Kaka Michu,
Naomba unifikishie ujumbe huu kwa
waheshimiwa wa NMB tawi la Morogoro road.

Mimi ni mteja katika tawi hilo.
Kwa kuwa siku hizi huduma ya ATM imepamba moto siku nyingi nilikuwa sijaingia ndani ya tawi hilo. Juzijuzi kadi ikaanza kusumbua hivyo leo 26/05/2010 nikaamua kwenda kuripoti tatizo.
Nilivyoingia ndani nikashangaa sana. Ground floor yote ni counters tu, hakuna ofisi wala ofisa wa kusaidia wateja. Mimi kwa bahati mbaya/nzuri ni mlemavu natembea kwa msaada wa cluches. Customer care yao wameihamishia mezzannine (kama siyo first) floor.
Any way nilijitahidi kupanda kitu kingine kibaya nilichokutana nacho ni kwamba ngazi haziko friendly designed ziko so steep. Kulikuwa na uwezekano mkubwa sana wa kuteleza na hata kuvunjika mikono.

Ushauri wangu ni kwamba kuwe na ofisi japo moja ground floor kwa ajili ya watu kama mimi. Wapo watu wanaotembea kwa wheel chair na wazee ambao hizo ngazi hawawezi kupanda, je? wao sio wateja?
Nawasisilisha,
Mdau Mkereketwa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 20 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 26, 2010

    Noted for compliance!

    SHYROSE BHANJI

    ReplyDelete
  2. VERY GOOD POINT.....next time usiweke account number yako, huwezi jua maana bongo kwa visasi unaweza kuta account yako imepotea!!

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 26, 2010

    Why would I care to consume Tanzanian Products while the very producers don't care about the consumers? Why would i care to be a Tanzanian while the government and fellow citizens don't even care about their own people and colleagues? Upumbafu wetu umetufikisha hapa!! Mungu Ibariki nchi yetu ya daraja la tatu na produce zetu zilizopo daraja hilo hilo.

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 26, 2010

    Da, pole sana ndugu yangu kwa yaliyokukuta, huo utaratibu wao haufai kabisa ni bora waweke ofisi hata moja kwaajili ya wateja floor ya chini kuna wagonjwa kama ulivyosema au watu wa namna yako, wao hawana nafasi ya kupata huduma katika benki hiyo? wafunge akaunti zao?

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 26, 2010

    Na huu uwe ujumbe kwa maofisi mengine yote nchini.

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 26, 2010

    LABDA NAANZA KUWA KIPOFU, KWANI MIMI SIJAONA MAHALA HUYU MDAU AMEWEKA AKAUNTI NAMBA YAKE, KAMA MDAU ANVYOMSHAURI HAPO JUU. HII NI SWALA LA WIZARA YA USTAWI WA JAMII INATAKIWA KUPITISHA SHERIA ITAKAYOWAAMURU WATU WOTE WANAOFANYA SHUGHULI NA JAMII KUZINGATIA MATWAKWA YA WENZETU HAWA, NA IWE NA MENO WASIPOFANYA HIVYO BASI KUWE NA ADHABU, HII IWE HATA KWENYE USAFIRI NA MAHALA POPOTE PALE PANAPOTOWA HUDUMA KWA JAMII

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 26, 2010

    Akauti namba ilikuwepo, ni vizuri Michuzi ameiondoa mapema.

    Wazo zuri sana...laiti kama wale wote wenye kero wangekuwa wanalalamika kwa ushahidi namna hii.

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 26, 2010

    Mdau ametoa maoni haya kuhusu NMB lakini nchi ina tatizo kubwa sana la kutofikiria walemavu katika usanifu wa mambo mengi, sio maofisi tu. Hata njia zetu za waenda kwa miguu hazirahisishi maisha kwa anayetumia baiskeli ya walemavu. Hakuna maegesho maalum kwa walemavu ili kuwapunguzia umbali wa kufika maofisini nk.

