Bwana Michuzi,

Naomba kutoa dukuduku langu la moyoni kutokana na jambo linalonisibu.

Mimi ni msichana wa kiislamu (27 years old), mwajiriwa wa Benki kubwa sana hapa nchini. Bado sijaolewa. Maisha yangu ni mazuri tu na naishi mwenyewe kwenye nyumba yangu

Naipenda sana dini yangu lakini kuna kipengele kinachonikwaza. Hapa ni pale dini yangu inapofundisha kuwa muwe wangu anaweza kuoa zaidi ya mke mmoja. Sipo tayari kabisa mimi ku-share mume wangu na mwanamke mwingine yeyote yule.

Hivi majuzi kuna kijana ameanza kunifuata na anapenda tuoane. Nimegundua kwamba ananipenda kwa dhati lakini bahati mbaya ni mkristo, nami naona sipo tayari kuolewa na mkristo japo kijana anaonekana ni mtu safi sana kimaadili.

Nashindwa kuamua maisha yangu. Naogopa kuolewa na mwanamme wa kiislamu, halafu baadaye aniletee mwenzangu. Pia kijana wa kikristu siwezi kuishi naye kwani maadili yangu ya kidini hayaniruhusu.

Najikuta njia panda. ndoa naipenda, watoto nawapenda, ila vikwazo vyangu ndo hivo hapo juu. Sasa nifanyeje wapendwa?? Or Should I just continue living a single life?

Ni Mimi Kuruthumu J.M,
Mdau wa Mwanza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 92 mpaka sasa

  1. dada, chelewa chelewa utakuta mwana si wako! nani kakwambia wakristo hawaoi waisilamu, nendeni kwa area commissioner. wewe huna msimamo. embu kuwa na msimamo ndo utajua uolewe na mume gani

    ReplyDelete
    Replies
    1. If it mean to be it will be , muombe mungu akuonyeshe yupi anafaa, pia shirikisha watu wenye elimu na busara kuhusu uislam na machaguo yako. Mwenyezimuungu anasema pengine unakipenda kitu lakini sio kizur kwako na pengine unakichukia kitu lakin n kizuri kwako ,na mungu wako ndio mjuzi wa kila kitu. Kama ww n mwislam basi sali sala ya istikhara kuomba mungu akupe msaada ,utaona tu jambo lenye vikwazo sio zuri na kama ni zuri itakuwa rahisi kwako ,pia kwa ushauri wangu kwakua upo njia panda basi usiusikilize moto wako kwasababu unachagua kile unachokitaka hasa hata kama hakifai utalazimisha. So shirikisha wazazi wako na watu wa karibu watakujuza na utajua tu wapi ni sahihi na wapi si sahihi. Kuna maisha baaada ya dunia pia fikiria hilo. Asante

      Delete
  2. Wengi watoto wa kike wa kiislamu wanacomplain na sheria hiyo.Wengi ya hao hawakusoma dini ya kiislamu na kuifahamu ni kwanini sheria hiyo ipo kwenye uislamu.Ningelikushauri ukatafuta scholar wa dini ya kiislamu akakuelezea vizuri sababu za msingi za uislamu kutumia sheria hiyo ya wake 4.

    Kwa mtazamo wangu (mwanamme muislamu, lkn sio scholar wa dini), hiyo sheria ina faida nyingi na wengi watu tunaitumia vibaya.Kwa maisha ya sasa yanavyokwenda, hatuna uwezo wa kuowa wanawake zaidi ya mmoja.

    Ukinitaka nikupe baadhi ya mambo ambayo naweza kuyafikiria ni faida ya sheria hii ni:
    **Mfano couples hawapati mtoto, na tatizo limethibitika kuwa ni la mkeo.Unaweza kuitumia kuongeza mke wa pili kupata watoto.

    Zipo sababu nyingi unaweza kupewa au pengine unazijua tayari, ningelipendekeza kutafuta scholar akupe majibu ya kitaalamu.

    ReplyDelete
  3. Majibu unayo mwenyewe kuruthumu, amua kusuka au kunyoa

    ReplyDelete
  4. Dada..fuata moyo wako...mambo ya kuolewa na kuletewa wanawake wengine siyo salama kabisa kiafya...maisha yamebadilika....hili gonjwa la ukimwi si la kuletewa wanawake wengine watano...!!Halafu mapenzi hayagawanyiki..!! Mume na Mke ni wa mumoja..siyo wawili..Lol..

    ReplyDelete
  5. dada yangu wee olewa tu na yeye tote ambaye roho yako i radhi.

    Mwenyezi Mungu anawajua walio wake..yaani watu safiiiiiii.

    Dini ni nini hasa?
    baba angekuwa meskimo ungeabudu dini gani?
    Dini ndio chanzo cha ustaarabu na ndio chanzo cha ubaguzi wa kiakili na kifikra?

    Dini kwa sasa ni fikra za kila mtu yeye bnafsi.Kuna watu wanaenda kusali na kuswala kwa ushabiki na wao wakifa wazikwe kwa heshima za dini zao....TATIZO NI KWELI WANA MWABUDU MUNGU WAO KWA ROHO NA KWELI.
    kuna mafisadi,wazinzi,walafi,wafiraji,wauaji,waongo kwenye dini zote....

    ReplyDelete
  6. Mimi nakushauri uolewe aisee. Kuna message nimetumiwa hapa na jinsi ninavyoona jinsi mambo yalivyo siku hizi, suala sio dini kwa sababu wachache sana wana dini. Ninachokiona hapa muhimu ni upendo. Nakushauri uolewe na huyo jamaa yako tena umpe ushirikiano wa kutosha kabisa.

    ReplyDelete
  7. Cha kwaza kabisa kabla sijakujibu nitaomba uede katika mtandao huu www.alhidaaya.com ukaulize hili suali lako unaweza kupata jibu zuri sana pale ambalo litakuongoza. Ama mimi kwa upande wangu nakushauri ukubali kuolewa na muislamu kwani ALLAH ametueleza kuwa kuolewa na mume asiyekuwa muislamu i kujielekezea ktk shari yaani mwisho wake ni mbaya mbele ya Allah kwani maisha haya ya dunniai hayana thamani sana kwetu sisi waislamu. Ama kuhusu sheria hii ya kuoa mke zaidi ya 1 ina faida kubwa sana hususan kwa nyinyi akina dada 1) Wajae ambao wameachwa au waume zao wamefariki hupata nafac na waoi kuolewa, 2) Mke akiwa na matatizo ya kiafya 3) Mke kama i tasa na mume anahitaji watoto nk. kwa kuzitaja hapa ni chache. Kama kwlei unaupenda uislamu wako basi wala usiwaze kuolewa au kujenga urafiki na mwanaume wa kikristo kwani huwa hawatutakii kheri Allah ameshatutanabahisha. Anasema "yale waliyoyafutika kwenye vifua vyao ni makubwa kuliko wanayokudhihirishieni na kila mkipata matatizo wao nndio hufurahi".Naomba kwa elimu zaidi unaweza kunitafuta kwa namba hii 0773190110

    ReplyDelete
  8. ndugu yangu alokwambia wakristo siku hizi wanaishi na mke 1 nani???? mbona kuna wati kibao ambao ni wakristo na wanavimada(nyumba ndogo) na wapo nao zaidi ya miaka mingi tu na wana watoto nao sasa hao sio wake? pia suala la kuoa mke zaidi ya 1 lina mambo mengi kama ulivyoshauriwa hapo juu soma dini yako uielewe.

    ReplyDelete
  9. ndugu yangu alokwambia wakristo siku hizi wanaishi na mke 1 nani???? mbona kuna wati kibao ambao ni wakristo na wanavimada(nyumba ndogo) na wapo nao zaidi ya miaka mingi tu na wana watoto nao sasa hao sio wake? pia suala la kuoa mke zaidi ya 1 lina mambo mengi kama ulivyoshauriwa hapo juu soma dini yako uielewe.

    ReplyDelete
  10. Uislamu unaruhusu mwanamke kumzuia mume wake kuoa mke wa pili iwapo hayo yatakuwa mmakubaliano ya ndoa na mwanamme ataridhia hivyo hivyo huna haja ya kujuta mpe sharti hilo awali kabisa.

    Ndoa ni fungamano la hiari kumbukumbuka inapendeza zaidi iwapo atakayekuoa mna vitu vyenye kufanana na hasa dini.

    Eddy mohdsafa2004@yahoo.com

    ReplyDelete
  11. Mdada hakuna mwanaume wa KIAFRICA WA PEKE YAKO sikuhizi, FULL STOP.Kama hajaanza kutembea nje, basi ana kimdada huko ofisini wana flirt flirt, au ataanza badae, au anything of that sort, so wanaobahatika kuishi bila kushare miaka yao yote hadi kifo ni WACHACHE, na ninarudia kwa lugha ya kiingereza VERY FEW PEOPLE, and the approximation of the few i am talking about is very close to ZERO, so tunarudi palepale, we ujue tu hakuna mwanaume wa peke yako dunia ya leo.SASA mimi ni mkristo, mwanamke nimeshaolewa long time, nateseka tu na kuvumilia nyumba ndogo ya/za Mr,Sasa wewe una bahati kweli na hiyo dini yako, ninachokushauri ni uamue tu moja 1. Uolewe na muislamu mwenzio akitaka kuongeza mke anakuambia kwa heshima, unakuwa unaelewa kinachoendelea
    2.Uolewe na mkristo akutafutie msaidizi wa nje, bila wewe kujua na nduguze wawe wanajua na marafiki, we uwe unachorwa tu na kuchekwa mgongoni,hujui kinachoendelea,,halafu uwe confident ukidhani uko peke yako kumbe waliwa kisogoni, mwishoni uje uzae watoto hapo kuondoka unashindwa kufanya uamuzi, unabakia kufuga WAZIMU kama mimi hapa.
    3 NA YA MWISHO NI ukaolewe na mzungu, hata kama ni mkristo anaweza kuwa mkristo jina hafuatilii kabisa dini, utafanya mambo yoote unayoyataka ya dini yako, ukitulia utafute mzungu fresh atakupenda wewe, na hapo kwa mzungu ndo naweza kusema unaweza bahatika kwa asilimia zaidi ya 95 kumpata akawa wa kwako peke yako, wazungu waaminifu sana kwa kweli, ila ndio tofauti za tamadunin.k utavumilia huko hadi ushikwe kichaaa...pili utanyanyaswa maana unaonekana we masikini tu hata kama umetoka kufanya kazi bank, atakuweka down tu one way or another, today or tomorrow,,,ukitaka kuenjoy na mzungu uwe na job yako nzuri halafu muwe mnaishi Tanzania, mkishakuja kwenda kwao tu, mkae huko, mzae watoto utajua kwanini kuku hana meno ukianza kuhesabiwa pesa zinaisha kwenye kununua diaper za mtoto, kazi kutuma hela kwenu tanzania etc hapo wewe una kazi ya cleaning, kazi ya bank uliiacha bongo ukawaaga watu kwa mikeke,ndio utakoma kuringa....
    KAZI KWAKO MAMA , CHAGUA UNALOONA AFADHALI.

