SERIKALI imepokea msaada wa magari manne na pikipiki 20 zenye thamani ya sh. .261,105,615 kutoka Shirika la Wahisani la Kijerumani linalohudumia Ukoma na Kifua Kikuu (GLRA) kwa ajili ya kusaidia sekta ya afya.

Akipokea msaada huo Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid alisema Tanzania imefikia lengo la kimataifa la kutokomeza ukoma kwa kuwa chini ya mgonjwa mmoja katika watu 10,000 hivyo kufanya ukoma kutokuwa tatizo kubwa la afya nchini.

Alisema pamoja na kupokea msaada huo bado kumekuwa na changamoto ikiwemo za ukosefu wa magari na pikipiki kwa mikoa na wilaya mpya ambapo Serikali kupitia mpango huo unafanya jitihada za kupata vyombo vya usafiri katika mikoa hiyo.

Alisema vyombo hivyo vya usafiri vitapelekwa katika mikoa ya Kigoma, Tanga, Halmashauri za Ilala na Kinondoni ambapo aliomba  vitumika vizuri kulingana na malengo yaliyokusudiwa.

"Napenda kuuwaasa waganga wakuu wa mikoa na wilaya kusimamia kikamilifu matumizi ya vyombo hivi vya usafiri kwa kuhakikisha wale wote watakaokabidhiwa wanavilinda kwa kuvitumia vizuri kulingana na malengo yaliyokusudiwa na kwa kufuata taratibu za serikali na si vinginevyo," alionya.

Dk. Rashid alitoa wito kwa Halmashauri zote nchini kuangalia namna ya kuchangia gharama za matengenezo ya vyombo hivyo ili kuziba pengo la kupungua kwa misaada inayotolewa na wahisani.

Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Wahisani la Kijerumani linalohudumia Ukoma na Kifua Kikuu (GLRA), Burchard Rwamtoga (wa pili kushoto), akimkabidhi  Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk.Seif Rashid (kulia),moja ya ufunguo wa gari kati ya magari manne na pikipiki 20 vyote vikiwa na thamani ya sh.261,105,615, Dar es Salaam leo, zilizotolewa na shirika hilo kwa Serikali ya Tanzania kwa ajili ya kupambana na magonjwa hayo nchini. Wanashuhudia kutoka kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Charles Palanjo na Naibu Waziri, Dk. Steven Kebwe.
Naibu Waziri, Dk. Steven Kebwe (wa pili kulia), na viongozi wengine wa wizara hiyo wakiwa kwenye hafla hiyo. Kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Charles Palanjo, Mganga Mkuu wa Serikali Donan Mmbando na Mkurugenzi Msaidizi Afya na Usafi wa Mazingira, Elias Chinamo.
Pikipiki zilizotolewa kwa serikali.
Magari yaliyotolewa kwa Serikali.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Tunahukuru misaada hii, kama ilivyoelezwa itumike kama ilivyotarajiwa.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...