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 26, 2010

    Ujumbe Huu ni kwa ofisi zote zisizojali baadhi ya watu

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 26, 2010

    Ujumbe Huu ni kwa ofisi zote zisizojali baadhi ya watu

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 26, 2010

    Hawa NMB nadhani imefika wakati waamue moja tu kupunguza wateja na aina za wateja kulikono kuendelea kufanya kampeni ya kuongeza wateja wakati huduma zao haziendi sambamba na ongezeko la wateja. Pia nawashauri wawapeleke training mara kwa mara watu wa Huduma kwa wateja kwani ukweli ni kwamba wengi wanaokaa pale ni wale wenye stashahada au shahada za Banking, Accounting,commerce au business adminitration tu lakini sio qualified customer care persons ndio maana pale unaweza kwenda kwenye desk lao kisha ukajutia ni kwanini ulikua mteja wa benki yao.Kuna rafiki yangu mmoja alitaka kufungua akaunti pale Mlimani city akapewa form ya kufungua akaunti akajaza vizuri, kapeleka picha na barua ya serikali za mitaa alipofika pale akakataliwa kufungua account ati barua ya serikali za mitaa imeomba apewe ushirikiano NMB lakini haikusema NMB tawi gani,yaani haiku address NMB MLIMANI CITY hii kutotaja MLIMANI CITY kwenye barua yake ya serikali za mitaa ikamkosesha kufungua account siku hiyo hadi jamaa atakapoleta barua nyingine inayoaddress NMB MLIMANI CITY! kwa hasira jamaa akaona isiwe tabu akatoka akaenda zake benki ya ushirika na maendeleo vijijini! Sasa ukiangalia hapo utaona kuna ka percentage flani ka profit NMB wamepoteza kwa kumkosa huyu mteja kutokana na Customer care desk(CCD) kufanya kazi kwa mazoea. Tubadilike jamani CCD sio NMB tu benki zote. Punguzeni huo msemo wenu wa "hivi ndivyo ilivyo" badala yake "use the principles and sometimes common sense" sio routine tuuu kila siku.

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 26, 2010

    Shyrose!
    For that comment you deserve to there, thank you. Very few manager admit mistake and respond to change.

    I call other to learn from that girl. Big up. Sio mtu anaambiwa anavimba mdomo na kuanza jeuri.

    Jamani wa kiswaili, Dada huyu anastaili kuwepo hapo alipo kwani anajua anachaofanya.

    Asanten. Michuzi nawe ubarikiwe kwa kablog kako haka. Mimi mdau wako sana hapa sweden japo unabana tucomment twangu.

    ReplyDelete
  13. Michelle Obama!May 26, 2010

    Naungana na mdau hapo juu kumpa big up da Shyrose! Manake kwa tabia zetu bongo navojua angelalamika hapo ofisin kwa hao kina dada customer service angebinjuliwa midomo mpaka ashangae mwenyewe! makarani wa benki bongo punguzeni nyodo! hiyo ni biashara kama biashara ingine yoyote na bila kuwa na wateja hata nyie kazi hamna! Da Shyrose hivi huwa mnawapa kozi mara kwa mara hao customer service wenu? they really need to be reminded frequently to do their job!
    thanx.

    ReplyDelete
  14. AnonymousMay 27, 2010

    SHY ROSE BANJI: sijui kama huyajui matatizo ya NMB au nawe ushkuwa mtu wa siasa sasa. Hili linalosemwa la ofisi ya huduma kwa wateja kutokuwepo chini ni moja tu, la pili ni kukosekana kwa sehemu za haja (vyoo) sijui kama ni sera za mabenki. Hata kama vitakuwepo nashani hata kwenye ofisi nyingi ni vya kibaguzi (havijui kuna walemavu.

    Inafafana na ile milango inayozunguka kama pale International House ambapo hakuna kwa kupita mlemavu....

    NMB kwa ujumla huduma kwa wateja ni zero kabisa kwa sasa ni afadhali hata Benki ya Waalimu ya "Sidanganyiki" (TPB) wameboresha huduma zao.

    ReplyDelete
  15. AnonymousMay 27, 2010

    We unayesema bank ipunguze watena are you serious...Nani anajukumu hilo? Ni wewe mwenyewe..usijali matangazo bali jali huduma hupendi huduma za mahali fulani funga account yako hapo fungua kwenye bank nyingine yenye huduma nzuri.

    Bongo hawajui kuwa mteja ni mfalme. Wanatreat wateja kama vile sijui nini wakati kama sio wewe mteja hiyo huduma yao isingeweza kuendelea.

    Inabidi watu wajifunze..Huku tuliko wenye kutoa huduma wanatulamba miguu na ukilalalmika tu ukaacha contact information zako watakupigia simu na kukubeembeleza na hata kama ulinunua kitu utarudishiwa hela yako na kam ani huduma za bank wamekucharge hovyo watakuomba msamaha na kama kunakitu walikosea watakurudishia zote na fees zilizoingia kutokana na hiyo transaction. Yote hiyi ni kunifanya niendelee kuwatumia hao.

