show itakayo fanyika Delft ijumaa 30/11/2007 na kaahidi kufanya maajabu huku akitamba na kibao chake kipya BABY CANDY.
Pichani ni wakati Mr. Misifa alipowasili Amsterdam Airport (Schiphol) akiwa na Promoter wake Charles Gadi kushoto pamoja na Pascal na Bachalla.
no image
Brother Michu,
Salaam Alaykum.Naomba nifikishie salamu zangu za pongezi kwa uongozi mzima wa ATC hususan rubani wa leo aliyetajwa kwa jina la Muze.
Katika hali isiyo ya kawaida nikitokea Dar kuja Arusha leo asubuhi, Rubani huyu aliamua kwa makusudi mazima kutupitisha juu ya mlima kilimanjaro ili kila mtu aliyekuwemo kwenye ndege auone kwa karibu saaaaaaana mlima huo na aliuzunguka kwa karibu dakika kumi hivi ila kila mwenye camera aweze kuchukua picha hiyo adimu kwa karibu na kwa ufasaha.
Bahati mbaya kinyamkwemba changu nilikuwa nimekisahau dar hivyo sikuweza kufotoa hiyo picha ili nishee na wadau wa blog hii but it was veeeery exciting!!!
Nilipenda maneno ya rubani " COURTESY OF AIR TANZANIA TO PROMOTE OUR MOUNTAIN AND WITNESS HOW GLOBAL WARMING AFFECTS THE SNOW TOP OF KILIMANJARO PLEASE HAVE A CLOSER LOOK AND IF POSSIBLE TAKE A PHOTOGRAPH FOR THOSE WITH CAMERA"
shukrani ATC
Mdau,
Mani-yuu
no image
kaka michuzi,
jana mgomo uliendelea hapa chuoni (Ardhi) ila ilipofika mida ya mchana hivi kwa wale wenye akaunti crdb waliekewa hela zao za project,sasa najiuliza hivi,kwanini linapokuja suala la fedha kwenye taasisi za elimu ya juu hazitoki mpaka watu tugome??
Kwa upande mwingine leo jumatano wanafunzi wote tumeingia madarasani huku tukisubiri muongozo kutoka kwa wanaharakati wetu(sio viongozi) kwani mpaka sasa viongozi wetu wa serikali ya wanafunzi hawajatuonesha ushirikiano wowote kuhusu matatizo yetu, sanasana wametubandikia orodha ya majina ya wanafunzi ambao hawajalipa fedha yao ya serikali tunayooiita 'union fees'
Kwakweli najiuliza viongozi wetu wamegoma kutupa ushirikiano kwakuwa hatujalipa hela au??mimi sidhani kama hiyo ni sababu,kwani hata katika semester zilizopita hela tumekuwa tukilipa kwenye serikali yetu lakini matatizo yapo palepale,,wengi wao ni puppet yani hawawezi kujiongoza wenyewe.
kwa ufupi tu ni kwamba tunasubiri wanaharakati wetu waliojitoa muhanga kwa ajili yetu watuambie nini kitafuata ama baada ya mgomo wetu huo wa siku mbili.kazi njema kaka.