    ReplyDelete
  12. Dada kuruthumu jibu ni rahisi sana,Kwanza mimi ni Muislamu km wewe na nina umri km wako,Nimeowa mwaka jana,kwakifupi kabla ya ndoa kuna makubaliano kati ya wewe na mumeo, So mwambie kile ambacho hupendi na unachopenda.Kwa maisha ya sasa sidhani km yuko anayetaka wake 4 especially sisi vijana.Na kusema kuwa ataowa mke mwingine ni kukariri huko au kutojiamini kny ndoa. chamsingi olewa kukaa single unajidanganya kabisa kwa kuwa akili yako ulishaiweka kifamilia mpk umeamua kutuomba msaada apa wa mawazo. So mkae na mpange things are simple. welcome to our team.

    ReplyDelete
  13. Hi! Lady you dont have to worry about nothing,technology ime kuwezesha. unaweza kupata mtoto bila mwanaume. all you need is UKP(United kingdom Pound) 2000.00 you got to Span, the thy will sort you out. hapo if you wht to leave a selfish life then it will be up to you. lakini kuna tatizo jingine je hao watoto wataitwa nani? maana kunamajina Bustad/mwana halamu and so on it is up to you. life is short make most of it.

    ReplyDelete
  14. Mimi pia nikushauri ulipeleke suala lako kwa maulamaa wa dini ya kiislamu (Ustadh, imam, sheikh n.k). Watakupa faida nyingi za sheria hiyo ya kiislamu.

    ReplyDelete
  15. Maadili gani ya Dini unayoyasema wewe ambayo unafuata? Umesema unapenda kuolewa, mwenzio usingependa na yeye aolewe/apate stara kama wewe? Muislam anatakiwa awe na huruma kwa wenzie, lakini wewe yaonesha unataka upate wewe lakini wengine hapana! Wanawake mko wengi zaidi ya wanaume. Kuwa na mke zaidi ya mmoja (si lazima) kwa Muislam sababu zipo nyingi na zinaeleweka lakini Kuruthumu hutaki. Nenda kaisome vizuri Dini ya Kiislam kam wewe Muislam kweli na si wa jina tu.

    ReplyDelete
  16. Sasa dada tukupe msaada gani, wewe mwenyewe kwa hao watu wawili unajiuliza, jibu ni lako mwenyewe dada, toa uamuzi wako, wewe siyo mtoto wa miaka 18 bali una miaka 27chukua uamuzi wako mama...by now ungekuwa na watoto hata wawili.

    ReplyDelete
  17. sema kuruthumu habari za siku nyingi tangu enzi za kule MASS?,kwanza hongera kwa kupata job, nadhani kama sijakosea niwewe.
    asee nipe contact zako hapa nitakuandikia in person au nitakupigia,maana ni muda mrefu sana. istoshe mie pia natafuta mtu kama wewe ikiwezekana nije huko summer tuyamalize kabisaaa:)))
    kama niwewe p'se jibu hapa. nipe na habari za kina go east go west mathematics is the best!!nadhani kama ni wewe utanipata. au za kina jump frog frog:)))heri ya mwaka mpya!!

    ReplyDelete
  18. Nakuelewa sana Kulthum, nami nina miaka 28 na kazi yangu na kuishi mwenyewe.
    Nakushauri kuwa usali sana my dear, hakuna lisilowezekana chini ya jua.

    Mi nakuombea umpate kijana wa kiislam (si kuwa wakristo hawafai, bali ni swala la maadili)atakae kupenda na kukujali. Si wote waowaji wa wake wawili (otherwise wote tungekuwa na mama wawili)..

    Sali, muombe Mungu akujaalie anaekufaa na kumbuka mapenzi ya ghafla ni matam lakini wabidi chunguza vizuri pia.

    Kila la kheri my dear.

    Hs

    ReplyDelete
  19. Dada pole sana.
    kwanza kabisa ningekushauri uisome vizuri dini yako na uielewe. Uislamu si mgumu, ila ni sisi tunaofanya uonekane mgumu. Kama wewe ni MUUMINI wa kweli na una TAQWA, then I dont think ati utafikiria ati ukiolewa a man will go to marry another wife.
    kingine ni imani yako tu juu ya Mola wako. Kama una muamini na kumtumainia yeye... basi ask HIM and He will give you.
    Hata suala la ndoa, muombe Mungu wako akupe mume wa kheir..... mtu anaweza ku-pretend ukafikiri ni right person kumbe akawa ni wrong person.
    Ni hayo tu. Mungu akuongoze.

    ReplyDelete
  20. Mtume alioa wake 7, na sisi alituruhusu kuoa 4 maximum. Mimi nina uwezo na sababu za kuoa mpaka wanne. Kwa sasa ninao watatu. kama unaweza tuwasiliane uwe mke wangu wa 4 na wa mwisho. Mali na mambo yote aliyoainisha mtume nimeyakamilisha. Pia mimi ni scholar aliyebobea.

    ReplyDelete
  21. we dada tatizo huna malezi ya dini na si kila mwanaume wa kiislam ni lazima aoe mwanamke zaidi ya mmoja,,kuoa mwanamke zaidi ya mmoja kama dini ilivyosema inatakiwa mume amshauri mke na kuwe na sababu maalumu labda mke hazai au mgojwa hawezi kumuhimili mume.kuna waislamu wangapi unaowajua wana mke zaidi ya mmoja na kwa sababu gani?,usikubali kuolewa na mkristo kwa kuwa utakuwa unazini hakuna ndoa kati ya mkristo na muislam hiyo sio ndoa ni mkataba wa dunia.

    ReplyDelete
  22. Kwanza kabisa mimi nafikiri wewe sio muislamu halisi kama unavyojiona. Kwani kama ungekuwa muislamu halisi basi ungekubaliana na sheria zote za dini kama zinavyoelekezwa na vitabu vya kiislamu

    Hivyo basi ushauri wangu wa bure ni kwamba kwanza jiangalie mwenyewe kama kweli ni muislamu haswa. Halafu nenda mbali zaidi angalia je sheria za dini zinasemaje? Halafu jiulize tena sheria hizo unazifuata? Kama utapata jibu kuwa hufuati hizo sheria basi wewe si muislamu hivyo unaweza kuolewa na huyu jamaa wa dini ya kikristo. Kwani yeye hatakuja kuoa wanawake wawili kama yeye kweli ni mkristo.

    Pia uelewe huwezi kufunga ndoa ya Kikristo kama wewe sio mkristo. Hivyo kama unataka kuolewa na huyu mkristo itabidi ubadili dini. Kama anakuambia anaweze kukuoa bila wewe kubadili dini basi jua kabisa huyu si mkristo halisi.

    Alternative ya mwisho unaweza kufunga ndoa ya kiserikali ambao haifungamani na dini yoyote ile.

    ReplyDelete
  23. LISTEN MY DEAR KURUTHUMU.NI JAMBO LA MAANA SANA KUZINGATIA MAFUNZO YA DINI NA SHERIA ZAKE KWANI NDIYO BAADHI YA MIONGOZO MUHIMU KATIKA MAISHA YETU.
    HATA HIVYO,DINI ZOTE NI IMANI INAYOTEGEMEANA NA MTU BINAFSI PARTICULARLY ANAPOKUWA AMETIMIZA UMRI WA HUTU UZIMA KWA MAANA KWAMBA ANAWEZA AKAFANYA MAAMUZI YAKE, AMBAYO KIMSINGI YANASTAILI KUHESHIMIWA.BABU ZETU HAWAKUZALIWA WAISLAMU WALA WAKRISTO ISIPOKUWA, BAADA YA HIZI DINI KULETWA NA WAZUNGU NA WAARABU, BASI WALIACHA DINI ZAO ZA KUABUDU MIZIMWI NA HIZO NJIA NYINGINEZO ZILIZOKUWA ZIKITUMIKA NA KUWA EIDHA WAISLAM AU WAKRISTO IKITEGEMEANA NA MAAMUZI YAO KAMA WATU WAZIMA, MAAMUZI AMBAYO HATA SISI TUMEYARITHI, NA NDIYO MAANA WEWE MWISLAM MIMI MKRISTO FULANI MBUDHA NK.
    KWA MAANA HIYO, HATA WEWE UNA HAKI MBELE ZA MUNGU, KUCHAGUA IMANI YAKO NA UAMUZI WAKO UKAHESHIMIWA.
    USHAURI: KAMA UMEMPENDA KWA DHATI NA AMEKUPENDA KWA THATI,BASI CHUKUA MSIMAMO, OLEWA KWANI NAAMINI HATA MWENYEZI MUNGU HAWEZI AKABAGUA KWA MISINGI YA KIDINI WANADAMU WOTE NI SAWA MBELE ZAKE NA KILICHO MUHIMU NI IMANI YAKO.

