Waziri wa Viwanda na Biashara,Dkt. Abdallah Kigoda (wa pili kulia) akikagua shughuli za Ujenzi wa kiwanda hicho huku akipewa maelezo na Meneja wa Mradi huo.kazi za ujenzi wa kiwanda hicho cha Cementi inaendelea kwa kasi sana.
Waziri wa Viwanda na biashara,Abdallah Kigoda akipata taarifa fupi ya kazi za ujenzi wa kiwanda cha Simenti toka kwa Mkurugenzi wa Meis Industries,Merey Ally Saleh. 
kazi za ujenzi zinaendelea katika kiwanda hicho kinachotarajiwa kuanza uzalishaji April mwakani.

Na Abdulaziz,Lindi

Zaidi ya dola milioni 30 zinatarajia kutumika kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha Lindi simenti ambacho kimeanza ujenzi wake mapema mwenzi feb na kinatarajia kumamilika baada ya miezi 14 kuanzi sasa.

Hayo yamebainishwa na mkurugenzi mtendaji wa Meis Industries company Ltd,, Merey Ally Saleh alipokuwa anazungumza na waziri wa viwanda na biashara Abdala Kigoda wakati alipotembelea kuangalia maendeleo ya ujenzi wa kiwanda hicho .

Meley alisema kukamilika kwa ujenzi wa kiwanda hicho kutasaidia kuajiri watu zaidi ya 1000 na kitakuwa na uwezo wa kuzalisha tani 600 hadi 700 za sement kwa siku ambayo Itasaidia wakazi wake kupata bidhaa hiyo kwa bei nafuu kuliko hivyo sasa.

Alisema kiwanda pia kitatumia raslimali zinazopatikana hapa nchini kwa asilimia 95 na asilimia tano bidhaa za kutoka nje ambazo ni kemikali za kuumulia udongo na kufanya kuwa sementi.

Kwa upande wake waziri wa viwanda Abdalah Kigoda ameipongeza kampuni ya Meis kwa kitendo cha kufikiria kujenga kiwanda hicho na kueleza kuwa kitakuwa kichocheo kikubwa cha maendeleo kwa mikoa ya kusini Lindi na Mtwara na kupunguza tatizo la ajira lililopo.

Kigoda alisema kiwanda hicho kitakuwa cha nne kwa ukubwa ambacho kinatumia raslimali za ndani kwa asilimia kubwa kama vile viwanda vya Twiga sementi, Tanga sementi na Lindi Sementi.

Alisema serikali inaona juhudi za wawekezaji na hivyo basi iko katika utaratibu wa kuondoa changamoto cha ukosefu wa umeme ambao umekuwa kero kubwa kwa wawekezaji wa viwanda hapa nchi kwa kuharakisha miradi ya uvunaji wa gesi kwa ajili ya nishati hiyo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...