Sherehe za mapinduzi ya Zanzibar zilivyofana New York , Sherehe hizo zilipendezeshwa kwa show ya mavazi, chakula na music wa Asili ya mwambao kutoka kwa Dj Bilal. Balozi wa kudumu wa umoja wa mataifa New York Mh. Tuvako N. Manongi ndiyo alikuwa mgeni rasmi wa sherehe hizo. Na alitoa hotuba fupi juu ya history ya mapinduzi. Na mama Ashura Babu pia kama ilivyo kwa Mh. Balozi Manongi alipata fulsa ya kuelezea mapinduzi hayo ya Zanzibar kwa ufupi.
Katibu wa community ya Watanzania New York bwana Mhella akitoa hotuba fupi ya kuwatambulisha viongozi na kuwakaribisha ukumbini hapo.
Mh. Balozi Tuvako Manongi akiongea historia fupi ya Mapinduzi ya Zanzibar katika sherehe hio
Aunt Ashura Dualle nae akitoa hotuba fupi juu ya Mapinduzi ya Zanzibar. Aunt Ashura anakumbukumbu  sahii ya Sherehe hizo kwa sababu alikuwa mke wa marehemu mwanamapinduzi hayo Abdulhaman Babu.
Mwenyekiti wa community ya Watanzania New York bwana Hajji Khamis akimtambulisha kiongozi wa Zanzibar Diaspora kabla ya Mh. Balozi kuongea.
Kiongozi wa Zanzibar Diaspora kutoka, PA akiongea ukumbuni hapo
Naibu katibu wa Community Mariam Abu akiongea
Wageni waalikwa kutoka New York Life Insurance Comapny wakielezea umuhimu wakujiunga na Bima ya maisha.
Bwana Amani Kitali  akizungumzia mambo ya maendeleo yanayotakiwa kufanywa na Watanzania wanaoishi na kufanya kazi nchi za nje.
Chini na juu mshereheshaji wa sherehe hizo Gaston akifanya vitu vyake
Msami akitoa burudani iliyowaacha wa mbavu zimetanuka kwa kicheko. 
Jessica kushoto ndiyo aliefanikisha mavazi haya ya Kinzanzibar, pongezi kwa Jessica kwa kazi mzuri pamoja na dada Asia Mwilima kwa kuweza kutoa ufafanuzi wa mavazi hayo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Safi sana New York. Wenye donge na wasage chupa. Mmetutoa kimasomaso wanzanzibar! Shukrani.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...