Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Makamu wa Rais Dkt.Mohamed Gharib Bilal  na Waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe wakiwa katika picha ya pamoja na mabalozi wapya waliopaishwa leo ikulu jijini Dar es Salaam.aliyesimama mbele kushoto no Balozi Liberata Mulamula anayekuwa Balozi Mpya wa Tanzania nchini Marekani.Waliosimama nyuma kutoka kushoto ni Balozi mpya wa Tanzania Uholanzi Wilson Masilingi,Balozi mpya wa Tanzania katika visiwa vya Commoro Chabaka Kilumanga,Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania Umoja wa Mataifa Geneva Balozi Modest jonathan Mero na Balozi mpya wa Tanzania katika falme za Kiarabu(UAE)Mbarouk Nassor Mbarouk.Kabla ya uteuzi Balozi Liberata Mulamula alikuwa msaidi wa Rais Masuala ya kidiplomasia na aliwahi kuwa katibu mkuu wa nchi za  Maziwa Makuu.(picha na Freddy Maro). 
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo ikulu jijini Dar es Salaam amemwapisha Jaji  Aloycius Mujuluzi kuwa Mwenyekiti wa  tume ya kurekebisha sheria pamoja na mabalozi wanne watakaoiwakilisha Tanzania nje ya nchi.Mabalozi walioapishwa leo ni pamoja na Balozi mpya katika umoja wa Falme za kiarabu(UAE) Mbarouk Nassor Mbarouk,Balozi mpya wa Tanzania nchini Uholanzi Wilson Masilingi,Balozi mpya wa Tanzania katika visiwa vya Commoro Chabaka Kilumanga na Mwakilishi wa  kudumu Tanzania Umoja wa mataifa Geneva Balozi Modest Jonathan Mero.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 23, 2013

    Hongera sana Balozi Liberata Mulamula kwa kuapishwa kuwa Balozi wa Marekani. Tunaomba ukaendeleze kazi kama Balozi Mwanaidi Maajar, uwe Balozi wetu mzuri, wasilisha Tanzania wasilisha wanawake.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...