Bwana Michuzi,
Nimesoma kwa makini habari yenye kichwa cha habari noma kwenye blog yako. Nikiwa kada mwenye uchungu wa nchi hii nimeonelea nami niweke mambo sawa kwa kujibu kila lililosemwa, na ushahidi nnao. Ni kwamba, Bwana Michuzi, yote yalosemwa ni uongo wa mchana usiokuwa na kichwa wala miguu. Hao bwana asikudanganye mtu, ni wenzetu ambao sasa wamegundua matumaini waliokuwa nayo yametoeka baada ya nyota ya CCM kurudia kung'ara. Wamepoteza muelekeo hawana pa kushika.Hivyo wameamua njia hii ya uongo na kupakana matope.Bahati mbaya nayo haitasaidia kwa sababu ni uongo wa kitoto. Na wewe Bw. Michuzi usipoibandika hii kitu hapo chini nitajua kuwa na wewe ni hao hao kwani ilitoka kwenye mtandao huo huo ila mahasidi wakaminya na kukuletea ya upande mmoja tu, nawe ukaingia geji. Washindwe!
Si Mwingine ila ni mimi,
Mdau Nambari wani wa Nambari wani
1.Hadithi ya Bw.Gogo: JK hana swahiba Bagamoyo anayeitwa Gogo ambaye kanunuliwa gari ya Nissan na kuzunguka misikitini nchini kuhamasisha Waislamu kumuunga mkono JK wakati wa mchakato wa kutafuta uteuzi ndani ya CCM.Ama kweli njia ya muongo ni fupi.Mchakato ulikuwa ndani ya CCM hapakuwepo na haja ya kuzunguka misikitini.Kutafuta nini?Hakuna kura kule? Mwandishi amethibitisha asivyokuwa mwana CCM ingawaje anajifanya ni mmoja wao. Pia amethihbitisha asivyomfahamu JK.Yeye(JK) si mdini na hakuna wakati wo wote ametumia Uislamu wake kutafuta kura kabla, wakati na hata baada ya mchakato.Yuko hivyo hata sasa na atabaki hivyo kesho na kesho kutwa.
Mdau Nambari wani wa Nambari wani
1.Hadithi ya Bw.Gogo: JK hana swahiba Bagamoyo anayeitwa Gogo ambaye kanunuliwa gari ya Nissan na kuzunguka misikitini nchini kuhamasisha Waislamu kumuunga mkono JK wakati wa mchakato wa kutafuta uteuzi ndani ya CCM.Ama kweli njia ya muongo ni fupi.Mchakato ulikuwa ndani ya CCM hapakuwepo na haja ya kuzunguka misikitini.Kutafuta nini?Hakuna kura kule? Mwandishi amethibitisha asivyokuwa mwana CCM ingawaje anajifanya ni mmoja wao. Pia amethihbitisha asivyomfahamu JK.Yeye(JK) si mdini na hakuna wakati wo wote ametumia Uislamu wake kutafuta kura kabla, wakati na hata baada ya mchakato.Yuko hivyo hata sasa na atabaki hivyo kesho na kesho kutwa.
2.Kutekwa Anna Kilango: Anadai "ana ushahidi wa kuhusu Ana Kilango kutekwa ENEO LA GAIRO nje kidogo ya mji wa Morogoro,kuibiwa shilingi milioni mbili na kufanyiwa mambo mabaya." Mtu mwenye kudai kuwa na ushahidi anashangaza pale anaposhindwa kujua kuwa Gairo si nje kidogo ya mji wa Morogoro bali ni kilomita 125 kutoka Morogoro.Pia kwamba Ana Kilango hakutekwa Gairo. Kesi iliendeshwa hadharani Mahakamani asibabaishe watu kuwa anazo habari za siri za kutoa.Kama kweli anao ushahidi zaidi ya ule wa Polisi mbona hakuwapa Polisi wakati kesi inaendeshwa mpaka ikaisha zaidi ya mwaka mmoja na nusu sasa. Hata kama alishindwa kuwapata Polisi angempa habari hiyo Ana Kilango au Mzee Malecela ambao wangemshukuru sana kwani wangenufaika nayo sana kwa maana ya kesi na siasa wakati ule. Kutunga na hata kutoa uongo huo sasa hauna tija na wala hautambabaisha mtu ye yote.JK
hakuhusika na wala hakuna rafiki yake aliyehusika na tukio hilo la ujambazi.
hakuhusika na wala hakuna rafiki yake aliyehusika na tukio hilo la ujambazi.