    ReplyDelete
  24. tueleze tu kuwa labda wewe ni msa..... Lakini usisingizie dini kwani hata ukristo unaruhusu wake zaidi ya mmoja.Soma vitabu vya manabii utakuta Ibrahim alikua na wake Sara,Hajer na ukisoma pia agano la kale utakuta Suleiman akawa na wake 900 wamwisho akiitwa BI KETHURA sasa sijui unachokiogopa nini,Mfano wa karibu wa wakristo walooa wake wengi angalia marais wa kiafrika tu.Kama vipi bakia tujipigie pigie bila kuoa.Mdau Uk

    ReplyDelete
  25. dada kuluthumu usiituhumu dini yako kama huelewi sheria zimesimama vipi na jinsi gani sheria hiyo inapaswa kutekelezwa.
    Mr Froasty kaelezea vizuri ila kwa kuongezea kwa maadili halisi haimpaswi mume kuoa mke wa pili bila kupata ridhaa kutoka kwa waifu wake.
    hivyo kuletewa mke mwenza kwa misingi ya dini ni makubaliano kati ya wewe na mumeo.
    vile vile misingi yake ni kwamba haki lazima itendeke sawa kwa wake zote, kila unachopata wewe basi na mwenzio apate ili mradi manumg'uniko ysiwepo ndani ya familia. kama yakiwepo basi misingi ya sheria hiyo haipo tena hapo !
    kwa mwelezo zaidi tembelea
    islam.road2us.com upate mafundisho ya dini!
    wasalaam!

    ReplyDelete
  26. KURUTHUMU SIONI KAMA SHERIA HII NI KIKWAZO SANA CHA WEWE KUOLEWA.

    KWANZA KABISA INABIDI UFANYE UAMUZI WA KUOLEWA AU KUBAKI SINGLE.

    SASA KAMA UAMUZI NI KUOLEWA BASI MIMI NADHANI HUYO WA DINI YAKO ATAKUFAA ZAIDI.

    ILA UMUELEZE KWA UWAZI KABISA TANGU MWANZO YA KUWA PAMOJA NA KWAMBA SHERIA INAMRUHUSU KUOA ZAIDI YA MKE MMOJA WEWE HUKUBALI KU-SHARE BWANA NA MKE MWINGINE.

    MCHUMBA WAKO AKIRIDHIA BASI POA HUYO NDIYE BWANA YAKO.

    JAPO HIYO HAITAKUSADIA SANA. BWANA ANAWEZA AKAWA NA MKE MMOJA HALAFU AKAISHI KAMA DAMIAN. KAZI KWELI KWELI, LAKINI YOTE MAISHA.

    ReplyDelete
  27. Kuruthum unaolewa na mtu uliyempenda rohoni na yeye anakupenda rohoni sio wa dini gani,dini ni utaritibu tuu wa maisha lakini ndani ya ndoa unaishi na mapenzi kwanza. Usiolewe na mtu tu kwa kuwa ni mwislam wakati mapenzi ni ya wasiwasi wala hayajakamilika, ndoa ni mapenzi usikilize moyo wako.

    ReplyDelete
  28. Kulthum,

    Mi nionavyo kama nia yako ni kuolewa na muislamu mwenzako, hicho kipengele cha wake wanne kisikupe shida. Cha muhimu ni kuweka msimamo wako wazi kabla ya ndoa ili mwenzako ajue. Mimi niko kwenye ndoa ya kiislamu kwa miaka 14 sasa, na ni ndoa ya mke mmoja kwa vile hili tuliliweka wazi mwanzoni na tukakubaliana.
    Uelewe pia kuwa mwanamme kuwa wa dini fulani sio kigezo kikubwa cha yeye kuamua kuwa na mke/mwanamke mmoja ama wengi kwani kama mtu ana nia ya kuwa na wake/wanawake wengi anaweza kufanya hivyo akiamua tu ama kwa kutumia hicho kipengele cha dini, ama hata kuwa na nyumba ndogo endapo dini hairuhusu. Kuna mifano mingi tu ya watu ambao ndoa zao ni za mke mmoja lakini ziko matatani kwa ajili ya nyumba ndogo. Kwa upande fulani you take chances kwa kuamini kuwa mwenzako anajua msimamo wako ukoje na kuwa hatakuja kubadilika. Na hasa jitahidi kuielewa vizuri tabia ya mwenzako kabla ya kuingia katika ndoa, kwani hiyo ndio kwa kiwango muhimu ita-determine tabia yake kwenye ndoa.

    ReplyDelete
  29. Inaonyesha si msichana wa kiislamu mwenye kuijua dini yake na kufuata maadili ya dini. Kama wewe ni muislam kweli na si muislam wa jina kwa sababu tu umekuta wazee wako ni waislam usingeuliza swali la kipuuzi humu bloguni. Ungelifahamu vilivyo misingi ya dini yako, Imani yako ingekuwa thabitim na ungelikuwa pia unavaa hijabu, na sidhani kama ungekuwa na wasi wasi na suala zima la ndoa yako.

    Swali kwako, ni ndoa ngapi za waislam zina mke zaidi ya mmoja? Ni zote au?

    Ni ndoa ngapi za kimila zina mke zaidi ya mmoja?

    Na ni ndoa ngapi za kikikristo zenye mke mmoja lakini kuna mke pembeni aambiwa kaolewa kimila au ni kimada.

    Nafikiri ukipata majibu ya maswali hapo juu hutakuwa na maswali ya kipuuzi yenye lengo la kuudhalilisha uislam.

    Mimi ni mwanamke wa kiislam, mimi na mume wangu wote ni wachamungu na tuko kwenye ndoa ya mume mmoja na mke mmoja karibu mwaka wa ishirini sasa. Na ndoa ya mke zaidi ya mmoja sio ibada wala lazima katika uislam.

    Nahisi aliyetuma hili swali si muislam, na kama ni muislam basi ni wale waislam wetu wa majina wasiotaka kujifunza dini wala kuifuata, lau ungelijifunza dini, ndoa, haki za mume kwa mke, na haki za mke kwa mume, usingelikuja humu. Pili usingelikaa miaka yote hiyo mpaka unafika miaka 27 huna mume, kwani katika uislam mwanamke anaruhusiwa pia kuposa, ungelikwisha peleka posa kwa mwanamume umtakae kupitia Imam wako wa msikitini. Na usingelikuwa na wasi wasi wa kuogopa kuolewa kwa sababu ungeliogopa kufanya zinaa!!

    Kama ni kweli ni binti wa kiislam na si katika kutaka tu kudhalilisha wanawake wa kiislam na uislam kwa ujumla na una shida kweli, basi ninakuombea kwa Mwenyezi mungu akupe ufunuo wa ilmu ili hayo madhila yakutoke na moyo wako ujae iman thabiti ya dini. Lakini kama si muislam umetumie tu kwa lengo nililotaja hapo juu basi Inshaallah Mwenyezimungu atakupa ujira wako hapa hapa duniani.

    ReplyDelete
  30. Wewe dada unajichanganya,kwani unamaanisha kwamba wakristu hawataenda mbinguni?wewe ingawa ulisoma au unafanya kazi nzuli bado nimshamba wa kufikilia.Ndoa ni kitu cha muhimu maishani mwako.Mimi ni muislamu lakini nakushauli kama huyu kaka mkristu umempemda na yeye akakupenda kapime damu tu muoane.Jali sana yule utakaeishi naye au ubavu wako tu! sio ujali dini,,kwasababu dini halitafikisha mtu mbinguni.Nikufuata maandiko tu.

    ReplyDelete
  31. dada mimi nakupa namba yangu kupitia michuzi naomba tuonane mimi ni mtu wa mwanza pia muislam na nina Masters in internationa; security na ninafanya kazi hapa dar tafadhali muombe michuzi details zangu au nipe zako

    ReplyDelete
  32. Hongera kwa kazi nzuri na jumba kubwaaaaa!!!! la kuishi Bibi,mjomba.....hawapo?uishi nao
    mume huna shida nae...........na ndoa ni ibada katika uislam na sio kama kupanga glass kwenye kabati!!!!!
    Mcha mungu ndio mume bora.

    ReplyDelete
  33. Hivi kuruthum aliyekudanganya kwamba wanaume wetu wa kikristo hawaongezi wake ni nani?? kwa taarifa yako chunguza zaidi nyumba ndogo zilivyojaa mitaani na wala hakuna dalili za kupungua,cha msingi ni kumuomba mola akuepushe na mwanaume usiyemtaka na hata huyo musilam akiamua kuongeza si unaondoka tu

    ReplyDelete
  34. Tena waume zetu wakikristu wanaongoza kwa kutuzunguka na nyumba ndogo na mitoto za zinaa, bora huko kwenu kuna talaka takikushinda unabeba vyako

    ReplyDelete
  35. Binti, pole sana kwa hiyo dilema inayokukabili.Binafsi nimekuelewa sana na tatizo lako lina maana sana si jambo la kuliamua kwa pupa kama wengine hapo juu wanavyosema na ndiyo maana umekuja hapa ili upate msaada wa maana.

    Ushauri wangu katika jambo lako ni huu:

    Kwanza mimi nikiwa mkristo sitaweza kuoa mwislamu hata kama nampenda kwa sababu ukioana na mtu uliye tofauti naye kiimani hamuishi mkaishiana hata siku moja ndani ya ndoa na kujenga familia.Ukifanya hivyo utakuwa umejiletea shida iliyo wazi kabisa kukusakama katika ndoa ya familia kwa ujumla.Vinginevyo uamue mapema kwamba unahama dini au anahama dini kujiunga nawe.Pia ni muhimu nuwe mwangalifu wengi wameamua hivyo hasa wanaume kuwafuata wanawake kuingia uislamu lakini baada ya kumpata kimwana wamegeuka wengine kabisa.Kwa hiyo dada usidanganyike katika hilo ndoa itakuwa ya mashaka mno ukiolewa na mtu wa dini tofauti na wewe.Katika maisha ya ndoa na kifamilia kwa ujumla, dini inachukua nafasi ya kwanza kabisa kuliko kitu kingine, ndiyo nguzo ya maisha yenu na dira ya maisha ya uadilifu wakati wowote, kwa hiyo kama dini zenu zitakuwa tofauti utakuwa umejiingiza kwenye mkenge.

