Ujumbe wa Tanzania katika mkutano wa 125 wa IPU chini ya uongozi wa Spika Makinda (katikati) ukijadili jambo kabla ya uchaguzi mkuu wa Rais wa IPU. Kulia kwake ni Mhe. Angela Kairuki na Kushoto ni Mhe Suzan Lyimo. Mhe. Kairuki amechaguliwa kuziwakilisha nchi za Afrika katika Kamati ya Bunge la Dunia inayoshughulikia Haki za Binadamu na Wabunge. Mhe. Hamadi Rashid ni Makamu wa Rais wa Kamati ya Bunge la Dunia inayoshughulikia Maendeleo endelevu, Fedha na Biashara.
Mhe. David Kafulila akitimiza haki yake ya kidemokrasia kwa kupiga kura ya kumchagua Rais wa IPU.
Spika wa Bunge la Uganda Mhe. Rebecca Kadaga (kushoto) akimpongeza Spika wa Morocco Bwa. Radi A. kwa kuchaguliwa kwake kuwa Rais wa IPU.Picha na Prosper Minja.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...