miss tz 1994 aina maeda akiwa na mshindi wa pili lucy tabasamu ngongoseke (shoto) na dotto siku umiss uliporudi rasmi baada ya kupigwa stop mwaka 1967 yalipofanyika mashindano ya kwanza kabisa ya urembo bongo na mshindi kuibuka theresia shayo ambaye sasa ni marehemu. richa adhia ndio miss tz mwaka huu na hivi sasa yuko sanya, china,k ambako jana miss ghana alishinda miss talent na kupata tiketi ya kuingia robo fainali moja kwa moja. katika ngwe hiyo miss scotland alikuwa wa pili na wa tatu alikuwa miss sweden.
*wadau naomba radhi. kweli nilichemsha kusema aina maeda alikuwa miss tz 2004. kunradhi kwa usumbufu, sasa nimerekebisha
no image
WANAFUNZI WA MWAKA WA KWANZA CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA ELIMU CHANG'OMBE (DUSE) WAMEGOMEA MASOMO LEO WAKIWA NA MADAI KADHAA MOJAWAPO IN ANAYOSEMEKANA KUSABABISHA MGOMO HUO NI KUSTUKIZWA MITIHANI KWA TAARIFA YA WIKI MOJA, INGINE NI KUAMBIWA KWAMBA WATAFANYA MITHANI MITATU KWA SIKU NA PIA WANAFUNZI KUSACHIWA VITABU VINAVYOSADIKIWA KUIBWA MAKTABA KWA NAMNA YA UNYANYASAJI WA KIJINSIA AMBAPO ASKARI WA KIUME HUSACHI WANAFUNZI WA KIKE
WAKATI HUO HUO LIBENEKE LA MGOMO CHUO KIKUU CHA ARDHI LINAENDELEA JAPO CHUO KIMEPIGWA MKWARA KWAMBA WANAFUNZI WATAKUWA WAMEJIFUKUZISHA MASOMO ENDAPO WATAKAIDI KURUDI MADARASANI AMBAKO WAMESUSA KWA SIKU TATU MFULULIZO KINYUME NA TARATIBU ZA CHUO
no image
MICHUZI,

UMEWAONA WEVI HAO, YAANI HUO NAPATA EMAILS KIBAO ZA KUSHINDA LOTTO ANGALAU WAO WAKO SMART SASA HATA HII VISA YA USA RIVER NAYO? YAANI JAMAA NI WAJINGA AJBU MIMI SIJAAPPLY HIYO DV LOTO WATANILETEAJE UTUMBO HUU KUWA NIMESHINDA? PILI HATA HIYO LOTO BADO TAREHE YA MWISHO KUAPPLY HAIJAPITA. THESE 9JAS ARE NOT CLEVER AT ALL. WANGESUBIRI HATA HIYO TAREHE YA KUAPPLY IKAPITA. MWANAWANE WASTUWE WATU WASIJE WAKALIWA MAPESA YAO BURE HASA WALIOAPPLY DV-LOTTO.
-MDAU

AMERICAN DV2007 VISA LOTTERY PROGRAM.
SUCCESS NOTIFICATION LETTER.
DV LOTTERY.STATE.GOV,

U.S Department of State,
Kentucky Consular Center,
1001 Visa Crest Migrate,
KY 41901-1000
www.dvlottery.state.gov

Dear Winner,
It is my pleasure to congratulate you on your success in the AMERICAN DV2007 VISA LOTTERY PROGRAM which was applied and processed by our agency. You were selected as one of the lucky winners on our internet screening machine,for the DV2007 USA national visa lottery program. Your visa lottery winner's identity is ID-7200DV and your serial net visa passport with us is SNVPh700IU.In this respect, you are directed to forward the following requirements:
l. Your present contact address (for correspondence) 2. Your recent passport photograph . 3. REGULAR MAIL.
You can also send your photo(s) by regular mail. The photo must be between 2 by 2 inches (37-50 mm) square, with the applicant's,spouse's, or child's name printed on the back.Please mail the photos to:
Immigration Services: PA/PL,Rm.3206, U.S.Department of State Kentucky Consular Center 1001 Visa Crest Migrate, KY 41901-1000.
Or preferably, you can scan them and send via email for faster processing. Clearance/acceptance fees is($989.67)
Details of requirements:
Your present contact address should be forwarded strictly to our receiving correspondent email address (
Verificationonline01@excite.com) We accept Western Union Money Transfer as the ONLY payment method due to some reasons from our past experiences. (Credit card is not acceptable, please.) Your payment confirmation shall be sent to you as soon as clarification is done on your payment.
Providing the above requirements will assure you of getting your Visa Lottery Acknowledgement Card and Visa Lottery Security Code which we shall send to your email address.
Important notice: Please make sure you report and forward your Visa Lottery Code and Acknowledgement Card to the USA embassy in your individual country for your Green Card and other necessary claims.
According to the United States of America's Code of Conduct and Constitution Vol.176/866:Act 690SN guiding all immigration, and Green Card permit Agencies, Non-Response,14 days after you receive this message to your winner's status shall reveal "No interest" and we would in return, refer your lottery code and acknowledgement card back to the USA Government/Immigration Service Center. We shall be anticipating your reply soon.
CONGRATULATIONS ONCE MORE.
Mrs. Magdalene Collins,
Coordinator.