    Kuhusu kuolewa na mwislamu ambaye anaruhusiwa kuoa zaidi ya mke mmoja.Mimi siyo Mwislamu, lakini nadhani naungana na msimamo wako kwamba hupendi kuchangia mume.Kwa maisha ya sasa ningekubaliana nawe kabisaaaaaa.Lakini sidhani kama Waislamu wote wanaoa wake zaidi ya mmoja.Bila shaka ni wachache, na zaidi labda ni watu rika kubwa yaani wazee, vijana wa siku hizi ni waelewa sana hasa kuhusu maisha ya sasa na madhara ya kulundika wanawake wengi na kasheshe zake. Mimi nakushauri uendelee kwanza kuvinjali kumpata Mwislamu mwenzako,kijana mwenye msimamo kama wako pia, kuna hata wakristo ambao wanaoa zaidi ya mke mmoja licha ya dini zao kukataza wakikengeuka huacha hata dini.Ukipata muda wa kutosha kuwaelewa vijana wanaokuja kwako kukuzengea utamjua nani kijana ana msimamo huo na ni vema uwe wazi.Ninalojua wengi wanaweza kutaka kuoa mke mwingine kwa sababu ya kutoelewana, lakini kama kutakuwa na maelewano katika ndoa hakuna kijana wa siku hizi atake wake zaidi ya mmoja.Tulia dada yangu na weka umakini wako.Misimamo yako ni mizuri sana mtu asikudanganye hapa.Maisha unaweza kuyajenga au kuyabomoa mwenyewe.Hivyo umakini wako huo ni muhimu mno.Kila la heri.

    ReplyDelete
  36. weka tangazo natafuta Mwanaume Muislam,then weka masharti unataka.akikubaliana na masharti yako basi mnaweza oana.tafuta ambae kipato mnalingana hiyo Ndiyo solution

    ReplyDelete
  37. Kwanza Asalaam aleikum Bi Kuluthumu(nafikiri jina lako lisomeka Kuluthum na sio Kuruthumu kwani ukiandika hivyo linaleta maana tofaui kilugha, Kuluthumu ni mibonyeo ya midomo wazungu huita Dimples)
    Kuhusu suala lako , Waisilamu wamefundishwa kumuomba Mola Ushauri pindi wanapopata suala nyet la kimaisha hususan kuoa au kuolewa.Jambo lako kwanza haliingi katika miizani ya Istikhara , kwani Shariah ishapiga pande suala la ndoa bainaya Muisilamu na asiyekuwa Musilamu na sababu zinaeleweka kama wewe mwenye unavyodai huwezi kuolewa na mtu asiyekuwa Musilamu.
    Kisheriah unaweza kuwekeana mkataba na mumeo mtarajiwa Muisilamu asiooe mke wa pili ila kwa sababu za Kisheriah kama kutopata mtoto na zinginezo kama alivyoainisha msemaji hapo juu.
    Vyema ukijifunza dini yako na suala la ndoa za serikalini zina matatizo yake.
    Dini ni suala nyeti na haliendeshwi kwa jazba wala matramanio ya nafsi.Epukana na huyo kijana japokuwa ni mzuri au ana kipato au ana elimu , chunga dini yako.Jiunge na ukurasa wa mafunzo ya Kiisilamu kwa Kiswahili yahoo group iitwayo jifunze uisilamu na pia tembelea ukurasa wa www.Alhidaya.com utapata masuluhisho ya masuala yako mengi kabisa ya kidini na dunia yako.
    Mimi mpendwa
    Halima(Mama Mawahib)

    ReplyDelete
  38. aya no 3 ktk sura nisaa inaelezea vizuri kuhusu kuoa wake 4 tafuta mtu akutafsirie vizuri na kwa binti wa kiislam hairuhusiwi kuolewa na mkristo mapaka asilimu

    ReplyDelete
  39. KWA MTAJI HUU HUWEZI KUPATA MCHUMBA UNAYEMTAKA KWA KUWA VIGEZO ULIVYOWEKA SANA SANA NAKUSHAURI UENDELEE KUWA SINGLE,PATA MTOTO AU WATOTO WAKO WASIO NA BABA SAFI KABISA HATA MIMI UKINIOMBA NITAKUPATIA BURE UMRI WANGU NI MIAKA 49 FEDHA NINAZO NINA BIASHARA NZURI TU ZA KIMATAIFA

    ReplyDelete
  40. ninafurahia sana wachokonozi au watafiti wa mitazamo ya kijamii kama hawa. kwa hakika hii inaonesha jinsi wabantu kama sio wabongo pekee tulivyochanganyikiwa na kwa nini tutaendelea kuwa masikini wa kiuchumi na kiroho. hizi dini za wazungu na waarabu zilipandikizwa afrika kama mbegu za bangi - kuwavuruga akili kama inavyojidhihisha katika maoni haya. kwani mababu zetu walio au waliolewa na nani kabla ya bangi hizi kupandikizwa barani afrika?

    ReplyDelete
  41. Umekufuru tayari unapinga aya za M Mungu?. unatoa fatwa zako?.
    Nenda dip ndani ya dini, maslahi ya dunia hayana mpango, waumini yetu akhera mali yako na kazi yako haijakupa raha mpaka sasa hivi. na bado unathubutu ku "eti takaa single" unajua hukumu yake.
    Tubu haraka na tena soma vitabu, waislam si mpaka uwe na padri au shekhe akutoshe ili uabudu. kuwa Muumini halisi sio tu kuwa mimi Muislam.
    Nadhani Bidada si muislam lakini kakupa busara nzuri sana.

    ReplyDelete
  42. Kaa mwenyewe.

    ReplyDelete
  43. Dada sikiliza, mwanaume kuoa au kutooa mke wa pili au wa nne itategemea we mwenyewe utakavyohandle ya maarriage,nasema hivi kwa sababu ukweli ni kwamba hakuna mwanaume anayetaka kuwa na wake zaidi ya mmoja kama hakuna sababu ya kufanya hivyo ila siku hizi madad zetu mmekuwa viburi,jeuri nk sasa mwanaume hataki kukuacha ila ili akwepe hayo yote inabidi atafute pa kutuliza moyo wake.Wewe nafikiri ushaona kuna wanaume ambao wanarudi majumbani kwao mara tu baada ya kutoka kazini na wengine huchelewa kurudi au hataki kuspend time na mke wake jiulize kwa nini?Wakristo wangapi wangapi wana mke mmoja lakini anarudi nyumbani saa nane usiku?Kwa hiyo dada jiulize upo tayari kumpa mmeo utulivu wa moyo?kama uko tayari basi hutakuwa na shaka kwamba utaletewa mke mwenza lakini kama ni kiburi na umejaza ujauri hata ukiolewa na mzungu utakuwa unatwanga maji kwenye kinu

    ReplyDelete
  44. utamaduni wa kikwetu tanzania kisheria unaruhusiwa kuoa au kuolewa na mtu wa dini yeyote ile. tuna tofauti za imani lakini sie sote ni ndugu. hamna Mtu anayeweza kubadili sheria za kidini lkn mambo mengine Mungu anatusamehe..tafuta mnaependana dada ndo kitakachodumisha ndoa yako.WAKRISTO WAISLAMU SOTE NI NDUGU. mdau Holland

    ReplyDelete
  45. Mungu ni mmoja, ametuumba binadamu wote sawa – dini isiwe kitu cha kututengenisha, kama kuna mapenzi hakuna ukuta wa taifa au kabila.
    Mimi ni Muislam nimeoa Mkristo – ndoa yetu ni zaidi ya miaka 15 – mimi nehishimu dini yake na yeye anaisheshimu yangu. Kama mmoja wa mpenzi anataka kubadilisha dini ni uamuzi wake wa binafsi. Kubaliana kwanza kama dini haitakuwa ni issue kati yenu – ndoa mnaweza kufunga serikalini sio lazima ifanywe kwa dini. Kama dini bado ni kikwazo sana kwako, basi endelea kutafuta kijana wa dini yako na huyo vile umuambie mbeleni kuwa hutaki aoe mke wa pili.

    ReplyDelete
  46. ALHAJ ABUBAKARYDecember 28, 2009

    BIBIE KURUTHUMU SWALI LAKO LOTE LIMESHAJIBIWA NA SURAT AL NISAA KABLA HATA HUJAZALIWA KWA MAANA HIYO MWENYEZI MUNGU AKISEMA HAKUNA WA KUMPONGA KWANI YEYE NDIYE ANAYETUJUWA SANA SISI KULIKO HATA TUNAVYOJIJUWA WENYEWE, KWA KIFUPI OLEWA NA KIJANA WA KIISLA MMWENZIO VINGINEVYO UNAJITAFUTIA MATATIZO AMBAYO UTASHINDWA KUYATATUA.

    ReplyDelete
  47. Sista KUlthum haupo sawa. Unahitaji mtu atakae kusaidia kisaikolojia maana na hisi hilo ndilo tatizo uliokua nalo.

    Dini haiwezi kubadilika kwa ajili yako hata kidogo. Swali mama yako ni mke wa ngapi kwa baba yako?? Ningependelea unijibu. Nahisi hilo swala lako litakua limejijibu.

    ReplyDelete
  48. Well I think you don't even know people very good! Who told u a muslim MUST marry four women. I am a muslim and i have one wife ten years now. Another thing I dont even think of marrying a second wife. What u have to do is look for a good Muslim man who loves u for real. Jumping to other religion will complicate ur life more. But at the end of the day it's ur decision!! Choose wisely!

    ReplyDelete
  49. HAHAHA!! KUNA MTU ANAJIITA BIDADA HAPO JUU ANACHEKESHA SANA,ETI WAZUNGU NI WAAMINIFU SANA,NILIKUWA NA MAWAZO KAMA YAKO ZAMANI,nimeishi na wazungu miaka zaidi ya 15 ndani ya nchi zao,wa hali tofauti za vipato,mtu asikudanganye!! wasifu wazungu kwa mengine lakini mimi na wazungu hunidanganyi kitu nawafahamu A-Z, maana nimekuwa nao marafiki wa kike kwa wakiume so just leave it the way it is kama huwajui!ama labda nawewe kinalia kitu huku unajifariji,au umebahatisha tu kama KURUTHUMU anavyoweza pia bahatisha mwafrika muaminifu. si mzungu si mhindi mwarabu wala mchina hilo nakuhakikishia BIDADA.

