Ankal na bendi yake aliyoipa jina la Orchestre les Libeneke akiwa mazoezini na vijana wake kwenye kambi ambayo kwa sasa jina kapuni kwa kuhofia wadaku. Tayari bendi hiyo ina nyimbo nne huku ikifanyia kazi mbili zaidi, kabla ya kuingia studio kurekodi. 

Akiongea na mwandishi wetu wa maswala ya burudani kwa njia ya simu, Ankal amesema ameamua kujiingiza katika muziki kwani umo ndani ya damu yake ambapo kaka yake mkubwa Ismail ni mmoja wa waanzilishi na wanamuziki wa awali wa Dar International ya Marijani Rajabu. Pia Ankal anasema anafanya sana mazoezi na Wananjenje na hivi sasa anakaribia kuhitimu kupiga drums. 

Hakupenda kuweka bayana bendi itazinduliwa lini na wapi, ila alisisitiza ni kabla ya SabaSaba mwaka huu. Hivi sasa anatafutwa producer mkali wa kurekodi nyimbo zao pamoja na video. Huenda wakamtumia tiketi Producer mkali Miika Mwamba aliko huko Sweden  aje ashurikiane na wakali wa nyumbani kufanya vituzzzz.
Ankal akiwa na kijana wake Omary Makuka ambaye naye alipigia Dar International. Kwa sasa wanakamilisha nyimbo mbili za mwishio kabla ya kuingia studio. Katika hizo sita mbili ni 'Remix' ya ngoma za 
Marijani Rajabu 'Mayasa' na 'Rosa Nenda Shule'

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 56 mpaka sasa

  1. Uzinduzi lini na wapi? Ningependa kukuona unaimba.

    ReplyDelete
  2. happy fools day

    ReplyDelete
  3. APRIL FOOLS.....
    Asante kwa kuniamsha na joke ya mwaka ankal!!!

    ReplyDelete
  4. Balozi TsereApril 01, 2013

    Saafi sana ankal tuko pamoja!

    ReplyDelete
  5. Ni kweli Ankal, nimekuona live na bendi jana sikukuu ya Pasaka kule mbugani halafu Kibo Sounds wakapanda jukwaani kuwapeni muda wa kupumua baada ya bendi yako Orch Les Libeneke kulazimishwa kupinga muziki masaa sita bila mapumziko na wadau uliopagawa na kazi yenu nzuri, show ilikuwa siyo mchezo.

    lini bebdi yako itafanya collabo na Msondo Ngoma au Mlimani Park ili wadau wa Dsm nao wafaidi?
    Mdau
    Mtalii wa Ndani

    ReplyDelete
  6. 1 April safi sana

    ReplyDelete
  7. Fools day... Thank you sir.

    ReplyDelete
  8. hapa utawapata wengi ANKAL

    ReplyDelete
  9. Good try Ankal.
    Siku ya wa..... hoyeeeee.

    Mwilima, NYC

    ReplyDelete
  10. Bw. Michuzi leo ni siku ya wajinga dunia!!!

    ReplyDelete
  11. Leo ni siku ya wajinga, wadaganye!

    ReplyDelete
  12. Siku ya wajinga duniani

    ReplyDelete
  13. HAHAHAHAHAHA DAH.. VERY SOON UNCLE UTAANZISHA CLUB YAKO YA MPIRA ( FC. LIBENEKE)

    BY TH WAY LEO NDO 1ST APRIL SIO???????????????????

    ReplyDelete
  14. Hongera sana ankal,kwahiyo unakwenda kama Nyoshi William?anyway kwangu leo hujanipata.

    MDAU TOKA K'KOO

    ReplyDelete
  15. kazi ipo

    ReplyDelete
  16. April fools day. Well try not this time ingawa una sauti kama ya Michael Jackson but this sounds fake April fools day.

    ReplyDelete
  17. kwikwikwi. hahahaha..mbavu zangu kwishnehy..
    2015 ntakubook kwenye kampen zangu za ubunge kwa tkt ya M4C. tafadhali usinisepe
    mdau USA

    ReplyDelete
  18. Sikukuu ya wajingaaa, SIDANGANYIKI
    Willy

    ReplyDelete
  19. Ankal haya sio mambo ya 1st April kweli? teheteheteheeee!!

    ReplyDelete
  20. Siku ya wajinga Leo, Hanna cha bendi wala kwaya, producer wala dj, Sweden wala mbagala.

