Gwaride la Askari wa  JWTZ Base ya Anga ya Ngerengere, wakifanya onesho la namna  mazishi ya Askari mwenzao aliyefariki  dunia yanavyokuwa upaande wa Kijeshi na kiraia , wakati wa  maadhimisho ya siku ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania ( JWTZ) ya kutimiza miaka 47 tangu kuanzishwa kwake Septemba mosi, 1964.
 Gwaride la Askari wa  JWTZ Base ya Anga ya Ngerengere, la mazishi wakipinga risasi baridi hewani , kuonesha mfano wa  namna  ya mazishi ya Askari mwenzao aliyefariki  dunia  yanavyokuwa upaande wa Kijeshi na kiraia , wakati wa  maadhimisho ya siku ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania ( JWTZ) ya kutimiza miaka 47 tangu kuanzishwa kwake Septemba mosi, 1964.
 Mkuu wa Komandi ya Vikosi vya Anga Base ya Ngerengere,Brigedia Jenerali Joseph Kapwani ( kushoto) akigonganisha glasi na Mkuu wa Wataalamu wa Kijeshi kutoka Jeshi la  Anga la Watu wa Jamhuri ya China, hapa nchini, Kanali Mwandamizi , Zhu You Yu ( kati kati) na (kulia ) ni Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Said Mwambungu, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania ( JWTZ) ya kutimiza miaka 47 tangu kuanzishwa kwake Septemba mosi, 1964.
 Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Said Mwambungu( wapili kutoka kushoto) akiwa na mweyeji wake Mkuu wa Kamandi ya Base ya Anga Ngerengere, Brigedia Jenerali, Joseph Kapwani ( watatu kutoka kushoto) pamoja na maafisa waandamizi wengine wa base hiyo
Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Said Mwambungu ( wenye suti) akisalimiana na Askari wanafunzi wa chuo cha Kijeshi cha Anga, Base ya Ngerengere.
Picha na John Nditi wa Globu ya Jamii, Morogoro

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Daa WAKUU wetu wa Wilaya na Mikoa mmmmhhhhhhh karne ya kale!!!!! Kama CCM na Kikwete wangependa Mapinduzi ya HARAKA waingize vijana wenye Exposure ya kutosha kushauri mikakati ya mapinduzi ktk nyanja za usalama na maendeleo kwa ujumla.

    Karim

    ReplyDelete
  2. Wajeda acheni ushamba jama, mwaka 2011 huu... Si uchuro huo, eti akifa anazikwa/anaagwa hivi! Pigeni sarakasi na hizo Chengdu zenu na MiGs walau mshtue kidogo. Hamjui parade za uhuru ni za kupiga bakora? Unadhani wenzetu wanavyopitisha miBulava na miICBM yao ni wajinga?

    Mambo ya kizamaaani ndo maana mnafanyia humohumo ndani kwenu, aagh! Make it a public parade/celebration. Earn some respect, threat some enemies... ndo maana ya hizo shughuli, eti jinsi ya kumzika mwenzetu, du hii kali!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...