    ReplyDelete
  50. dah kweli hii ni baaab kubwa sasa hawa waungwana wanaoelezea faida ya mume kuwa na wake wengi kuwa ni kupata watoto kama mke ana matatizo ya kiafya na pia wajane kupata fursa ya kuolewa sasa nina swali JE KAMA MUME AKIWA HAWEZI KUMPA MIMBA MKEWE,AU ANA MATATIZO KIAFYA ATAKUBALI MKEWE AONGEZE MUME MWINGINE? NA PIA HAMUONI KUWA MKE NAE ANAWEZA KUONGEZA MUME ILI KUTOA FURSA KWA MUME ALIYEFIWA NA MKEWE KUOA?

    ReplyDelete
  51. TATIZO LINGINE UMELISAHAU!!

    WSLAMU HUTALIKI LAKINI WAKRISTO "HAIFUNGULIWI DUNIANI"

    ReplyDelete
  52. Mi naona huyu dada kaanza uzushi labda kaachwa na mtu mbaye alikuwa anataka kumuoa inawezekana alifanya Miujinga fulani akakosa mume, ndio maana anatumia trik ya kutafuta ushauri,kwa ushauri wangu wewe dada nenda ukaonane na wakuu wa dini zote mbili kisha kaa chini utafakari wapi pakwenda maana, vinginevyo waweza kuchanganyikiwa na kuwa mwendawazimu!

    NI mimi Juma!

    ReplyDelete
  53. Dada pole sana.

    Kwanza: Simjui hata muislamu mmoja mwenye umri chini ya miaka 40 mwenye wake wawili.

    Pili: Simjui hata mwanamme mmoja, mkiristo au muislamu aliyeoa lakini nje hana kimada.

    Tatu: Ukiristo haukatazi kuoa wake wawili. (Sitaki ligi najua mpo mtakaosema kwamba ukiristo unakataza, lakini ni uzungu ndiyo unaokataza, kwenye biblia hakuna andiko linalokataza)

    Nne: Kama umempenda mshikaji wewe anguka naye tuu mambo ya dini yatakuzingua tuu.

    ReplyDelete
  54. Kuruthumu yaelekea humpendi vya kutosha huyo mwanaume wa Kikristo. Kama unampenda vya kutosha tofauti za dini zisingekuwa kikwazo. Wakati wowote unapofikiria Ukristo na Uislamu ukumbuke kwamba imani hizo zilitokea Mashariki ya Kati, sio Afrika. Hazipaswi kuwa kitu cha kututenganisha Waswahili hata siku moja.

    ReplyDelete
  55. Kutokana na suala lako hukuuliza kwa misingi ya kidini, kwa sabau dini ya kiislamu inaruhusu mke zaidi ya mmoja lakini kuna taratibu na sheria ambazo zifuatwe. Sasa mimi nataka kukupa ushauri wa kimaumbile tu, Waislamu wanaonekana kuoa mke zaidi ya mmoja na wake wote kuwa na usawa katika masuala yote kwa mume wao, wasiokuwa waislamu pamoja na baadhi ya waislamu huoa mke mmoja tu na kuwa na wanawake wengi wa nje ambo hupewa hadhi kubwa na wanaume zao ukizingita pia wanawake hao huwa na wanaume wengi pia kwa kuwa wako huru (hawajaolewa) sasa pointi sio uislamu au ukristo, suala ni nani wa kukaa na wewe tu bila ya kimada au mke mwenza? nafikiri uoelewe na Mitume tu. Wafuasi ni zito kwa hilo.

    ReplyDelete
  56. KWANZA NANI SIKU HIZI ANAOWA WAKE ZAIDI YA MMOJA, SHIDA YOTE YA NINI, HUO SI UCHIZI TU!!!! NA KUOWANA NA MTU WA DINI YAKO TU NI MAMBO YA ZAMANI/YA KIKALE SANA YAMEPITWA NA MUDA, UNAWEZA KUOLEWA NA MTU YOYOTE YULE MKRISTO, MUISLAMU AU HATA ASIYE NA DINI KWA MKUU WA WILAYA NDOA YA SERIKALI DINI NI NINI? NANI KENDA KARUDI NA KUTUELEZA JUU YA MASWALA YA DINI NI UZUSHI TU WA WATU WA KALE TUNAUFUATA KWA VILE TUMEKUTA WAZAZI WETU WAKO HUKO WANAUFUATA WASINGEKUWA HUKO TUSINGEKUWA WATU WA DINI, PAMOJA NA YOTE HAYO UNAWEZA KUANDIKIANA KATIKA MKATABA WENU WA NDOA KWAMBA NDOA YETU NI YA MKE MMOJA NA MME MMOJA, ITAVUNJIKA PALE MMOJA KATI YETU ANAPOTAKA KUOA AU KUOLEWA NA MTU MWINGINE, KUNA WATU HAPA WANASEMA ETI KUNA FAIDA YA WAKE WENGI ETI MKE AKIWA TASA AU KAMA ANAUMWA KUWE NA MWINGINE WA KUSAIDIA, HIVI HUKU KUUMWA AU UTASA NI MKE TU MUME HAWEZI KUWA TASA AU KUUMWA SASA MBONA WANAWAKE HAWARUHUSIWI KUOLEWA NA WAUME WENGI!!! HII SHERIA IMEPITWA NA WAKATI NA NI YA KIKWARE/MFUMO DUME HAIFAI NI YA UONEZI NA UKANDAMIZAJI WA WANAWAKE. DADA UNAWEZA KUOLEWA NA MTU YOYOTE UMTAKAYE ACHANA NA MAMBO/MASWALA YA DINI

    ReplyDelete
  57. ASSALAM ALAYIKUM SWITIE,nice to here from you its great that you are so open minded,I want t tell you dear read and read about Uislam,make sure you know it,you are eduacate you have a nice job But I am afraid you dont spend much to educate yourself about your own religion,you should know a muslim man is allowed to marry more than one wife not for leisure,there reasons very strong reasons which he has to discuss with you and you must agree,if you dont he is not allowed to do it.so my advice to you sister learn about your religion and know your rights as a woman in Islam,as somebody said above there you might get a christian who will also have many mistresses without you knwng while if you get a religious man who is muslim GOD FEARING HE WILL OBEY AND NOT DECEIVE YOU.So the point is not a man who looks decent to you a point is a man who is GOD fearing and follow his religion,please be carefully,and always remember life after and a good husband some one is given by GOD.feel free to contact more am soon coming to mwanza would like to meet you here my mail zkapemba@yahoo.com,please write shukran MAY ALLAH SHOW YOU THE WAY.

    ReplyDelete
  58. kuluthum,huna imani ya dini.ungeisoma au ukaeleweshwa yaliyo kwenye kitabu,usingethubutu hata kuandika hoja yako.

    ReplyDelete
  59. my sis ndoa inaweza kuvunjika any time but Allah yupo milele na milele kwa kumtii mwanamme ukamkera mungu wako mimi sikushauriii usihadaikee na mapenzi ya sasa beleive me yatapunguwa kila siku zikendaa
    na unapofanyaa jambo fikiria future ya watoto wako watakuwa a malezi na tabia ya dini zipi itafika wakati watoto watataka kuchagua njia ya kwendaa na itazushaaa zogo familia nzimaa kuna case nyingii tuu tumeziona na mfano kuna mtoto anaitwa adams qatar now kuna fight btn ubabani na umamani angalia news
    kuna mtu hapo juu kasema dini zimeletwa na wakoloni mbonaa tunazifata wakoloni ndoo walotufunzaa ustarabuu before tulikuwa tunaishii km wanyama
    ndo maana leo tukawezaa kuandikaa hizi comments hapa kwa product za kikoloni km si wakolonii kiswahili kisingekuwa na mwandikoo huu ambao tunatumiaa tumetayarishiwa na waoo mbona hatujaupingaa

    ReplyDelete
  60. Dada yangu kwanza hujiamini na sheri aza dini yako,pili kabla ya adhabu ya Mungu, utajiadhibu mwenyewe hapa hapa duniani, kwani pande zote mbili kama wazazi zina haki kwa watoto, kama wewe ni muislam utapenda kizazi chako kiwe kufuate wewe na huyo mwenye dini nyngine nae atapenda kuwa na wafuasi kati kizazi chake, kama kweli unamsimaamo na dini yako na uanauchungu lazima utataka kizazi chako kikufuate wewe, sasa uko tayari kupanda ngano ukavuna pumba? icho kitakuadhibu hapa duniani kwa kutokukosa raha na kizazi chako ikiwa hasa una uchungu na dini yako, utakapokuwa namentality za kuwa watoto wataamuwa wenyewe wanakotaka bado huja wa na uchungu na dini yako, na Mungu anakusubiri, kawani tumeambiwa tuowane tuzaane ili mtume wetu asikie ufahari kwa umma wake kuwa mkubwa, nani watakaouongeza kuwa mkubwa ni waislam, ukiolewa na mkisto umeongeza umepunguza? na umekwenda kinyume na dini yako, Mungu akusitiri na akunusuru nahilo, isome dini, au ingia alhidaya mdau mwengine alivyokueleza utapata manufaa mengi

    ReplyDelete
  61. ndugu kulthum ama nashukuru kwa kutaka kupata maoni hakika e-mail haitoshi lakini ukweli wa mambo siku hizi huwezi kusema wakristo wana mke mmoja au waislamu maana wote ni binadamu na dhaifu sana. cha kufanya naomba nitumie sms katika simu yangu number 00971505623298 niko dubai nategemea kuja bongo kunako uzima on leave 5/1/2010 shukrani

    ReplyDelete
  62. Dada yangu wa Kiislam - kwanza kabisa ikiwa wewe muislam kweli basi uijuwe dini yako na Mola wako ameamrisha nini,na hasa imeamrishwa nini kuhusu jambo la ndoa za halali. Muislam huolewa na Muislam mwenzako. Ukiwa wewe utaolewa na mtu ambaye si mwislam basi ujuwe unakwenda kinyume na dini yako ya kiislam. Dini ya kiislam haikuteremshwa kwa watu wa midlle east (mashariki ya kiti tu) bali imeteremshwa kwa watu wote hapa ulimwenguni. Mtoa maoni mmoja anakwambia kuhusu maadili ya waafrika na ya mashariki ya kati hayo hayaingiliani kabisa na dini. Yeye nafikiri mentality yake anafikiri imekuja kwa watu wa mashariki ya kati tu.Dini ya Kislaam imekuja kwa watu wote. Na yeye huyo mkristo kama anakupenda kweli mwambie asilimu kwanza kabla ya kukuoa. Usidanganyike na dunia dada. Hayo yote ni mapambo tu ya dunia. Fata dini yako inataka nini. Hivi ndivyo watu wengi wanakuwa wanakosea hapa kwetu Tanzania kuhusu ndoa. Inakuwa wanajifnayia mambo kinyume cha dini ya kiislam hasa katika mambo ya ndoa. Kama hukuolewa duniani utaolewa peponi. Basi usisikie ya watu kaa na dini yako na utapata mchumba wa kislam. Na sote tunakuombea dua upate Mume mwenye dini yake ya kiislamu. Ndugu yako katika uislam.