KELVIN POWELL,
Executive Director.

Note: Your response/reply should be sent ONLY to the above stated Email network. This is for security reasons

hi Michuzi,
i hope unapambana kiubishiubishi na libeneke la hapo EastAfrica please post picha ya my confidant wangu SIAN. hapa ni jana amevuta nondo ya Bachelor of Science(Hons) Health Services Management toka University of East London ilikuwa safari ndefu na ngumu lakini amefika.God bless u and ur heavenly work at our Blog.
-Internet Enterpreneur at
www.nunuatokalondon.co.uk

waziri mkuu wa canada mh. stephen harper alitembelea bongo kwa ziara ya siku moja ambapo pamoja na mambo mengine alitembelea shule na kutoa ahadi ya nchi yake kusaidia afrika na asia katika masuala ya afya. nenda http://pm.gc.ca/eng/media.asp?id=1911
no image
H.E. President Jakaya Mrisho Kikwete has appointed Dr. Mohammed Omar Maundi (54) to the Tanzanian High Commissioner to Addis Ababa, Ethiopia. Dr. Maundi is replacing Ambassador Walid Mangachi who was earlier this year transferred to Abuja, Nigeria.
Before the appointment, Dr Maundi was a Minister Counselor in the Permanent Mission of the United Republic of Tanzania to the United Nations, New York.
He joined the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation on 24 March, 1981 as a Foreign Service officer before serving twice as a Lecturer and Head of the Department of Strategic Studies at the Centre for Foreign Relations, Dar es Salaam between 1992-1993 and July 2000 –October 2004.
He also rose to the rank of Acting Director of Studies and Programmes at the Centre Foreign Relations, Dar es Salaam from November 2001 to December 2002. For a period of one year served as a Senior Officer, Political and Diplomatic Affairs, SADC Secretariat, Gaborone Botswana.
Dr. Maundi also served as Political Officer and Head of Chancery at the Tanzania Embassy in Addis Ababa, Ethiopia between 1987-1991. The appointment is with immediate effect.
Issued by:
The Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation
no image
ROMANCE MATHEMATICS

Smart man + smart woman = romance

Smart man + dumb woman = affair

Dumb man + smart woman = marriage

Dumb man + dumb woman = pregnancy

______________________________

OFFICE ARITHMETIC


Smart boss + smart employee = profit

Smart boss + dumb employee = production

Dumb boss + smart employee = promotion

Dumb boss + dumb employee = overtime

_____________________________

SHOPPING MATH

A man will pay $20 for a $10 item he needs.

A woman will pay $10 for a $20 item that she doesn't need.

_____________________________

GENERAL EQUATIONS & STATISTICS

A woman worries about the future until she gets a husband.

A man never worries about the future until he gets a wife.

A successful man is one who makes more money than his wife can spend.

A successful woman is one who can find such a man.

_____________________________

HAPPINESS


To be happy with a man, you must understand him a lot and love him a little.

To be happy with a woman, you must love her a lot and not try to understand her at all.

______________________________

LONGEVITY


Married men live longer than single men do, but married men are a lot more willing to die.

______________________________

PROPENSITY TO CHANGE

A woman marries a man expecting he will change, but he doesn't.

A man marries a woman expecting that she won't change, and she does.

_____________________________

DISCUSSION TECHNIQUE

A woman has the last word in any argument.

Anything a man says after that is the beginning of a new argument.

