WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe amekutana na Mwanaharakati wa
Kimataifa wa haki za wanawake na watoto, Graca Machel na kujadili masuala mbalimbali ya
haki za wanawake na watoto katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam leo.
Katika mazungumzo yao, Waziri Chikawe alimwambia mke huyo wa Rais wa zamani wa Afrika
Kusini, Nelson Mandela, juhudi zake za kuingiza katika Katiba Mpya kifungu cha kuzuia mtoto
wa chini ya miaka 18 asioe wala asiolewe.
Hata hivyo, Mama Machel kwa upande wake alimshukuru Waziri Chikawe kwa maoni yake
na kusema kuwa ni muhimu kwa wadau wote wa haki za watoto wakashinikiza wajumbe wa
Bunge Maalum la Katiba na watunga sheria wote wahakikishe kipengele hicho kinaingia ndani
ya Katiba. Mama Machel yupo nchini kuhudhuria mkutano wa ufunguzi wa Kampeni ya Kitaifa
ya kutokomeza ndoa za utotoni.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (Kushoto) akizungumza na
Mwanaharakati wa Kimataifa wa haki za wanawake na watoto, Graca Machel katika
Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam leo. Waziri Chikawe alimueleza Mama Machel,
juhudi zake za kuingiza katika Katiba Mpya kifungu cha kuzuia mtoto wa chini ya miaka
18 asioe wala asiolewe.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kulia) akiagana na
Mwanaharakati wa Kimataifa wa haki za wanawake na watoto, Graca Machel baada ya
kikao chao kifupi kilichofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam leo. Waziri
Chikawe alimueleza Mama Machel, juhudi zake za kuingiza katika Katiba Mpya kifungu
cha kuzuia mtoto wa chini ya miaka 18 asioe wala asiolewe. Picha zote na Wizara ya
Mambo ya Ndani ya Nchi.
Jamanii usiniangalie mimi hivyo naona aibu....
ReplyDeleteTehe tehe tehe tehe tehe.... karibu tena Tanzania, nami ni jirani yako hapo Nachingwea njoo uitembelee nyumba MLIOISHI wakati wa vuguvugu la uhuru wa Nchumbiji...
Ntakutembeza UFURAHI...
nimeipenda hiyo comment ya kwanza...
ReplyDeleteMama anajua kujimaintain, ametoka kuomboleza mumewe anaendelea na kazi ya kuhamasisha ulimwengu katika maendeleo na haki za wakina mama na watoto.
ReplyDelete