    ReplyDelete
  63. "Kwa bahati mbaya ni mkristo" are you joking me? aliyekwambia ni bahati mbaya nani? Umeitoa katika aya gani hiyo habari?

    Utaishia kunawa !!!!!!!

    ReplyDelete
  64. Dada yangu katika uislam, once unapodeclare kuwa wewe ni muislam

    kwanza huna hiari juu ya sheria aliyoiteremsha Allah

    Pili usihoji uhalali au uzuri wa maneno ya mtume wa Mungu

    Uislam haukutakii mabaya, yote ni mazuri ikiwa wewe unajua

    Achana na huyo mkristo, kwani itakuwa umekwenda kinyume.

    Allah akupe moyo Mwepesi na akupe mume mwema miongoni mwa waumini.

    Maasalama

    ReplyDelete
  65. Dada Kuitwa Kuruthum haina maana kuwa wewe ni muislam kwa maelezo uliyoyatoa tafsiri yake ni kwamba wewe si muislam.
    Endelea na unungayembe wako, gawa uroda kama njugu, Mzinzi mkubwa we na usiutukane uislam kwa kutokuuelewa kwako.

    ReplyDelete
  66. Asalaam aleikhum Kulthum.
    Umepata ushauri mwingi sana, kitu cha muhimu sasa ni kutumia akili yako kuuchambua ili ufikie uamuzi ulio sahihi na wenye manufaa kwako, mmeo na familia yako kwa ujumla . hatua zote za maisha tangu kuzaliwa mpaka kufa zina mazuri na mabaya yake, zina furaha na machungu yake. Bahati nzuri kwa hili liko ndani ya uamuzi wa busara zako, jitahidi ufuate njia aliyonyooka. Mtoa maoni wa Tarehe Tue Dec 29, 12:45:00 AM ameongea vitu vya maana sana ila anavyoomba kuonana na wewe ndo nashangaa kidogo!! Jukwaa la maoni NI HAPA.
    Ni vema ukapata mme ambaye mna imani moja na ambaye utaweza kuelewana naye na kupendana naye kwa dhati.
    Naamini Mme wako anaweza kupata kila kitu toka kwako na asihitaji mke wa pili wala wa nne. Mimi mwenyewe ni kijana wa Kiislam but I have never thought of being Polygamous, na ata kama ikitokea mme wako akaoa mke wa pili (kwa kufuata misngi ya Dini ambayo ni lazima apate ridhaa yako) ni vema pia kwani atakuwa ni mke anayetambulika kisheria tofauti na kukimbilia kwa Mkirito na akawa na vi Concubine vya kutosha huko uchochoroni! itakwa hatari zaidi dada yangu.
    CHOOSE WISELY
    Hussein, Mwanza

    ReplyDelete
  67. Assalaam Allaikhum Binti Naona Mwenye uweza usiowezwa amekupa MTIHANI amekujalia kupata hicho KIJIKAZI cha kupata visenti sasa unaingia ktk anga zake na kutakabali.Nenda MUHIMBILI kaone wagonjwa wammkosea nini MOLA wa viumbe na wengine wamelazwa bila kutarajia na wana ELIMU na UZOEFU wa kazi kukushinda MOLA anaweza kukunyang'anya hivyo ulivyojaaliwa navyo ukamtafuta MSUKUMA mkokoteni ukamkosa.huku ulaya Wanawake wanakulipa ili uwaoe.KWANZA OMBA MSAMAHA KWA MOLA pili OMBA DUA iliupata MUME MZURI sio wa sura Atakaekufaa na kutokukudhumu haki yako kama MKE usijejuta na kulia MDOMO juu kama MMBWA.

    ReplyDelete
  68. MUNGU akupe hekima katika kuchambua majibu yote hapo juu yanaweza kukuchanganya zaidi. Usichukue hatua zaidi bali tulia utafakari zaidi, ukipata amani utachagua la kufanya, lakini ukichukulia uamuzi unaotokana na mashambulizi hapo juu hutapata
    jibu lililo sahihi. MUNGU aliyekupangia hutamkwepa

    ReplyDelete
  69. Kulthum
    Pata knowledge zaidi kuhusu uislam wako, na zijue haki zako kwenye 'islamic prenuptial agreement', haki za mke kwenye ndoa, na masharti unayoweza kuweka kabla ya ndoa.

    ReplyDelete
  70. JAMANI KWA NIN MNAZUNGUMZIA WANAWAKE TU KUWA TASA JE MWANAUME AKIWA TASA NA MWANAMKE ANAHITAJI MTOTO ITAKUAJE,HAPO ITABIDI KUFANYIKE MAREKEBISHO KIDOGO NA MWANAMKE NAE ARUHUSIWE KUOLEWA NA WANAUME ZAIDI YA MMOJA.

    ReplyDelete
  71. We Bidada kama umeolewa na mzungu mwaminifu basi umebahatisha lakini usigeneralise.

    Wanaume wote ni sawa kabisa ila wanatofautiana mbinu kulingana na maeneo wanayotokea.

    Kwa taarifa yako, wazungu wanapenda sana kuriot nje ya ndoa. Kwa standard ya maisha ya kwao ni vigumu kuwa na nyumba ndogo kama tunavyofanya huku kwetu. Badala yake yake wanatumia sana brothel, escort na call services. Hizo ni huduma za maexpert na huchukua muda mfupi tu kumaliza mambo yao na vigumu kwa mke kugundua. Ndio maana hizo huduma zimeshamiri sana huko kwao.

    Hawa jamaa issues zinapokuwa zimefunuka kunakuwa na mlolongo wa wanawake aliyowapitia.

    ReplyDelete
  72. assalam aleykum kulthum,hope u a duin great. kwanza mshukuru allah sw kwa kukupa kazi na pili hukyo mkristu wako ni mtihani allah anakupa hivyo muombe sana mola akuepusha na mtihani huo leo dunian hadi kesho akhera na ishu ya wake wengi kuna sababu tena za msingi hadi mwanaume kuoa na kam kweli wewe unamuamini allah ni muweza wa yote sidhani kam utaacha kuolewa mna mume wa kiislam kwa sababu ya mke mwingne inaonekana huna msimamo na dini yako so ukipata mtu wa kukushawishi vilivo hukawii kwenda kufunga ndoa ya mseto na kwa udhaifu wetu wanawake hukawii kubatizwa kabisa maana nimeisha ona wengi wa sampuli yako na hawana maisha mazuri kama unavyo fikiria wewe bali ni mateso kila siku, sali sana muombe mungu akupe mume mwenye heri kwako,pamoja na din yako na wazazi wako na nduguzo hilo ndo kubwa mengne matoke kuna watu wana kazi za maana kuliko hyo yako but hadi leo hawana waume kwani kitu hakiwi hadi ALLAH apange na ukiamini hilo utaishi maisha ya amani hapa dunian na dini ya kiislam iko kamili mumgu aliishayaona ambayo we hujayaona na ndo maana kila ktu kwenye KITABU KITUKUFU "HOLY QURAN" haikukiacha kazi kwako soma dini yako na uijue au uliza watu weney kuifahamu dini vyema wakuelimishe,au ukiona hilo ulilonalo kichwani kwako bora basi fanya ila majuto ni mjukuu na si mwana, Inshaallah Allah akuvushe katika mtihani huu na akufanyie wepesi katika hilo kama riziki yako ipo ipo siku utaipta mana riziki ya mtu haipotei hukawia tu ila kwa kuwa sisi ni viumbe dahifu na kutaka yale tuyatakoa na si ayatakoyo Allah basi hujikuta tunaishia kusema ningejua when it's too late. kwa msaada zaidi visit islamonline.net

    assalam aleykum
    mdada single kama wewe ma umri sawa nawe na kazi ya haja.

    ReplyDelete
  73. Rais Zuma kuoa mke wa tano
    Imeandikwa na KWAZULU-NATAL, Afrika Kusini; Tarehe: 29th December 2009 @ 08:06



    RAIS , Jacob Zuma, anatarajiwa kufunga ndoa Jumatatu ijayo.

    Thobeka Mabhija, atakuwa mke wa tano wa kiongozi huyo wa Afrika Kusini.

    Ingawa ufafanuzi juu ya ndoa hiyo unafichwa, gazeti la Sowetan, limebainisha kuwa Zuma atamwoa Mabhija. Zuma atafunga ndoa ikiwa imepita miaka miwili tangu aoe mke wa nne, Nompumelelo Ntuli-Zuma.

    Mabhija amekuwa akionekana katika matukio mbalimbali rasmi akiwa na wake wenza wenzake akiwamo Sizakele MaKhumalo-Zuma. Msholozi (Zuma) alilipa ilobolo (mahari) kwa familia ya Mabhija miaka miwili iliyopita. Mapema mwaka huu familia hiyo ilituma zawadi kwa familia yake, ikiwa ni ishara kuwa masuala yote kuhusu ndoa hiyo, ikiwa ni pamoja na siku, yameshapangwa.