_____________________________

HOW TO STOP PEOPLE FROM BUGGING YOU ABOUT GETTING MARRIED

Old aunts used to come up to me at weddings, poking me in the ribs and cackling, telling me, "You're next." They stopped after I started doing the same thing to them at funerals.
no image
Wadau,
nawaombeni munisaidie kwenye hii mada; nimeombwa niongelee juu ya economic development in tanzania hapa kwenye chuo kikuu huku czech republic, before colonisation and now. sina moja. naombeni michango yenu.
natanguliza asante zangu.
nana.
no image
Massimo yaanda mbio za baiskeli Dodoma

KLABU ya mbio za baiskeli ya Massimo ya mjini Dodoma, imeandaa shindano maalum kwa ajili ya Siku ya Ukimwi Duniani zitakazofanyika Desemba Mosi, mwaka huu mjini humo.
Kwa mujibu wa mratibu wa mbio hizo za kilomita 135, Nicola Morganti, uandikishaji wa washiriki utafanyika siku moja kabla ya shindano kwenye Uwanja wa Jamhuri, Dodoma.
Hata hivyo mshauri huyo wa klabu ya Massimo alisema bado wanahitaji kwa udi na uvumba wadhamini wa mbio hizo za aina yake.
“Udhamini ni tatizo, inatufanya tushindwe kufanya mambo makubwa zaidi, lakini kwa kadri ya uwezo wetu tunajitajidi kuandaa ili kuendelea kuyafanya kuwa ya kila mwaka,” alisema Morganti ambaye ni raia wa Italia.
Mbio hizo ambazo mshindi wake atajinyakulia kitita cha sh 100,000, zimepangwa kuanzia Dodoma Mjini na kufuata barabara ya Dar es Salaam hadi eneo la Mbande, linalotenganisha wilaya za Dodoma na Kongwa.
“Kutokana na kukosa wadhamini, hata zawadi zetu zimekuwa ndogo, lakini tukipata wa kutuokoa angalau kwa wakati huu, mambo yanaweza kuwa mazuri zaidi katika mashindano yetu na ustawi wa mbio za baiskeli kwa ujumla nchini,” alisema Morganti, akiongeza kwamba, mshindi wa pili atajipatia sh 75,000 wakati mshindi wa tatu atajinyakulia sh 50,000.
Washiriki wawili watakaoshika nafasi za nne na tano kila mmoja atajipatia sh 25,000, wakati watakaoshika nafasi kati ya sita na 10 kila mmoja atapata sh 10,000. Kifuata jasho cha sh 5,000 kitakwenda kwa washiriki watakaoshika nafasi kati ya 11 na 20.

KWA MAWASILIANO ZAIDI;
The Team Leader
Luis Musisi
0757622633
P.O. BOX 2938
Dodoma
The Advisor,Nicola Morganti,0782490917,
dodocola@maf.or.tz

Kaka Michuzi,

Pole kwa kazi. Naitwa Rachel Manning Mwalwaka. Naomba nikupongeze kwa kazi nzuri uifanyayo ya kupashana habari. Nina Imani hata baba yangu Manning Jasson Mwalwaka huko Uholanzi haimpiti mbali hii Blog.
no image
Iwapo Tanzania itafanikiwa kuingia kwenye kundi la timu 20, majaliwa ya kuwa wa kwanza au wa pili katika kundi letu la kwanza, basi tutakuwa tumejiweka katika nafasi nzuri ya kucheza fainali za Afrika mwaka 2010 nchini Angola hata kama hatutafanikiwa kwenda Kombe la Dunia Afrika Kusini. Kwa nini? Kwa sababu washindi watatu wa kwanza wa kila kundi (kundi litakuwa na timu nne), watakwenda moja kwa moja kwenye fainali za Afrika. Sasa hapo tushindwe wenyewe tena.
Angalia hapo makundi yalivyo, halafu soma utaratibu wake utakavyokuwa, kwa Kimombo ili kuweka msisitizo.
Africa draw:
Group 1: Cameroon, Cape Verde Islands, Tanzania, Mauritius.
Group 2: Guinea, Zimbabwe, Namibia, Kenya.Group
3: Angola, Benin, Uganda, Niger. Group
4: Nigeria, South Africa, Equatorial Guinea, Sierra Leone.
Group 5: Ghana, Libya, Gabon, Lesotho.
Group 6: Liberia, Algeria, Senegal, Gambia.
Group 7: Ivory Coast, Mozambique, Botswana, Madagascar.
Group 8: Morocco, Rwanda, Ethiopia, Mauritania. Group
9: Burkina Faso, Tunisia, Burundi, Seychelles.
Group 10: Mali, Congo, Sudan, Chad.
Group 11: Togo, Eritrea, Zambia, Swaziland.
Group 12: Egypt, DR Congo, Malawi, Djibouti.
1. They will play six rounds of matches through 2008 with the 12 group winners plus eight best runners-up progressing to the last league stage.
2. The 20 remaining teams are to be divided into a final stage of five groups of four, with the resultant group winners going onto the World Cup in South Africa and the top three in each group qualifying for the 2010 Nations Cup finals in Angola.

