Ankal akijiandaa kuingia ndani ya ndege yake ndogo inayoweza kutua popote aliyoinunua hivi karibuni kutoka katika visiwa vya Ushelisheli (Seychelles Islands) ili kuepukana na adha ya foleni jijini Dar es salaam. 
Ankal ameiambia Globu ya Jamii kwamba amekuwa akisomea urubani wa ndege hiyo kwa siri kwa mwaka mmoja na sasa ameshatimiza  masaa 450 hewani na tayari ameshapata leseni ya kupaa katika jiji la Dar (mchana tu, kati ya saa 12 asubuhi hadi saa 12 jioni) na kutua katika viwanja mbalimbali vikiwemo vya Gymkhana (kwa wilaya ya Ilala), Uwanja wa Taifa wa zamani (wilaya ya Temeke) na Biafra (wilaya ya Kinondoni) na Maisara (Unguja). 
Maombi yake ya kutua katika miji  mingine mikubwa kama vile Mbeya, Mwanza, Arusha, Rukwa, Katavi, Njombe, Dodoma na Morogoro yanashughulikiwa na huenda akafanikiwa mara baada ya sehemu za kutua katika mikoa hiyo zitapothibitishwa na mamlaka husika.
Ankal anakuwa blogger wa kwanza Mtanzania mwenye kumiliki ndege yake mwenyewe. Anasema hiyo ni hatua moja kubwa aliyokuwa akiiota miaka kadhaa wakati alipokuwa anafikiria si tu namna ya kupambana na foleni mijini, bali pia kufikia habari moto na kwa muda muafaka..

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 84 mpaka sasa

  1. Haaaa haaaa tumestuka LEO NI SIKU YA WAJINGA, hakamatiki mtu hapa!

    ReplyDelete
  2. Siku ya wajinga hiyo ha ha ha ha najua unawezo Ankal wangu lakini aaaaahhh...!! umetupiga changa la macho.

    ReplyDelete
  3. April's Fool>>> hehehee

    ReplyDelete
  4. Hongera sana Ankal. Mungu ni muweza wa yote kwake yeye aaminiye na kumtukuza. Mimi binafsi nimefurahishwa na hatua hii nzuri uliyoipiga kwani naamini itarahisisha kazi yako kwa kiasi kikubwa nasi tutafaidika pia.

    ReplyDelete
  5. April Fools Day....

    ReplyDelete
  6. SIKU YA WAJINGA DUNIANI. HONGERA KWA NDOTO NJEMA

    ReplyDelete
  7. Hahahaha ankal hongera sana kwa kupiga hatua kubwa Kama hiyo kwenye karne hii yenye changamoto nyingi kwa sie wabeba boksi, swali la kizushi mbona hii sehemu Kama pale uwanja wa nanihiu pembeni mwa jnia maana hizo rangi za jengo na Ac za sanyo zilizochoka malaya Kwikwi Kama hapa ni sychells as u said... jibu tafadhali na kumradhi Kama kwa mbaaaali ntakuwa nimekutibulia kwa bbys maana uzee umeisha kule kwenye kampeni so unajua tena bbys za mujini ukiwa na ka private jet tena mweh kwa ubuah..ni hayo tu

    ReplyDelete
  8. tehe tehe tehe......fools day

    ReplyDelete
  9. Siku ya wajinga ankal!! But was good one though!

    ReplyDelete
  10. Hongera sana Ankal na MUNGU akuzidishie am really proudly of you

    ReplyDelete
  11. Ankal,

    Hongera na pia sikukuu ya wajinga!

    ReplyDelete
  12. Karibu kwenye ulimwengu wa kupasua anga.... angalia jamaa wa TRA wasikupe usajili wa MH370

    Karibu Aprli 01

    ReplyDelete
  13. Wajinga Day Ankal

    ReplyDelete
  14. hongera sana kama kweli...ila nawasiwasiiiiiiii

    ReplyDelete
  15. tarehe moja mwezi wa nne,

    ReplyDelete
  16. Mjinga mwenyewe

    ReplyDelete
  17. Asante ankal.. Tunajua hii ni April Fools day.. Lakini kwa uhakika imekaa vizuri hii, fanya kweli basi.

