Awamu ya kwanza ya zoezi la kwasaka vijana watakaoweza kumudu mchakamchaka wa shindano la Maisha Plus, imeanza jana (Agosti 27) huko Bagamoyo mkoani Pwani.
Leo shindano hilo litafanya usaili katika wilaya ya Lushoto ambako zoezi hili litafanyika katika maeneo ya mjini mwa wilaya hiyo.
Baada ya hapo ratiba za audition zitaendelea kama ifuatavyo;
Agosti 29- Kilimanjaro/ Sanya juu
Usaili utafanyika katika mji wa Bomang’ombe
Agosti 30- Arusha/ Ngorongoro
Usaili utafanyika Karatu
Agosti 31 – Singida
Usaili utafanyika Singida Mjini
Septemba 1- Iramba
Usaili utafanyika Iramba Mjini
Septemba 2- Dodoma
Usaili utafanyika Kondoa Mjini
Hii ni awamu ya kwanza ya usaili wa shindano hili, audition zitaendelea stay tuned kwaajili ya tarehe na mahali ya auditon zitakazoendelea……….
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...