Should South Africa finish top of their group, the runner-up would qualify for the 2010 World Cup.
Caf also used the 2006 World Cup qualifiers to determine the 16 Nations Cup finalists in Egypt the same year.
Africa are to have six teams at the World Cup finals for the first time.
-Mobhare Matinyi.

no image
Mkubwa michuzi assalaam aleykum? naomba uniwekee hii kwenye web yako maana washikaji wanapitia wengi. Nawatafuta washikaji zangu kwa mara ya mwisho tulimaliza wote Mgulani Primary School 1990- Lusungu Mng`ong`o na Ferdinandi Nyaluchi kwa yeyote anaeyejua walipo hao jamaa plesase mail me!Thanx in advance kaka.

Hello vipi mjomba michuzi,
mimi ni mdau hapa uk. leo tupo kazini kuna jamaa wawili wa kimarekani wakawa wananiulizia kama nashekherekea `kwanzaa` nikashangaa kwani sijawahi kusikia sikukuu hiyo,ila baadae wakanionyesha web-site ya african-americans nikagundua ni sikukuu kubwa huko america.wanaaita kwanzaa,na pia wana nguzo (principle) zao ambazo ni pamoja na ujamaa,umoja nk maneno wanayotumia ni hayo hayo ya kiswahili. Nikaona nikujulishe ili wengine waelewa jinsi lugha yetu inavyotumika ulimwenguni.
no image
Bwana Michu,
naomba ufungue ukurasa wa habari hii, naona wadau wamebinya kimyaaa, vilevile cheki link hapo chini ya TED talks [Andrew Mwenda anavyochambua wazungu:Tatizo ni Lugha
Ukiangalia AY yeye kwenda kwa wifi zetu Kenya na Uganda ndo amefika, ni kweli sio mkali lakini namheshimu kwa kujenga jina lake East Africa.
MwanaFa huyu bwana ninaheshimu mashairi yake, ni mkali ktk lyrics, namshauri sasa atunge albamu moja tuu ya kiingereza. Kisha aendelee na nyimbo zake za kiswahili.
Haya sasa nakuja kwa Mr Misifa, hapa ni talent iliyokosa manager wa nguvu na sio wa kutoka bongo. Kwanza kabsa atafute manager nje ya Africa halafu aingie full shangwe katika reggae dancehall riddims, achukue beats zinazotoka kila siku Jamaica, awe anatunga nyimbo hata akiweza aimbe kwa English.
Kila siku kina Sizzla, Jah Cure, Morgan Heritage na kadhalika wanafanya vitu vya uhakika.Sababu moja Bongo Flava haisikiki kimataifa ni lugha, kina 2Face wamefika mbali ni kwa sababu ya English.
Sasa muda umefika kwa hawa wana bongo flava kuanza kuimba kwa kiingereza angalau albamu moja wapige kwa kiiengereza kwa ajili ya INTERNATIONAL MARKET.
Andrew Mwenda:
http://tedtalks.blip.tv/ , cheki video ya Andrew Mwenda.

wadau wa tampere huko ufini majuzi walisherehekea mwanza dei kwa libeneke hadi lyamba. watembelee kwenye globu ya mdau mjema http://kilimanjaro-wim.blogspot.com/pamoja na ya wadau wa tampere http://watanzaniatampere.blogspot.com/