    ReplyDelete
  18. siku ya wajinga

    ReplyDelete
  19. april fool!!!!!!!!!

    ReplyDelete
  20. Ankal safari hii hutu pati ;) 1/04 / 2014; )

    ReplyDelete
  21. I'm not fool. Hahaaa

    ReplyDelete
  22. 'You can fool people some time but you can't fool people all the time'.

    Don't try to hoodwink peole please

    Nimekuona eeeeee. April fool!

    ReplyDelete
  23. siku ya wajinga leo

    ReplyDelete
  24. Duh! Big up ankal. ...Hongera sana kaka!

    ReplyDelete
  25. Hongera, ha ha ha
    Nionavyo mimi ingekuwa bora kama ungejinunulia helichopa.

    ReplyDelete
  26. April wise men's day.
    Hahhaaaaaaaaa hutupati ng'o

    ReplyDelete
  27. Ankal kweli kaukata siyo mwenzetu tutakuwa tunamuona kwa juu lakini atatua wapi akiwa anaenda kwao kwani kuna uwanja wa ndege. Au ndiyo April fool.

    ReplyDelete
  28. Hahahaha. Ankal ungenunua kwanza fulana zingine kabla ya hiyo ndege.

    ReplyDelete
  29. Hongera sana uncally wetu kwa kununua ndege kwa ajili ya april/1 tu, kwani kesho hutakuwa nayo

    ReplyDelete
  30. Congratulations, big up, hongera sana, kila la kheri, Tegeta utatua kwenye uwanja gani, nataka niwe nawahi lift nitachangia wese.

    ReplyDelete
  31. Hongera Ankal (KAMA NI KWELI!!!)

    ReplyDelete
  32. siku ya wajinga duniani

    ReplyDelete
  33. Congratulations Ankal. Ila tu taarifa hizi zilipaswa kutufikia jana au kesho na sio leo kwakuwa leo ni tarehe 01/04/2014. Kwa wajanja mmeshaelewa ninachomaanisha.

    ReplyDelete
  34. Ankal na vijijini pia kuna shemu kuna viwanja.Omba pia kutuwa katika kiwanja cha kijiji kiitwacho TUTAYAONA kilichopo mpakani baina ya kijiji cha Kufikirika na Kusadikika katika wilaya ya Mambousiayaige.

    ReplyDelete
  35. JINGA`S Day

    ReplyDelete
  36. Anko hampati mtu, n'a April fool

    ReplyDelete
  37. hahaha anko asante kwa April full...

    ReplyDelete
  38. Is it April Fools day au nimekosea?

    ReplyDelete
  39. well done uncle happy fools day

    ReplyDelete
  40. APRIL FOOLS DAY!

    ReplyDelete
  41. Tumekushtukia Anakali, yaani hapa humpati mtu. Tarehe 1 Aprili hiyo.

    ReplyDelete
  42. Ni tarehe 1/4 so ankal kajipange upya!

    ReplyDelete
  43. Hongera sana Michuzi kwa hatua hiyo,Sasa ni News kwa kwenda mbele.

    ReplyDelete
  44. April Fools hiyo!

    ReplyDelete
  45. Hongera uncle kwa wazo zuri isije kuwa ni foolish day. Nachelea kuamini.

    ReplyDelete
  46. Sikukuu ya wajinga ....

    ReplyDelete
  47. shauri yanko ankali si uwezi wa kukutafuta DEEP SEA hatuna.

    ReplyDelete
  48. we ankal unafikiri hatujui kwamba leo ni siku ya wajinga

    ReplyDelete
  49. Ze Mamba:
    Kwi kwi kwi. Haya ankal, kanyaboya zuri sana, na nimelipenda. Umewapata wangapi? Kwi kwi kwi.

    On a serious note, inabidi ununue ndege ankal, maana wewe ni alwatani kwenye hili gemu.

    ReplyDelete
  50. Sikukuu ya wajinga leo.

