Kundi
la kwanza la wasanii watakaotumbuiza katika tamasha la Kilimanjaro
Music Tour 2013 limewasili mkoani Kigoma kwa ajili ya onyesho hilo.
Wasanii hao 8 ni kati ya 12 watakaopanda katika jukwaa moja uwanja wa
Lake Tanganyika siku ya Jumamosi.
Kundi la pili la wasanii ambao ni Profesa Jay, Diamond, Lady Jaydee na Barnaba wanatarajiwa kuwasili siku ya Jumamosi asubuhi.
Baada
ya kupata mlo wa mchana ulioandaliwa na mwenyeji wao ambaye ni Doctor
Gerrard Mipango wasanii hao walipata nafasi ya kutembelea makumbusho ya
Doctor Livingistone yaliyoko Ujiji na kujionea historia mbalimbali ya
mzungu huyo anayetambuliwa kama mvumbuzi wa Ziwa Tanganyika na pia kuona
maeneo biashara ya utumwa ilipokuwa ikifanyika na kujifunza kuhusu
asili ya wenyeji wa Mkoa wa Kigoma.
Wasanii wakiwa katika eneo la mbele ya makumbusho ya Doctor Livingstone.
Wakali wa muziki katika picha ya pamoja na wenyeji wao mkoani Kigoma.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...