    ReplyDelete
  21. Fools day ankal ujatupata hapo! Band na ankal wapi na wapi........camera zitaota kutu

    ReplyDelete
  22. Tafadhali!!!!,tafadhali!!!!Ankal hatutaki wawepo wacheza show maana vijana wa siku hizi wa zama za dijitali hawana adabu hata kidogo maana nina hakika mapigo ya bendi yetu yatakuwa ni ya kiutu uzima ya zama za analoji.

    ReplyDelete
  23. ANKAL APRIL MOSI NINI?

    ReplyDelete
  24. April Fool!!!!!!!!!!

    ReplyDelete
  25. Sikukuu Ya ......

    ReplyDelete
  26. leo mjomba umpati mtuuuuu

    ReplyDelete
  27. 1st April, fools' day!!!!1

    ReplyDelete
  28. April fool!! Hamnipati ng'o nimewashtukia!!

    ReplyDelete
  29. wajingaz day! Humpati mtu ankal

    ReplyDelete
  30. Yes, one of the best April Fools prank I have seen so far!

    ReplyDelete
  31. Hongera sana uncle Michuzi

    ReplyDelete
  32. Ankal hiyo umpati mtu

    ReplyDelete
  33. ankali sio mbaya kuchangamsha blog lakini tuangalie hizi skukuu tunazozishabikia zina faifa gani kwa sisi wabantu?

    hivi kweli sisi wabantu na skukuu za kuiga tunaendana au ndio kwenye msafara wa wanyama hata panya yupo?

    hizi skuu za wajinga hatuna haja nazo sisi wabantu tupiganie njaa zetu

    wenzetu wameshashinda hili game la maisha ndio ukaona wanakuwa na skuu za ajabu ajabu

    wenzetu hawana shida ya UMEME,MAJI,NJAA,ELIMU,MATIBABU,KAZI,MAKAZI,N.K

    Shukrani kwa kutuchangamsha lakini kiukweli tusizifate hizi sio zetu.

    ReplyDelete
  34. Mhhhh!!!machale yamenicheza,SIKU YA WAJINGA.

    ReplyDelete
  35. April fools!

    ReplyDelete
  36. Pole ankal! kidogo umechelewa baba Sela mbona wenzio wameanzaga mapema sana ushindani utauweza na Banza, Ila pia nikupe hongera, angalau utasema ulijaribugi

    ReplyDelete
  37. Leo ni April 1st? Nimekubamba!

    ReplyDelete
  38. Mnh! Ankal, leo ni siku ya wajinga.

    ReplyDelete
  39. HII NDIO MAANA YA MJASIRIMALI AU ENTREPRENEUR ankal unakipaji hiki

    ReplyDelete
  40. I Hope sio April fools day

    ReplyDelete
  41. april fools..hahaa ankaaaal

    ReplyDelete
  42. ankal hujakamata hata mmoja! leo umekamatwa weye yakhe
    --bpm

    ReplyDelete
  43. hongera lakini mbona unaimba huku umeshika simu?

    ReplyDelete
  44. Fools day au?

    ReplyDelete
  45. Ankal - Hongera, lakini siyo sikukuu ya wajinga hii

    ReplyDelete
  46. Siku ya awnings

    ReplyDelete
  47. April 1, everyone knows that.

    ReplyDelete
  48. Ankal,judging by the date of this post;I think you are pulling my leg...Happy april fools' day..

    ReplyDelete
  49. aaaaa ap-- foolish

    ReplyDelete
  50. Happy Fool's day!!

    ReplyDelete
  51. *APRIL FOOLS DAY*!!!!!

    ReplyDelete
  52. ankal leo ni sikukuu ya wajinga...hujui kuimba, hujui kucheza, una aibu sana kusimama mbele za watu, mkeo hata kuruhusu, huna kipaji...kiufupi si mwanamziki..!!

    Hapi april fools!

    mdau
    uswis

    ReplyDelete
  53. Ankal ! hongera sana sana,umepiga hatua kubwa sana sana,kila kitu kinawezekana,tunataka kuona vitu kama hivi vinavyodumisha na kuendeleza muziki wa dansi na utamaduni wa muziki wa dansi wa kiswahili.
    Safi sana,babu kubwa.
    wadau
    FFU ughaibuni

    ReplyDelete
  54. Tukumbuke leo ni 1-04-2013 yaani siku ya wajinga duniani,msisahau siku hii ya leo

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...