leo nimepata heshima sio tu kutembelewa ofisini hapa dar na mzee wa busara, yusuf mahmoud a.k.a dj yusuf, bali pia kukabidhiwa kitabu cha picha kinachoelezea mambo yote ya tamasha la sauti za busara lifanyikalo kila mwezi februari ya kila mwaka kwa mwaka wa tano sasa. kitabu hiki ambacho kimeandikwa kistadi na kusheheni picha kibao za sauti za busara ni mkusanyiko wa matukio yote muhimu ya tamasha hilo ambalo limejipatia umaarufu mkubwa duniani kama 'the friendliest festival on earth'. asante sana dj yusuf na peter bennet kwa tunu hii.
kwa habari zaidi na picha za sauti za busara bofya hapa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Kabla sijasoma story yenyewe.. nikajua umetembelewa na mchawi!! Viswahili vingine bwn

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...