Waziri wa Viwanda na Biashara,Dkt. Abdallah Kigoda (wa pili kulia) akikagua shughuli za Ujenzi wa kiwanda hicho huku akipewa maelezo na Meneja wa Mradi huo.kazi za ujenzi wa kiwanda hicho cha Cementi inaendelea kwa kasi sana.
Waziri wa Viwanda na biashara,Abdallah Kigoda
akipata taarifa fupi ya kazi za ujenzi wa kiwanda cha Simenti toka kwa
Mkurugenzi wa Meis Industries,Merey Ally Saleh.
kazi za ujenzi zinaendelea katika kiwanda hicho
kinachotarajiwa kuanza uzalishaji April mwakani.
Na Abdulaziz,Lindi
Zaidi ya dola milioni 30 zinatarajia kutumika kwa ajili ya ujenzi wa
kiwanda cha Lindi simenti ambacho kimeanza ujenzi wake mapema mwenzi
feb na kinatarajia kumamilika baada ya miezi 14 kuanzi sasa.
Hayo yamebainishwa na mkurugenzi mtendaji wa Meis Industries company
Ltd,, Merey Ally Saleh alipokuwa anazungumza na waziri wa viwanda na
biashara Abdala Kigoda wakati alipotembelea kuangalia maendeleo ya
ujenzi wa kiwanda hicho .
Meley alisema kukamilika kwa ujenzi wa kiwanda hicho kutasaidia
kuajiri watu zaidi ya 1000 na kitakuwa na uwezo wa kuzalisha tani 600
hadi 700 za sement kwa siku ambayo Itasaidia wakazi wake kupata bidhaa
hiyo kwa bei nafuu kuliko hivyo sasa.
Alisema kiwanda pia kitatumia raslimali zinazopatikana hapa nchini
kwa asilimia 95 na asilimia tano bidhaa za kutoka nje ambazo ni
kemikali za kuumulia udongo na kufanya kuwa sementi.
Kwa upande wake waziri wa viwanda Abdalah Kigoda ameipongeza kampuni
ya Meis kwa kitendo cha kufikiria kujenga kiwanda hicho na kueleza
kuwa kitakuwa kichocheo kikubwa cha maendeleo kwa mikoa ya kusini
Lindi na Mtwara na kupunguza tatizo la ajira lililopo.
Kigoda alisema kiwanda hicho kitakuwa cha nne kwa ukubwa ambacho
kinatumia raslimali za ndani kwa asilimia kubwa kama vile viwanda vya
Twiga sementi, Tanga sementi na Lindi Sementi.
Alisema serikali inaona juhudi za wawekezaji na hivyo basi iko
katika utaratibu wa kuondoa changamoto cha ukosefu wa umeme ambao
umekuwa kero kubwa kwa wawekezaji wa viwanda hapa nchi kwa kuharakisha
miradi ya uvunaji wa gesi kwa ajili ya nishati hiyo
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...