MAREHEMU PIUS WILFRED SHANGALI.
Ni Miaka 5 sasa tangu
ulipotutoka ghafla alasiri ya tarehe 30/4/ 2008 huko nchini Ujerumani.
Hakika ilikuwa ngumu sana kukubaliana na taarifa za kifo chako kwani ni wiki 2 kabla ya
taarifa hizo ulikuja kutusalimia hapa nyumbani Tanzania, Laiti tungejua ulikuwa
umekuja kutuaga na hatutaonana tena. Mpendwa na kiongozi wa familia yetu,
tunaamini umepumzika kwa amani, japo hatuko nawe kimwili lakini imekuwa vigumu
mno kukusahau kulingana na umuhimu na nafasi uliyokuwa nayo kwenye familia
yetu.
Unakumbukwa
na Wazazi wako Mr & Mrs W. Shangali,dada na wadogo zako
Suzy,Jane,Theophil,John,Christer na Bertha. Umetuachia fumbo zito lakini
kwa yote tunamshukuru Mungu kwani umetuachia mengi ya kuiga, Hekima zako,
upendo, upole, uvumilivu vimebaki mioyoni mwetu na tutavienzi daima.
Tunaamini kukutana paradiso ya milele. upumzike
kwa amani kaka Pius.
Jina la Bwana libarikiwe . Amen.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...