    ReplyDelete
  51. Kaka nashukuru kwa kutukamata vizuri siku ya wajinga nami nimekuwa mjinga kwa leo asante sana mkuu wa kazi.
    Ila kwakuwa umenikamata vizuri nakuombea ununue helkopta kabisa ili kukidhi matakwa yetu sie wapenzi wa mi-newzzzzz ya kukata na shoka.

    ReplyDelete
  52. Ndio Mzee wa Libeneke! Napenda kutoa Pongezi kwa Jitihada zako na mafanikio ya kuliendeleza Libeneke! Pia Hongeza sana kwa Kumnunua huyo ndege ingawa inatia mashaka kuona ndege hana Jina! Ndio maana hisia zangu zinaniambia kuwa ni Jiwe la Fool's Day so Ngastuka Mzee! Nice try though! Ila kama ni kweli Hongera tena Uncle!

    ReplyDelete
  53. Uncle hili ni changa la macho sikukuu ya wajinga leo ,mdau wa Ukerewe

    ReplyDelete
  54. Braza michu acha hizo leo sikukuu ya wajinga

    ReplyDelete
  55. 1.4.2014

    ReplyDelete
  56. umeniokota kweli siku ya wajinga leo.du...

    ReplyDelete
  57. Hichi ni kibonzo cha Fulls Day! Good luck with that!

    ReplyDelete
  58. 1st April ni siku ya akina nani vile?

    ReplyDelete
  59. NADHANI LEO NI TRH 1

    ReplyDelete
  60. Sikukuu ya wajinga

    ReplyDelete
  61. Hapo kama Dar sa Salaam terminal 1 vile???.....hahahahaha.....April 1st

    ReplyDelete
  62. Hongera, weka nembo ya Fulanaz basi.

    ReplyDelete
  63. Hongera Ankal...lakini kununua hako kapipa siku ya April 1st mimi bado hujanipata.

    ReplyDelete
  64. April fool!!!! Misupu nimekushtukia....ha ha ha

    ReplyDelete
  65. "Fools Day 01 April ni Siku ya wajinga"

    Ankal kwa leo sitokupa Hongera
    labda kama ukitoa hizi habari tena
    kesho nitakupa hongera saana mkuu

    Mikidadi- Denmark

    ReplyDelete
  66. 1st april Ankal teh teh teh

    ReplyDelete
  67. Its april fooooool

    ReplyDelete
  68. Kama nakumbuka vyema tarehe kama hii mwaka fulani huko nyuma ankal aliteuliwa kuwa mkuu wa wilaya, sasa kanunua ndege, mhhh, mambo yake si mabaya!!!

    ReplyDelete
  69. Ndege hii inafafa ya kwangu niliyopaki mujini Dar es salaam. Imepata pancha ya tairi la kulia.

    Hongera sana

    Karibu kilabuni ankal

    pilot mzoefu

    ReplyDelete
  70. Leo si ile siku yao....!

    ReplyDelete
  71. April moja utawapata wengi ankal! lol!

    ReplyDelete
  72. Wooote nyie mmechemsha leo sio siku ya wajinga but the Mduduz day.

    ReplyDelete
  73. ukiwa mjinga...na sisi sio wajinga..

    ReplyDelete
  74. Ama kweli Fools Day! Ndege gani kutua uwanja wa biafra ambapo pamekuwa dimbwi la maji!!

    ReplyDelete
  75. kwa april2nd..... mimi nitanunua ikulu ndogo pale chamwino ankal, sitaki tena kukaa darchalama, kuna vumbi na fujo nyingi mno....ankal

    ReplyDelete
  76. Hakikisha unaisadili kwa number AK040114.

    ReplyDelete
  77. DUUH BRO HONGERA SANA ILE AHADI YAKO IME TIMIA KAMA TULIVYO ONGEA USUBIRI MPAKA SIKU KAMA YA LEO U BREAK NEWS NA KWELI USEMI WAKO WATU WATAFIKIRI APRIL CHANGA LA MACHO INA BIDI KUWAPA KIZARAMO KALAGA BAHO BIG UP BRO

    ReplyDelete
  78. Angalia usipotelee mto ruvu au wami kama malysia airline = april fool

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...