Mkuu wa wilaya na balozi nilikua safarini kidogo mitaa ya Peramiho nikaona nikupatie hii zawadi ya kikwangua anga cha peramiho kilichoanza kukwangua toka mwaka 1943. i think the Oldest kati ya vikwangua anga vya tanzania.Zawadi hii pia iwafikie wale wote wanaotokea maeneo hayo Mkoani Ruvuma.
Mdau na Mpenzi wa Masnep
Stewart

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 17 mpaka sasa

  1. Asante sana Mdau.

    Hii picha nimefurahia sana, nimekuwa nikisafiri na Mhashamu Askofu Msaidizi Method kilaini Katika simulizi zake za historia ya kanisa katoliki (au uinjilishaji kwa ujumla) Duniani, Afrika , na sasa tuko Tz ,na alishatupeleka (kihistoria) mpaka Peramiho. Hii picha imenifanya niamini kwamba Kweli wa Benedictine walifanya kazi.

    Asante sana.

    Mdau Kiwoso

    ReplyDelete
  2. Asante sana Mdau.

    Hii picha nimefurahia sana, nimekuwa nikisafiri na Mhashamu Askofu Msaidizi Method kilaini Katika simulizi zake za historia ya kanisa katoliki (au uinjilishaji kwa ujumla) Duniani, Afrika , na sasa tuko Tz ,na alishatupeleka (kihistoria) mpaka Peramiho. Hii picha imenifanya niamini kwamba Kweli wa Benedictine walifanya kazi.

    Asante sana.

    Mdau Kiwoso

    ReplyDelete
  3. aiseeee si mchezo kitu balaa ile noma
    kuna kikwangua anga kingine wadau kipo itengule mwakujua???maeneo ya malangali iringa uwezi amini,,oldest jengoz adi leo zaishi,chekshia sasa majengo yetu ya mitaa kati dar yavoanguka wakati yaendelea na ujenzi,,
    WIZI MTUPUUU

    ReplyDelete
  4. Daah naona hii ingeitwa peramiho twin tower tokea tunakuwa nasikia tu peramiho kumbe kumetulia itabidi siku moja niwe tourist ktk nchi yangu manake hata siijui mikoa kibao

    ReplyDelete
  5. Asante sana mdau kwa picha nzuri ya Peramiho yetu. kwa sisi tuliokulia maeneo ya jirani na hapo tunapafurahia sana na leo umenifanya nipakumbuke zaidi, ungetelemka na pale bondeni seminari kuu maarufu kama "major". Du kupitia picha hii nimemkumbuka Br. Polykarp GAMA (Polikalipi) wa kitengo cha uchapishaji bila kuwasahau marehemu Pd. Clemens na Michael OSB. Hapo palikuwa na bado pataendelea kuwa ni kimbilio la walio wengi wetu, maana hapo tunapata huduma za hospital (chini ya uongozi wa Br. Ansgar OSB na wasaidizi wake). Du, kuna mengi ya kuongelea kuhusu Peramiho lakini kwa leo naishia hapo.

    Mtoto wa Mngongoma kule Nakahuga.

    ReplyDelete
  6. mdau hapa ndo nyumbani, ni sehemu ya historia si tu ya kanisa bali hata kuwa kwamua watu katika ujinga, kwa vile ni sehemu ya kwanza kanda ya kusini kutoa kozi ya uwalimu na ufundi na hivi tunaweza kusema ni sehemu kati ya sehemu muhimu kusini mwa Tanzania.

    ReplyDelete
  7. Duh...mswahili bado anamuabudu mungu wa kizungu!!!

    ReplyDelete
  8. Du! Penye apa! bomba hii nyumba hii.

    Mdau Lizaboni.

