Na Abdulaziz Video,Dodoma

WAKULIMA wa zao la korosho nchini wametakiwa kubadili mitazamo yao kuona zao hilo kuwa la kudumu badala ya kuliona la kujikimu kwa muda na kusababisha kushuka kwa uchumi wao, na kuendelea kuwa masikini, kila mwaka.

Hayo yamebainishwa na waziri wa Kilimo, chakula na ushirika Mhandisi Christopher Chiza wakati alipokuwa anafungua mkutano wa wadau wa korosho wa siku mbili ulifanyika mjini Dodoma.

Chiza aliyasema hivi sasa za la korosho linazidi kupanuka kiuzalisha kwa kuongezeka kutoka wilaya 34 hadi 41 na mikoa tisa mipya inayolima zao hilo Mbeya, Iringa,Njombe, Morogoro,Dodoma Singida Alisema kuwa zao hilo bado halijaweza kutoa tija kwa wakulima, kwa hiyo aliwataka watendaji kutumia vyema kikao hicho kujadili kwa kirefu juu kuleta mabadiliko kwa wakulima na kuondokana na umasikini.

Waziri Chiza alifananisha na mazao mengine ya kudumu kama, Kahawa, migomba ya ndizi, Pamba ambayo yaliweza kuleta sura nzuri ya kiuchumi kwa wakulima wa mazao hayo.

Hata hivyo aligusia swala zima la ubanguaji wa zao la Korosho, kuwepo na jopo maalumu ambalo litaweza kukaa pamoja na kuhakikisha zao hilo linabanbuliwa nchini.

Aliongeza korosho inayosafirishwa ghafi inasababisha hali ya wakulima kuendelea kuwa masikini.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho Tanzania Anna Abdallah alisema kuwa viwanda bado vinashikiliwa na wafanyabaishara wabangue hapa hapa nchini.

Alisema kuwa korosho ghafi soko lake liko sehemu moj tu ni nchini india jambo linalosababisha kuleta mgongano wa kimaslai kati ya wanunuzi watendaji wa sekta ya ushirika na walimu
Waziri wa Kilimo,Chakula na Ushirika,Eng. Christopher Chiza akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wadau wa korosho wa siku mbili ulifanyika mjini Dodoma.
Baandi ya Wajumbe wakiwa kwenye mkutano huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Tatizo sugu la Kihistoria nchini Tanzania lipo katika Mfumo wa Masoko ya mazao ya Wakulima:

    (i)-BODI ZA MAZAO:
    1.Kahawa,
    2.Korosho,
    3.Pamba,
    4.Chai,
    5.Pareto,


    (ii)-HALMASHAURI:

    (iii)-WADAU NA MADALALI (vishoka):

    Serikali ivunje Udhalimu huo hapo juu (REGIME) ndio mambo yaweze kuwa mambo kwa Wakulima.

    Sasa kutokana na Mfumo huo hapo juu Dhalimu wa 'KARATA TATU' (i), (ii) na Masoko (iii) ndio sababu Mkulima anazidi kuwa Masikini hivyo kulichukulia zao kama la kumpatia Tija ya muda tu ambapo kilimo kinakuwa ni cha kujikimu na si kama Biashara!!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...