3.Ngono na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uganda mwaka 2004: Huyu mtu anastahili kupuuzwa na kudharauliwa kwa uongo wa kijinga. Mwaka 2004 Uganda haikuwa na Waziri wa Mambo ya Nje mwanamke.Waziri alikuwa marehemu Wapakabulo na baada ya kufariki yeye akateuliwa Bw.Sam Kutesa anayeendelea mpaka sasa. Hili la JK kufanya ngono kwa siku mbili mfululizo na kushindwa kwenda mkutanoni halina msingi wowote. Rais Museveni hajaandika barua ya aina hiyo kwa sababu haikuwepo sababu ya kufanya
hivyo.
hivyo.
4.Fedha Chafu: CCM wala JK hawajapokea hata senti moja kutoka kwa Rais Joseph Kabila. Hapakuwa na haja ya kufanya hivyo. JK na CCM haijachangia hata senti tano kwenye uchaguzi wa Joseph Kabila na Chama chake. Hawajahi kuombwa na hivyo hawakuwa na sababu ya kufanya hivyo.Serikali ya Tanzania ilitoa mchango kwenye mpango wa SADC kuisaida Tume ya Uchaguzi ya DRC uliobuniwa na kuchangiwa na nchi wanachama wa SADC. Michango
iliratibiwa na ilitolewa kupitia Sekretariet ya SADC Gaborone, Botswana. Kamwe mchango huo haukupelekwa kwa mgombea ye yote binafsi, bali kwenye Tume tena kwa kuwapatia vifaa vilivyohitajika kufanikisha uchaguzi.
iliratibiwa na ilitolewa kupitia Sekretariet ya SADC Gaborone, Botswana. Kamwe mchango huo haukupelekwa kwa mgombea ye yote binafsi, bali kwenye Tume tena kwa kuwapatia vifaa vilivyohitajika kufanikisha uchaguzi.
5.Millennium Towers Hotel: Madai ya JK kuwa na swahiba yake Jack Gotham katika hoteli hiyo na kufanya vitendo vya ngono na msichana wa UDSM ni uongo mtupu.Kwanza JK hana uswahiba na Jack Gotham. Ni watu wanaofahamiana lakini si watu waliowahi kuwa pamoja wakati wo wote katika hotel hiyo kwa ajili hiyo inayodaiwa.Hawako karibu kiasi cha kufikia kufanya hayo yanayosemwa.Ni maneno ya hasidi mwenye nia mbaya tu kwa JK. Lakini hapa amechemsha.
6.Klabu karibu na Red Cross: JK hajawahi kutembelea klabu hiyo maisha yake yote.Hata yeye haijui jina kama vile ambavyo hata mwandishi haijui.Isitoshe hajawi kukaa pamoja na vijana hao katika klabu au bar au mahali pengine po pote.Hivyo basi kuhusishwa na mkutano na vijana aliowataja mwandishi katika klabu hiyo na hadithi zote zinazodaiwa kutokea kwa ajili hiyo ni mambo
yasiyokuwa na hata chembe ya ukweli.Ni mambo ya kugushi tu.Hakika mwandishi hamfahamu JK ndiyo maana amesema mambo ambayo hata mtoto anajua uongo.JK hakuwa na matembezi ya klabu wala bar yo yote hapa jijini.
yasiyokuwa na hata chembe ya ukweli.Ni mambo ya kugushi tu.Hakika mwandishi hamfahamu JK ndiyo maana amesema mambo ambayo hata mtoto anajua uongo.JK hakuwa na matembezi ya klabu wala bar yo yote hapa jijini.
7.Kuoa mke kutoka Uarabuni: JK ana mke mmoja tu Salma. Hana mke mwingine, si kutoka Uarabuni wala kwingineko. Hadithi ya kuoa mke mpya ni upuuzi mtupu. Hii ni Bongoland kama mwandishi kakutana na tapeli shauri yake.Siku nyingine akikutana nae amtake ushahidi wa ndoa. Morogoro kuna kijana kawaibia watu wengi kwa kujiita mdogo wa JK aitwaye Yusufu. Alikamatwa na sasa anatumikia kifungo.
8.Hoteli ya Serengeti: Kwa kuwa suala la kuoa mke mpya ni jambo la uongo hivyo hadithi ya JK kuchukua eneo Serengeti la kujenga hoteli kwa ubia na mke huyo si jambo la kweli.JK hajengi hoteli po pote pale.