    ReplyDelete
  9. hawa jamaa hawana lolote nasikia wezi sana hapo chini ya hiyo tower naambiwa kuna MADINI KIBAO sisi wajinga tunasali hapo juu yake na kuimba kwaya wenyewe wanadokoa kiulaini.Kwa hiyo kina tower hapo TZ tujaribu kuichunguza wao wanaona raha gani kujenga Africa? Kila kwenye kanisa (PAROKIA)KULIJENGWA STRATEGICALLY KUWAONYESHA WAJUKUU ZAO KUNA CHOCHOTE ENEO HILO HIVYO MNAKARISHA UWEKEZAJI WENZENU WANAJUA WAPI KWA KWENDA.
    Kalaga bao!
    MWONILE BAMBO KAPINGA!!!!

    ReplyDelete
  10. Karibuni Sana Wadau Ndani ya mji wa Peramiho.Ni Mji ambao umejengeka una majengo mengi ya zamani ambayo yanavutia,Una vitu Vingi sana ambavyo vinavutia...karibia ujionee mwenyewe...

    ReplyDelete
  11. PALI-PALI PENYEE PALI BWANA. UMEPATIA KABISA. HII NI ILI ILI TWIN TAWA YETU BWANA.

    Imenikumbusha tulipokuwa tukienda kununua mitumba, na kusafisha picha zetu (black and white), tukitokea Songea Boys' miaka ya 79-82.

    Nawakumbuka rafiki zangu kina
    Adoh,
    Aaron,
    Chacha Mwita,
    Ussi,
    Cuthbert,
    Apolinary,
    Marehemu Shilatu,
    Na wengineo.

    Nawatakia Christmas njema.

    Siamini kuwa ni miaka karibu 30 sasa imepita tangu tulipokuwa Box 2.

    Mdau,
    London-Paris-Tokyo (ommi_r@hotmail.com)

    ReplyDelete
  12. Duuh!mdau amenikumbusha mbali sana.Nilibatizwa na kupokea komunio ya kwanza na kipaimara katika hili kanisa.Shukrani mdau

    ReplyDelete
  13. nadhani na huu msamiati wa kikwangua anga itabidi pia nao tuambiwe maana hwenda mwengine akaleta kichuguu cha mchwa kilichoongoka nacho kikawa kikwangua anga!!!

    ReplyDelete
  14. We mtoa maoni wa novemba 28, 10.26pm una uwezo mdogo sana wa kufikiri! Unapowashangaa waswahili ambao bado wanaabudu Mungu wa kizungu, jishangae kwanza wewe kwa kutumia mashine na teknolojia ya kizungu kutoa maoni yako. Suala la kuabudu Mungu wa Kiarabu, Kizungu, Kiafrika, nk ni uamuzi wa mtu binafsi. Uwe na heshima kwa uhuru na utashi wa wenzako!

    ReplyDelete
  15. Hii picha imenikumbusha my 4 years spent at Peramiho Girls school in early 90's tulikua tunasali hapo kila siku asubuhi.

    ReplyDelete
  16. Tukuoni bambo,
    mmmhh Bwana mimi hapo ndio kwetu hospitali hii ilikuwa na huduma bomba kuliko zote tanzania at 1990's. Kuna hoteli ilikuwa inaitwa kwa deo moka alikuwa anatengeneza mikate si mchezo na chai ya maziwa. Hawa jamaa wa peramiho ni mabingwa wa kutengeneza soseji na mikate hakuna tena tanzania. Ansagar alikuwa ni rafiki sana wa baba angu mkubwa alikuwa anagawa sana mitumba na vitu mbali mbali vya msaada. Bila kuisahau Trade school ambao ndio mabingwa wa kufundisha ushonaji wa suti Tanzania nzima. Wazee suti ya peramiho si mchezo

    ReplyDelete
  17. Tunashukuru sana kwa picha hiyo nzuri ya Minara Pacha ya Peramiho. Kwa yule aliyetoa maneno ya kashfa kuhusu majengo hayo tunamsamehe kwa kuwa hata hajui chochote. Wale wazungu wemetumia nguvu zao zote na hata wanafia peramiho na wanazikwa pale pale. Europe to them is nothing than proclaiming the good news to the poor.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...