    Mabhija alizaliwa Durban mwaka 1973. Alikulia Umlazi na kusoma katika shule ya juu ya biashara ya Umlazi. Alisoma pia katika kampasi ya Umlazi ya Chuo Kikuu cha Zululand ambako alipata Shahada ya Kwanza ya Biashara (BCom). Baada ya hapo alifanya kazi Standard Bank, Ithala na Cell C.

    Ndoa hiyo ilikuwa imepangwa kufungwa mapema mwaka huu, lakini ikaahirishwa kutokana na Zuma kuwa na kazi nyingi. Inaaminika kuwa baada ya kuapishwa kuwa Rais, kazi nyingi zilizomkabili zilimnyima fursa ya kushughulikia ndoa hiyo. Tangu Jumanne iliyopita, Zuma alikuwa nyumbani kwao Nkandla, ambako alishiriki mashindano ya kucheza chess jimboni KwaZulu-Natal.
    Pia alikula Krismasi na familia yake na ndugu na kujipumzisha kwa kutembeatembea na familia yake bila walinzi. Pia alishiriki kuwinda ndege na kunywa umqombothi (pombe ya asili).

    Juzi Zuma aliandaa hafla ya Krismasi na kundi la wazee wastaafu. Jana alitarajiwa kuandaa hafla nyingine kwa ajili ya watoto yatima. Vyanzo vya habari vimebainisha kwamba ndoa hiyo itafungwa, lakini itakuwa ya faragha. “Ndoa itafanyika Januari 4," kilisema chanzo cha habari. "Ni ndugu na marafiki wa karibu wa familia na wakazi wa eneo hili tu ndio watakaoruhusiwa kuhudhuria."

    Zuma alimwoa rasmi Kate Zuma, ambaye alifariki dunia mwaka 2000, pia Waziri wa zamani wa Mambo ya Ndani, Nkozasana Dlamini-Zuma. Waliachana mwaka 1998.

    Wake wa sasa wa Rais ni pamoja na Sizakele Khumalo na Nompumelelo Mantuli.

    Source: Habari Leo, 29.12.09

    ReplyDelete
  74. Achana na huyo Jamaa,njoo kwangu uone mambo mpaka ujutie kwanini unamkataa huyo mkristo! Yaan nitakutesa mpaka ufe kwa ugonjwa wa moyo

    ReplyDelete
  75. Dada wewe usitudanganye kuwa eti unafuata maadili, huo uongo na kama kweli maadili si ungeolewa na Muisilamu mwenzio eti unaogopa ataoa Mke mwingine.Hapo maadili huna na kama unayo olewa na huyu muisilamu vinginevyo tuambie kama una tatitizo lingine.

    ReplyDelete
  76. Dada yangu miningependakukushauri jambo moja,swali lako linahitaji ushari/ufafanuzi wahali yajuu sana wakiimani,nibora umtafute mtu ambaye amebobea katika masuala yakidini naimani atakushauri vizuri tu kwanikunamambo kadhaa unawezakufanya ilikumtambua mume,hayo yote yamefundishwa katika Dini yetu yakiislam,kumbuka dada yangu ''dhalikal-kitab lallaibafy''

    ReplyDelete
  77. Dada unaonekana uko ktk(midlife crisis)au kwa lugha yetu tungesema njia panda ya maisha.Ambapo unashindwa kufikia maamuzi based on what believe in or what you desire!.But you are trying to justify your desire through your jealousy and doubts.As a muslim we have been advised to refer to our holy Quran and the Sunah`s of Our beloved prophet Muhammad(PBUH)whenever we have our doubts.Kwani katika Juzuu ya kwanza sura Al-BAQARAH aya ya 2, Inasema,"Hiki ni kitabu kisichokuwa na shaka ndani yake,ni mwongozo kwa wamchao Mwenyezi Mungu" sasa wewe kama mwiislam na hujui ni kwa misingi gani mwanaume wa kiislam anapewa haki ya kuoa mke zaidi ya mmoja,basi fungua msahafu wako na ujielimishe na kama hivyo itakuwia vigumu basi wasiliana na wakufunzi wa dini ya kiislam ambao utaona wana upeo wa juu kielimu ili waweze kukuelimisha. Lakini ukituambia eti ukiolewa na mkristo una-guarantee ya kuwa mke wa pekee.Kwanza unajidanya wewe binafsi na pili unadhihirisha upeo wako finyu ktk kuona ukweli wa maisha.Sii ajabu wee mwenyewe unataka kufanywa kimada au mke wa pili na huyo huyo mkristo unayetaka akuowe.

    ReplyDelete
  78. Yes that's true dini ni utaratibu tu tulijiwekea na kufuatwa but mtu hatakwenda binguni kwa ajili ya dini bali ni kwa matendo mema yampendezayo mungu so binti sikiliza moyo wako na wala sio dini kwani huolewi na dini bali u're being married to a person(so it's the person whom you love and not Dini) Acha ushamba dada!Kwani hujawahi kushirikiana na mkristo katika maisha yako? Au Elimu uliyopata haijakusaidia kuchambua mambo.....!
    Mdau Ize.

    ReplyDelete
  79. Mimi nitaanza kwanza na kutoa jibu la jumla kwa masuali ya dizini hii ambayo yameshamiri katika blogu kama hii.
    Jamani kuna mambo ambayo tayari yameshaamulika na mamlaka husika; iwe serikali, dini, vyama, jumuiya n.k. sheria zake tayari zimetajwa kwenye asasi husika hivyo huhitaji kuja hapa kwenye blogu ati unataka ushauri. Sheria imeshatungwa; hapa unakuja kutaka ushauri wa nini? wa kuivunja? sidhani kama hapa ni pahali pake kupewa ushauri huo. Nitatoa mfano, Tume ya jiji; kama asasi husika ya planning ya mji wa dar imeamua kwamba eneo la mnazi mmoja kuweka bustani ya kumpumzikia, hivi inaingia akili kutujia hapa na kutuuliza nataka kujenga nyumba yangu ya kuishi eneo la bustani ya mnazi mmoja, vipi niendelee au niache?!!! Hivi kama hiki hakitokuwa kichaa ni kitu gani? unawajua lakini Tume ya jiji au unawasikia tu?
    Sasa hapa unakuja kuulizia suala ambalo tayari limeshakatiwa shauri ktk dini yako; unataka ushauriwe vipi? kuvunja sheria? hii inabaki shauri yako.
    Tafuta kwa yoyote na popote hamna ktk uislam mwanamke wa kiislam kuolewa na asiye muislam, bado unataka ushauri? na hili unalijua! Kuolewa ama kubaki single? nako unauliza na wakati unajiita Muislam, wapi umekuta ktk uislam ikizungumzwa watu kubaki-single?
    Tatizo ni elimu ndogo ya dini unayojinasibu nayo na kudai kuwa unaipenda, isome basi uifahamu na uwache kuja kuuliza masuala ya kitoto ktk blogu ya jamii.

    ReplyDelete
  80. Asalam alaykum, kwa kuwa wewe ni muislam huna budi kuolewa na muislam mwenzio na hiyo ni sheria ya mwenyezi Mungu, soma Quran 2:2 (hiki ni kitabu kisicho na shaka ndani yake na ni uwongofu kwa wachamungu).Soma dini yako na kuifuata sio kufuata maneno ya mitaani, utafata hasara duniani na kesho akhera.
    Nakuombea Mungu akuzindue utekeleze uislamu kwa vitendo.
    Wasalaam

    ReplyDelete
  81. assalam alayikum,I would like to clarify something kwa mtoa maoni aliejiita Hussein Mwanza,at 9.17am 29 dec 2009.just get me right am a girl I just want to meet Kulthum to help her as a muslim sister so dont be worried please,cause I have seen many of US we fall into this dilema and she sounds she needs more help rather than just putting views in here so I thought I will be going there I would like to meet her but if she wishes.shukran again sister plz write if okay we can share a lot you need to know your rights you dont have to be afraid,shukran.zkapemba@yahoo.com

