Waziri wa wa Kilimo Chakula na Ushirika Mh.Eng Christopher Chiza amewataka wanunuzi wa tumbaku kuja na mikakati mipya ili kuwanufaisha na kuimarisha soko la wakulima wa tumbaku.
Mhe. Chiza ameyasema hayo leo ofsini kwake alipokutana na Meneja mkuu wa kampuni ya ununuzi wa tumbaku kutoka kampuni ya JTI.
Pamoja na mambo mengine waziri amewataka wafanya biashara hao kuaanda mikataba kwa lugha ya Kiswahili na kingereza ili kuwafanya wakulima waelewe masharti na manufaa ambayo yanaweza kupatikana katika mikataba hiyo
Akiongea na meneja mkuu wa Kampuni hiyo Bwana Robert Glenn amewataka kuleta mabadiliko chanya kuanzia kwenye hatua ya ulimaji hadi kwenye soko la zao la tumbaku
Aidha naye Bwana Robert amesema kuwa Kampuni yake imejipanga kupeleka huduma za ugani kwa wakulima wa tumbaku ili kuongeza ushindani na wafanyabiashara wengine wa ndani na nje.
Waziri wa wa
Kilimo Chakula na Ushirika Mh.Eng Christopher Chiza akiongea na meneja mkuu wa Kampuni ya JTI Bwana Robert Glenn kuhusu ununuzi wa
zao la tumbaku.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...