Ujumbe wa Sekretarieti ya CCM,ukiongozwa na Katibu Mkuu,Ndg. Abdulrahman Kinana,Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro na Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye ukiwa katika matembezi ya kuangalia maendeleo ya Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Malagarasi na Ujenzi wa Barabara ya kutoka Kidawe mpaka Uvinza kwa kiwango cha lami leo.
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana (kushoto) akizungumza na Meneja wa Kampuni ya HANIL ambao ni Wakandarasi wa ujenzi wa Daraja hilo,Bw. Jung-Sik You kutoka nchini Korea.
Meneja wa Kampuni ya HANIL ambao ni Wakandarasi wa Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Malagarasi na Ujenzi wa Barabara ya kutoka Kidawe mpaka Uvinza kwa kiwango cha lami,Bw. Jung-Sik You (kushoto) akitoa maelezo machache juu ya maendeleo ya ujenzi wa Daraja hilo kwa Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana na kuahidi kuwa mpaka ifikikapo mwezi Septemba ama Oktoba,Daraja hilo litakuwa limeshakamilika na kulikabidhi kwa Serikali.
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Nguruka,Wilayani Uvinza Mkoani Kigoma leo,waliojitokeza kwa wingi kumsikiliza na pia kusikiliza shida zao wakati alipofanya ziara ya kutembelea vijiji viwili vya Wilaya hiyo ya Uvinza.
Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akiwasalimia wananchi wa Kijiji cha Nguruka,Wilayani Uvinza Mkoani Kigoma leo.
Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Uvinza,Wilayani Uvinza mkoani Kigoma leo.

BOFYA HAPA KUONA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...