    ReplyDelete
  82. Bi kuluthum kwanza Imani ya bwana iwe nawe au kwa lugha ya kiarabu Assalam Akaykum?Pili napenda kukuwekea wazi kwa mujibu wa vitabu vya dini mbili,MATHEW 19:1-11 inaeleza kuwa Mwanamme akimwacha mke akaoa mwengine basi anazini"na vile vile Yesu akasema si wote wanaoweza kukaa bila ndoa ila wale waliozaliwa hivyo au wakafanywa au wakajifanya,na wawili watakua kama mmoja aya inaendelea kusema:JIBU LA KWANZA:Lazima uolewe,AMA kuhusu kuoa wake wengi hata ukristo haujakataza au hakuna maandiko yaliyokataza soma JEREMIA 29:05 Mungu anasema oeni wake waozesheni watoto wenu wake na mabinti wapate kuzaa"1Kings 13:5 Suleiman akawa na wake 700"GENESIS 16;3"Sara akampa Hager mjakazi wake Abraham awe mkewe:pia Yesu alisema Mathew 05:17 sikuja kuitengua torati bali kutimiliza kwa hiyo anakubaliana na hayo ya manabii na UFUNUO 22:18 inasema usiongeze wala kupunguza kwa hiyo kuoa zaidi ya mke mmoja haijakatazwa au upunguze torati usiikubali agano la kale.PILI KWA UISLAMU wengi wamesema mkubaliane na mume lakini Sio sahihi Kabisa,katika Qur-an 33:36 inasema "Mungu na Mtume wakiamua jambo basi hakuna khiyari.."na Qur-an 4;59 inasema "Enyi mlioamini mtiini Mungu na Mtume na wenye mamlaka na ikiwa mkitofautiana jambo lirudisheni kwa Mungu..'Sasa wacha tulirudishe kuhusu la wake wanne:Qur-an 4:3 INASEMA"OENI mnaowapenda katika wanawake 2 au 3 au 4 lakini ikiwa mnahofu hamtofanya uadilifu basi muoe mmoja:Qur-an 4;129 insema "Na hamtoweza kufanya uadilifu baina ya wake zenu hata mfanye nini..Kwa hiyo hapa tayari ishaonesha kuwa mwanamme aoe MKE MMOJA TU kwa kuwa Mungu ashasema hatuwezi kufanya uadilifu.Kwa ufupi wewe unataka kuolewa na Mkristo Je mtafunga ndoa kwa sheria gani za nchi?15:15 MATHEW inasema :watu hawa huniabudu kwa midomo na kufundisha sheria za wanadamu nao waniabudu bure:Qur-an 5-47 inasema Tusihukumu kwa kutofata njia za Mungu,kwa ufupi hapo utakua umekwenda kinyume na hautokua na ndoa,kwani mwanamke muislam haolewi na mwanamme wa dini nyengine ila Wanaume waislam wanaruhusiwa kuoa wake waliopewa kitabu kwa kuwa wanaume ni strong kwa asilimia kubwa kuliko wanawake.BASI kama mmependana shaurianeni aingie katika dini ya kiislam na akikataa basi jizuilie kwa kufunga hadi Mungu atakapokupa yule anaekufaa Qur-an 24;33 inasema "Na wasiona uwezo wajizuilie hadi mungu atakapowawezesha kuoa..: kwani katika Dini ya kiislam UTAWA HAUKUBALIKI qur-an 57:27"NA Utawa ambao wamejifanyia wenyewe na wasiutimize hakizake..NA NDIO MAANA UNAKUTA WANASHINDWA WATU KUKAA NA KUJIFANYIA ZINAA "JEREMIA 29;05"OENI NA MUOZE NA MZAE-Kwa ufupi huo ni ushauri wangu na kuhusu mali na kazi uliyonayo,hayo ni matatizo mengi ya wanawake hasa wa kwetu Tanzania elimu yake mtu inamuhangaisha kwa mfano ukiangalia mawaziri wengi wa kike utakuta hawajaolewa,na hiyo inapingana na dini zote kama yesu alivosema,hapo juu na vile vile qur-an.Na hili linatokana kuwa wakati wa kuipata hiyo elimu kama amekua nje ya nchi BASI amekua akifanya zinaa sana kwani Dada zetu wengu wanaokuja Ulaya hata wakiwa na waume huku huendeleza zinaa tu,Tena nchi mbali mbali Na mi nitakuuliza swali moja JE BABA YAKO ANA WAKE WANGAPI?najua kwa umri wake itakua baina ya 53-57 kwa maelezo zaidi wasiliana nami katika www.tanzaniansingreece.com AHSANTE:NURAMO GREECE.

    ReplyDelete
  83. ok so mkristo hatoowa mke mwenngine lakini hapana guarantee kuwa hatokuwa na nyumba ndogo. sasa suali ni kwako unataka kusuka au kunyoa. mume wa kiislamu ambae huenda akaowa mke mwengine na ukajuwa kuwa una mke mwenza, au mume asokuwa muislamu wa kweli na huenda akawa na nyumba ndogo usiyoijuwa.

    ReplyDelete
  84. MIAKA 27 BADO MDOGO SANA SUBIRI SUBIRI KIDOGO INAONEKENA BADO HUJAPENDA. KWANI MOYO WA PENDO HAUNA SUBIRA. UTAKAPOPENDA HUTATUULIZA UMENIPATA

    ReplyDelete
  85. KWANZA KABISA KAMA ULIVYOSEMA MKIRISTO UTAKI KUOLEWA NAE...KWA KIFUPI SASA HIVI DUNIA IMEBADILIKA DADA INAONEKANA UMESOMA SEMA BADO UKO MBALI SANA NA DUNIA...NYAKATO NI MBALI SANA.SASA NAKUPA SABABU ZA MAISHA YA LEO...UKIWA UMESOMA NA UNAJUA MAISHA DINI SIO ISSUE KABISA KUHUSU MUME GANI WA KUOHANA NAE.KINACHOMA NANI UNAMWAMINI NA UNAMPENDA....KAMA WEWE UWEZI KUBADILI BASI MUHULIZE YEYE ABADILI DINI...KAMA WOTE HAIWEZEKANI NENDENI CITY HALL MKALE KIAPO...KUMBUA NDOA NI KARATASI TU SIO BIG DEAL SANA.KUHUSU WAISLAM KUOA WAKE WENGI..ASILIMIA KUBWA YA WANAWAKE WANAOKUBALI UKEWENZA NI MASIKI NA ELIMU DUNI...LAKINI SIO WENYE UWEZO WAO NA ELIMU NZURI WATAKUBALI UPUUZI HUO.NAZANI UMESOMA HIVYO SIONI KAMA UTAKUWA MJINGA KIASI HICHO.
    MDAU UK.

    ReplyDelete
  86. Dada Kuruthum,

    Je uliingiaje kwenye Uislamu ? Nadhani ulizaliwa ukajikuta Muislamu kwa kuwa wazazi wako pia walikuwa waislamu.
    Je bado unadhani wewe ni mtoto mdogo wa kushika dini ambayo hujui chanzo chake na ambayo huwezi kufuata masharti yake???
    Kama dini ya Kiislamu inaruhusu wake wengi sasa unachopinga nini ? Hukubaliani na UISLAMU ? Sasa kwa nini unakataa Mkristo ambaye dini yake hairuhusu mke zaidi ya mmoja ?
    Naona hujatulia hata kidogo. Msaada wangu kwako kwa kuwa unataka watoto zaa tu na mtu yeyote na usifunge ndoa.Period

    ReplyDelete
  87. Jamani, isije kuwa siku hizi watu wanatumia blog hii kufanya utafiti!!. Ku'thumu, masumbufu juu ya nini dada yangu. Wengi wamekujibu kwa hekima kubwa. Nimevutiwa na aliyesema ndoa ni ibada. Hapa ndipo asili ya uamuzi wako itakapojikita (kama wewe ni mcha Mungu). Ukifahamu hilo basi suluhisho umelipata. Lakini inavyoonekana wewe bado hujaijua imani yako vizuri na ukiendelea hivyo nina wasiwasi ukakwazika zaidi manake muislamu na mkristo wamekwisha kukuchanganya, je, akiongezeka mtao, mbudha na huyo dkt. wa kinigeria (kisa anakufurahisha kwa kuzungumza kama ingwe) si ndo utashaa. Fuata mafundisho ya dini yako suluhisho utalipata. We kalaghabao, itakula kwako oohoo!!!!!!!

    ReplyDelete
  88. dada Kuruthum,unasahau kitu kimoja kuwa wanaume washenzi wapo kote kwenye dini zote mbili mwanaume wa kiislam anaweza asioe mke wa pili bado akawa na vimadaa wa nje kibao kwahiyo swala la kusema kwamba wanaume wakristo ndo wana tabia hiyo peke yao si kweli ushenzi upo kote,ushauri wangu ni kwamba ukitaka ndoa ya amani na nzuri angalia mwanaume ambaye mnapendana naye kama atakuwa mkristo jaribu kumshauri awe mwislamu ili uweze kuolewa naye na kama atakataa si tatizo mnaweza kuoana kikatiba cha msingi umpate ambaye interest zenu zinafanana halafu muwe mnapendana nadhani hapo utaishi maisha ya ila kinyume na hapo bora ubakie single

    ReplyDelete
  89. Mtaka yote hukosa yote shosti, mbona huna msimamo wewe huwezi kusema mwislamu unaogopa kuolewa nae, hapo hapo mkristu hutaki eti una imani ya kiislam, wewe huyo huyo unapenda maisha ya ndoa na unahitaji watoto!!!! kaa chini uamue mwenyewe na uamuzi wako lazima ukubali kuacha kimoja ndio upate kingine.

    ReplyDelete
  90. Wengi hawajamuelewa Kuluthumu, hajasema kwamba kuna mvulana wa Kiislamu amemfuata, yeye amesema kwamba kuna mvulana wa Kikristu amemfuata. Kwa hiyo kumuelekeza kwamba aolewe na muislamu ni kujaribu kumchagulia mwenzi wake wa maisha, jambo ambalo atalijutia sana. acheni aolewe na huyu aliyempenda mwenyewe. Mimi mwenyewe ni mkristu na nina msichana muislamu ambaye kwangu amefika, hasikii wala haambiwi lolote na mtu juu ya dini yangu !! Ninamshauri Kuruthumu aendelee na huyo na kama mvulana ni RC basi wafunge ndoa ya mseto na kila mtu ataendelea kuabudu anakotaka. Atayafurahia maisha yake na hata wakikwaruzana, hatajuta kwani alimchagua mwenyewe, hakuchaguliwa na mtu !!

    ReplyDelete
  91. Ukiona umeshindwa kugundua kwamba kuolewa na mume asokuwa muislamu ni kharam; basi huna maadili ya kiislamu hata kidogo!..
    1- anaweza akakuhitaji ktk tendo wakati wewe una udhu unataka usali!..

    2- kuhusu sitara za kiislamu kwa mfano,sahau kutoka naye umevaa full hijab,hilo hatoruhusu hata awe na moyo gani!.

    3- pia ndoa hufungwa kwa kuzingatia maamrisho ya Allah, je hiyo yenu atairidhia nani ikiwa mashart yote ya ndoa utakiuka?.

    Kuhusu kuoa mke zaidi ya mmoja:
    Wanawake duniani kote ni wengi kuliko wanaume i.e ktk watu bilioni 8 unakuta wanawake mko bilioni 5!.. sasa wanaume wanakuwa wapo bilioni 3..kila mume akioa mmoja tu kuna wake bilioni 2 wanakuwa hawana waume, unaonaje na wewe ukiwa katika hao bilioni 2???. Pia kumbuka wanaume wote wana nguvu za kuhudumia wanawake zaidi ya mmoja kibaiolojia, pia wana saikolojia ya kuvutiwa na mke zaidi ya mmoja!.

    By the way, ktk hii blog sio mahala pale kuuliza suala la kiimani!.. utapotezwa hapa kuna miluzi mingi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...