Meneja Mwandamizi Mahusiano ya Wateja wa CRDB, Silas Katemi (wa pili kulia) akitoa maelezo kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana ya utaratibu mpya wa ukopeshaji pesa za ununuzi na ujenzi wa nyumba za makazi kwa wateja wake ‘CRDB Home Loans,’ wakati wa Maonesho ya Pili ya Sekta ya Nyumba ‘Tanzania Homes Expo 2012 yaliyomalizika jana jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Ofisa Mauzo wa CRDB. (Picha na Habari Mseto Blog)
Baadhi ya Maofisa wa Benki ya CRDB walkiwa katika picha ya pamoja wakati wa maonesho Maonesho ya Pili ya Sekta ya Nyumba ‘Tanzania Homes Expo 2012 yaliyomalizika leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Ofisa Mauzo wa CRDB, Theresia Lubogo, Meneja Mwandamizi Mahusiano ya Wateja wa benki ya CRDB Silas Katemi, Nirrah Chemchem, Neema Daniel na Ofisa Masoko wa CRDB, Ninael Munuo.
Meneja Mwandamizi
Mahusiano ya Wateja wa benki ya CRDB, Silas Katemi (kushoto) akitoa maelezo kwa
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Prof. Charles Kitwanga ya utaratibu mpya wa ukopeshaji pesa za ununuzi na
ujenzi wa nyumba za makazi kwa wateja wake ‘CRDB Home Loans,’ wakati wa
Maonesho ya Pili ya Sekta ya Nyumba ‘Tanzania
Homes Expo 2012 yaliyomalizika leo jijini Dar es Salaam.
BENKI
ya CRDB imetambulisha utaratibu
mpya wa ukopeshaji pesa za ununuzi na ujenzi wa nyumba za makazi kwa wateja
wake ‘CRDB Home Loans,’ utakaowawezesha watu binafsi na waajiriwa kumiliki
makazi bora na ya kisasa kwa riba ndogo.
Akizungumza na Tanzania Daima wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya Sekta ya
Nyumba ‘Tanzania Homes Expo 2012, Meneja Mwandamizi Mahusiano ya Wateja wa CRDB,
Silas Katemi, alisema kipindi cha ulipaji wa mkopo wa Home Loans ni kirefu hadi
miaka 20.
Aliwataka
Wanzania kutembelea matawi ya CRDB yaliyo karibu yao ili kupata maelezo kuhusu
CRDB Home Loans – utaratibu rahisi, wenye riba ya kuvutia na unaomuwezesha kila
mteja wa benki hiyo, mwajiriwa na asiye mwajiriwa kumudu kuulipa taratibu
tofauti na kampuni au mabeki mengine.
“Miradi
ya ujenzi wa makazi bora kwa Watanzania kwa sasa inahusisha kampuni mbalimbali
kama unavyoziona hapa, ushindani huu umetusukuma sisi CRDB kuweka riba ndogo kati
ya asilimia 16 hadi 20 ambayo itamvutia kila mmoja,” alisema Katemi.
Katemi
aliongeza kuwa, gharama za ujenzi kwa sasa ziko juu, hali inayowakwamisha
wateja wengi kujenga makazi bora kwa awamu moja hivyo kufanya ujenzi wa
‘kuungaunga,’ lakini kupitia CRDB Home Loans, wateja watajenga na kununua mara
moja, kisha kulipa taratibu. Tanzania
Homes Expo 2012 ni maonesho ya pili kufanyika nchini, ambapo mwaka huu
yalifunguliwa Ijumaa kwenye Viwanja vya Mlimani City na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni
Jordan Rugimbana na kushirikisha kampuni mbalimbali zinazojihusisha na sekta ya
nyumba.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...