Mkaazi wa kijiji cha Magomeni Wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani,  Khamisi Tanga (46), ameota  matiti katika hali isiyo ya kawaida ikidaiwa imesababishwa na kutumia dawa za kupunguza  makali ya Ukimwi   ARV’S.
     Akizungumza na waandishi wa habari waliokwenda Wilayani humo kufanya utafiti kuhusu utekelezaji wa sheria ya Ukimwi na Chama cha Waandishi wa habari za Ukimwi (AJAT),Khamisi (Pichani) alisema alipatwa na mkasa huo miaka mitatu iliyopita.
    Akisimulia namna alivyoanza kuugua alisema awali aliona matiti yake yakiongezeka ukubwa kila kukicha lakini hakujua kama lingeweza kuja kuwa tatizo kubwa kama lilivyo sasa.
    Baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya ilimbidi kwenda kliniki anayohudhuriaga kupata dawa na kuwaeleza manesi ambapo walimjibu kuwa imesababishwa na dawa anazotumia na hivyo kulazimika kukatizwa dozi hiyo na kupewa aina nyingine.
    Hata hivyo Khamisi alisema kwamba pamoja na kubadilishiwa dozi hajaona kama kuna mabadiliko yoyote aliyoyapata na kuongeza kwamba hivi karibuni alipewa dawa nyingine ambazo kati ya hizo kuna zile ambazo zilimsabishia matiti na tayari ameanza kupatwa na maumivu aliyokuwa akisikiaga awali wakati matiti yalivyokuwa yanaanza kuota.
     Kwa mujibu wa Khamisi ameshahangaika kupata matibabu hadi Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili lakini hadi leo hajapatiwa tiba stahili ya kumaliza tatizo hilo.
    “Jamani Watanzania naomba wanisaidie kwa njia yoyote ile ili niondekane na hali hii kwani inanidhoofisha sana na kunikosesha raha hasa mbele ya wanaume wenzangu.
"Kwani hapa navyoongea na nyie waandishi nilipimwa hadi kansa na matiti ndio kama hivyo mnavyoyaona yanaendelea kukua na huniuma sana hasa wakati ninapolala,”alisema kaka huyo.
Pia alitumia fursa hiyo kumuomba Rais Jakaya Kikwete kumsaidia ili arudi katika hali yake ya uanaume kwa kuwa maisha kwa sasa kwake yamezidi kuwa magumu kwa kuwa hawezi kufanya kazi yoyote kutokana na hali hiyo.
Mtaalam wa magonjwa, Dk. Dina Komakoma,akielezea kuhusu sababu za kutokewa kwa hali hiyo kwa wagonjwa wenye maambukizi ya VVU ni jambo la kawaida japo hutofautiana.
Dk. Komakoma alisema wengine hujikuta wakinenepa au wakikonda sana na hili la Khamis sio mtu wa kwanza kupatwa na hali hiyo na kuongeza kwamba inapotokea mgonjwa akapata hali tofauti kama hiyo anapaswa kusitishiwa dawa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 18, 2012

    Pole sana kaka Khamis, inasikitisha sana.

    Ugonjwa huu tutapona kweli? Manake usipoleta wewe utaletewa na mwenzio mwenye tamaa zake.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 18, 2012

    huyu mtu apelekwe India , huko hakuna kinachoshindikana -wahindi kwa matibabu ni wachawi !!!! sasa , duh !! jamani nauliza -kweli hizi dawa zinaotesha maziwa ??? je ikiwa mwanamke mwenye virusi akizitumia , naye ataota maziwa -labda sehemu nyingine ?? maana tayari maziwa anayo, au hapa daktari Komakoma ,imekaa kaa je ?? Kingine , jamani wanaume tuwaheshimu wanawake zetu-siyo kushika shika maziwa kwa nguvu-kumbe yanauma, na pia ,kumbe si rahisi kuwa mwanamke, lakini tunavyowanyanyasa !!!! .Jamani TUKOME. Zebedayo-kweli inauma.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 18, 2012

    "anayohudhuriaga". mhhhhhhhhhh!!!!

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 18, 2012

    Nashauri TFDA waangalia element zinazotengeneza ARV na wafananishe za homoni za kike zinazojihusisha na matiti.Hii itasaidia kufahamu ukweli wa hizi dawa kwa kuwa watengenezaji si Mungu ambaye amekamilika katika uumbaji wake.Na kama TFDa hawatakuwa na uwezo wa kutambua hilo jambo mapema wawapatie kazi hii taasisi zetu za elimu ya juu,wanafunzi wanaofanya kozi za uzamili au uzamivu inaweza kuwa ni tasinifu ya kwao.Taasisi za kuzitumia ni kama MUHAS, NM-AIST, n.k. Pole kaka na hilo na endelea kuwa mvumilivu kwani Muumba analipa kwa kila anayevulimilia apatapo na msiba/shida

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 18, 2012

    ewe mungu muweza muumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake....tunakuomba sisi waja wako tujaalie mema ya huko peponi na tufanyie wepesi katika kumalizia hii dunia

    kwani dalili zote za mwisho wa dunia zilizoandikwa kwenye kitabu cha dini zinaonekana na zimekamilika

    kilichobaki tu ni kurudi kwa nabii issa au yetu ili kila mmoja abebe mzigo wake.

    mungu atakupa salama ameen.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 18, 2012

    Michuzi mbona kichwa cha habari sio sahihi? itakuwaje anadai ilhali ushahidi huo hapo kafunua na pia wataalamu wamethibitisha kuwa amefikwa na hayo kwa kutumia dawa alizokuwa akitumia? Hapo utasemaje kuwa anadai?

    ReplyDelete
  7. Hii inawezekana kuwa jamma alipewa dawa za"hormons"za kukuuza matiti kwa wale wanaume wanaofanyishiwa operation ya kubadilika kutoka mwaume kuwa mwanamke! Ingekuwa Ulaya angedai fidia.
    David O. Gang'ai

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 18, 2012

    Pole ndugu yetu!

    Mola atakusitiri na mtihani huu!

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 18, 2012

    jamani hichi ni kitu cha kawaida huku ulaya haswa watu kibao wanashikwa na matatizo haya hii inaitwa GYNECOMASTIA

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 18, 2012

    ''jamani hichi ni kitu cha kawaida huku ulaya haswa watu kibao wanashikwa na matatizo haya hii inaitwa GYNECOMASTIA

    Mon Jun 18, 06:01:00 PM 2012''

    Asante kwa darasa fupi!!
    Inakuwa ngumu kidogo kuingia akilini!

    Eh! huku virusi huku 'kifua' jamani!

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 18, 2012

    Pole sana kaka kwa hayo. Ila GYNECOMASTIA husababishwa na hormone za kike ambazo ARVs esp HAART zinazi-induce angalia links hizi zinaweza kukusaidia jinsi ya kufanya kupunguza hormone hizi za kike mwilini lakini pia tafuta dawa ingine.

    1: http://www.livestrong.com/article/187828-how-to-reduce-male-breasts-without-surgery/

    2: http://www.mayoclinic.com/health/gynecomastia/ds00850/dsection=causes

    3: http://www.thebody.com/cgi-bin/bbs/showflat.php?C=&Board=gaymen&Number=42305

    Pia google na utapata lots information kuhusu haya matatizo na jinsi ya kuyatatua.

    Akhsante:

    Mama H

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...