Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akipata maelezo mafupi kutoka kwa wenyeji wake kuhusiana na ujenzi wa hatua za awali za bandari ya Kabwe,wilayani Nkasi mkoani Rukwa.
Katibu Mkuu wa CCM;ndugu Kinana akiwahutubia wakazi wa kijiji cha Kirando,wilayani Nkasi mapema jana jioni.Kinana alisema kuwa tahakikisha Barabara ya kutoka Sumbawanga mjini kwenda kijiji cha kabwe itatengenezwa kwa kiwango cha lami."Nitaenda na mbunge wenu kushinikisha suala la barabara hii ili ijengwe kwa kiwango cha lami na kuwarahisishia sughuli za kibiashara"alisema.Alisema kuwa maendeleo hayawezi kuja ikiwa miundombinu ni mibovu hivyo atahakikisha analifikisha kwa waziri mwenye dhamana pamoja na mkuu wa nchi ili kazi hyo ifanyike mapema.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akiwahutubia wananchi na wanachama wa CCM,mapema jana jioni katika kijiji cha Kabwe,Wilayani Nkasi.Kinana alisema kuwa, Serikali inatambua matatizo ya wananchi wa kjijini hapo ikiwemo suala la pembe jeo, maji pamoja na uvamizi wa wavuvi. "Miradi yote inayotekelezwa nchi nzima kwa sasa ni utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya mwaka 2010, hatubagui kwakua wote ni watanzania"alisema.Alisema kuwa Serikali inatambua kuwa shughuli kubwa ya kijini hapo ni uvuvi hivyo itajitahidi kuwe na utaratibu wa kuwasaiidia kupata mikopo ili waweze kununua zana za uvuvi ili waweze kujiendeleza.
Katibu
Mkuu wa CCM,Abdulrahman Kinana akiangalia samaki katika kiwanda kidogo
cha kuhifadhia samaki na kuuza katika kijiji cha Kabwe,Wilayani Nkasi
mkoa wa Rukwa mapema leo,ambapo pamoja na mengine Ndugu kinana alifanya
mkutano wa hadhara ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku 21 katika
mikoa ya Rukwa,Katavi na Kigoma,ziara hiyo ikiwa na lengo la kuimarisha
Uhai wa chama,kusikiliza kero mbalimbali za wananchi na kukagua miradi
mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa kwa kufuata ilani ya CCM.
Samaki
aina ya Migebuka ikiwa imeandaliwa kwa ajili ya kukaushwa kabla ya
kuhifadhiwa kwenye majokofu na kusafirishwa maeneo mbalimbali,ndani na
nje ya nchi.
Katibu
Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akizungumza jambo na Mbunge wa Jimbo la Nkasi
Kaskazini,Mh.Ally Keisy alipokwenda kukagua ujenzi wa bandari ya Kabwe
katika hatua za awali na kujionea shughuli mbalimbali za uvuvi
zinazofanyika katika kijiji hicho kabwe.
Ndugu Kinana akishiriki ujenzi wa Ofisi ya CCM katika kijiji cha Kabwe,wilayani Nkasi mkoani Rukwa mapema leo jioni.
PICHA ZAIDI BOFYA MICHUZIJR.BLOGSPOT.COM
PICHA ZAIDI BOFYA MICHUZIJR.BLOGSPOT.COM
smoke screen...
ReplyDelete