    Tanzania wanazania wakiwa na mteja mammilionear wawili basi wasio na hela nyingi hawawataki kumbe hawajui kidogo kidogo hujaza kibaba. Kila mteja ni faida

    Tujifunze kutumia power zetu mtu anakutreat vibaya hama

    ReplyDelete
  16. AnonymousMay 27, 2010

    Am very shocked!! Inakuwaje kampuni inafungua benki na kupitishwa kuhudumia wananchi bila kuwa na sehemu ya WALEMAVU??? AMERICANS CALL IT "ADA" AMERICA DISABILITY ACT- THIS MEANS ALL THE FINANCIAL INSTITUTIONS MUST HAVE A SPECIAL COUNTER FOR DISABLED PEOPLE!! THIS WOULD HAVE BEEN A JUICY LAWSUIT IN AMERICA!!! Ndo maana wenzetu wa nchi za majuu wako juu siku zote na wanamaendeleo. TZ twatia huruma sana-wananchi wananyanyasika hadi sehemu wanazo weka hela zao jamani??? kweli TZ imefikia pabaya sana!! am so sorry to hear that! Duu!

    ReplyDelete
  17. AnonymousMay 27, 2010

    mimi niliwahi kuchana barua ya mtendaji mbele ya mhudumu wa benki ya muleba nmb kutokana na maswali ya kijinga nilichomwambia kuwa hela si zangu naondoka nazo

    ReplyDelete
  18. AnonymousMay 27, 2010

    Mimi natoa lawama kwa vyama na vikundi vya walemavu. Moja ya kazi zao ni lobbying ili vitu vifanyike kwa kuwajali wao pia. Ni wao wakuwabana wadau watekeleze majukumu yao. Waajiri wengi utakuta kwenye nafasi za kazi wanasema wanatoa nafasi za upendeleo kwa wanawake wakati wanatakiwa watoe nafasi za upendeleo kwa vilema pia. Muanzishe aina ya certification kwa mashirika na asasi zinazowajali walemavu, mnawapelekea vigezo vyenu na atakaevifanikisha mnampa haki ya kutumia nembo yenu kwenye matangazo na bidhaa zake kama wanavyofanya UK.

    ReplyDelete
  19. AnonymousMay 27, 2010

    MICHUZI NA MDAU ALIYETUMA MADA NAWASHUKURU SANA,YANI ME MWENYEWE KWELI NMB MOROGORO RD, WAMENIBOA SANA KUNA SIKU NIMEENDA KUDEPOSIT CHEQUE YA BOSS WANGU,KWANZA NIMEPELEKA NIKAAMBIWA MPAKA UPELEKE UKAGONGE MUHURI HUKO JUU WANAPOSEMA FLOOR YA 1,NIMERUDI KUJA KUPANGA FOLENI TENA NAAMBIWA MUDA WA KUPOKEA CHEQUE UMEISHA MPAKA KESHO JAMANI KWELI HII NI HUDUMA?ALAFU HAO WADADA SASA WANAVYOKUANGALIA KWA DHARAU,YANI WANAONA MTU UKIENDA PALE HUNA UNALOLIJUA WAO NDIO WAO,MSIWE HIVYO SISI NDIO TUNAOWAWEKA HAPO JAMANI,YANI HAWATAKI KUKUBALI KAZI ZAO,KWASABABU MTU KAMA UMEIKUBALI KAZI YAKO ALWAYS YOU HAVE TO SMILE NA UWAHUDUMIE WATEJA WOTE SAWA HATA KAMA UNAMATATIZI YA NYUMBANI KWAKO,PALE WEKA KANDO,YANI MTU ANGEPATA KUJA KUNIONA OFICE KWANGU ME NI RECEPTIONIST KWELI UNGEFURAHI SANA,DADA SHYROSE WW UMKARIMU SANA TUONMBA UWE UNAWAPA DARASA HAO WANAWAKE WENZIO SIO WAWEWANANUNA TU KILA MTU WANAMDHARAU,NA HII SIO KWA NMB PEKEE,NBC NA BENKI ZINGINE ZOTE

    ReplyDelete
  20. AnonymousMay 27, 2010

    Nashauri NGOs pamoja na serikali zifanye jitihada kuwafunza architects/ building designers kuhusu michoro inayokubalika kwa walemavu wote. Nashangaa Manisipaa na serikali zinapitihs michoro hiyo bado. Nilifurahishwa sana na majengo na miundo mbinu ya Mzumbe University jinsi inavuojali walemavu. Au ni kwa kuwa misaada ilitoka Norway/NORAD?. Watanzania tubadilike, miaka 50+ ya uhuru sasa.
    Richard Mazingira

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...