Familia ya Marehemu Mzee Robert Jaka wa Forest Hill - Morogoro, inapenda kutoa shukrani za dhati kwa ndugu, jamaa na marafiki wote walioshiriki kwa namna moja au nyingine katika kumuuguza na hatimaye katika kuifariji familia wakati wa msiba wa mpendwa wao Mzee Robert Jaka, aliyefariki tarehe Jumapili ya tarehe 22.01.2012 na kuzikwa Jumatano ya tarehe 25.01.2012 katika makaburi ya Kola-Morogoro.

Kwa kuwa si rahisi kuwataja wote, familia inapenda kuchukua nafasi hii kutoa shukrani kwa Madaktari na wauguzi wote wa hospitali za Mkoa Morogoro na Regency ya jijini Dar-es-salaam: Pia tunawashukuru Magereza Makao Makuu; Chuo Kikuu cha Dar-es-saalam kwa msaada wao wa hali na mali.

Shukrani za pekee pia ziuendee uongozi wa kanisa katoliki parokia ya Mtoni Kijichi-Dar-es-salaam na Mtakatifu Patrick Morogoro kwa msaada wa kiroho.

Tunaomba wote mzipokee shukrani zetu hizi za dhati na kwamba Bwana awabariki kwa moyo mliounyesha kwa familia.

Mkesha wa msalaba utakuwa tarehe 13.04.2012 kuamkia tarehe 14.04.2012 (Jumamosi) ambayo itakuwa ni siku ya msalaba wenyewe.

Bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe [Ayub. 1:21]

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Mimi nilitoa maoni ya kuilaumu serikali najua Michuzi hawezi kuyatoa na hata haya maneno hatoi. Najua yupo upande wa SIRIKALI.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...