Taasisi ya RafikiElimu FOUNDATION kupitia Mradi wa Elimu Ya Ujasiriamali Mijini & Vijijini, inatangaza nafasi za MAFUNZO YA UJASIRIAMALI. Mafunzo yatakayo tolewa ni pamoja na :
1. Jinsi ya kutengeneza mashine za kutotolea vifaranga wa kuku.
2. Uanzishaji na undeshaji wa taasisi zisizo kuwa za kiserikali.
3. Jinsi ya kutengeneza aina sita za soda
4. Jinsi ya kutengeneza bia aina mbali mbali
5. Jinsi ya kutengeneza vodka na pombe nyingine kali kwa vipimo
6. Jinsi ya kutengeneza fruit wine ( wine ya matunda mbali mbali)
7. Jinsi ya kutengeneza pipi, jojo (chewing gum), toffee n.k
8. Jinsi ya kutengeneza yogurt, ice cream na cheese
9. Jinsi ya kutengneneza tambi aina ya pasta.
10. Jinsi ya kutengeneza sabuni za kuogea
11. Jinsi ya kutengeneza scrub
12. Jinsi ya kutengeneza lotion
13. Jinsi ya kutengeneza manukato (perfumes) za aina mbalimbali.
14. Jinsi ya kutengeneza mafuta ya kupaka
15. Jinsi ya kutengeneza lip balm
16. Jinsi ya kutengeneza dawa mbalimbali za mimea zitokanazo na mimea tunayotumia kila siku
17. Jinsi ya kutengeneza vyakula lishe mbalimbali.
18. Jinsi ya kutengeneza Sabuni za mche
19. Jinsi ya kutengeneza Sabuni ya unga
20. Jinsi ya kutengeneza Sabuni ya maji
21. Jinsi ya kutengeneza Shampoo
22. Jinsi ya kutengeneza Dawa ya usafi chooni
23. Jinsi ya kutengeneza Dawa ya kusafishia Tiles.
24. Jinsi ya kutengeneza Mishumaa
25. Jinsi ya kutengeneza Chaki
26. Jinsi ya kutengeneza Tomato & Chilli Sauce
27. Jinsi ya Kutengeneza Jam ya Nyanya na Nanasi
28. Jinsi ya kutengeneza Biscuits
29. Jinsi ya kutengeneza Mkate wa ndizi
30. Usindikaji wa vyakula mbalimbali.
31. Jinsi ya kutengeneza kiwi
32. Jinsi ya kutengeneza blue band.
33. Usindikaji wa bidhaa za ngozi.
34. Somo la masaji
35. Ubunifu , uendeshaji na usimamizi wa miradi mbalimbali.
36. Uendeshaji na Usimamizi wa vikundi vya kuweka na kukopa fedha.
37. Utengenezaji wa vyakula vya mifugo.
38. Utunzaji wa wazee na watoto wachanga.
39. Kutunza na kulea watoto yatima.
40. Pamoja na vitu vingine vingi.
SIFA ZA MWOMBAJI :
1. Awe kijana wa kitanzania
2. Anaye jua kusoma na kuandika.
3. Kwa watakao taka kutosoma kozi namba 2, 35 na 36, mwombaji lazima awe na elimu ya kuanzia kidato cha nne na kuendelea.
ADA YA MAFUNZO :
Mafunzo haya yanatolewa bure.
FOMU ZA KUJIUNGA NA MAFUNZO :
Fomu za kujiunga na mafunzo haya zinapatikana ofisini kwetu kwa gharama ya SHILINGI ELFU KUMI NA TANO TU (Tshs.15,000/=)
OFISI ZETU zinapatikana jijini DAR ES SALAAM katika eneo la CHANGANYIKENI karibu na CHUO CHA TAKWIMU mbele ya CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM.
JINSI YA KUFIKA OFISINI KWETU :
Kufika ofisini kwetu panda daladala za MAWASILIANO TOWER - CHANGANYIKENI kisha shuka kituo cha TAKWIMU halafu tembea hatua ishirini mbele utaona ofisi imeandikwa RAEFO TANZANIA.
KWA WAOMBAJI WALIO NJE YA MKOA WA DAR ES SALAAM.
Kwa waombaji waliopo nje ya mkoa wa Dar Es salaam, mafunzo yatatolewa kwa njia ya posta. Jinsi ya kuomba,andika barua pepe ya maombi ya fomu ya kujiunga na mafunzo haya, nasi tutakutumia fomu yenye maelekezo yote.
Maombi yako yaandikwe kupitia barua pepe yetu : rafikielimutanzania@gmail.com
Maombi yaelekezwe kwa
Mkurugenzi Mtendaji,
RafikiElimu Foundation,
S.L.P 35967,
DAR ES SALAAM.
MWISHO WA KUPOKEA MAOMBI NI TAREHE 28 FEBRUARI 2015.
MAFUNZO YATAANZA TAREHE 02 MACHI 2015.
Kwa maelezo zaidi, piga simu 0688 049 687.
Au tembelea
www.rafikielimu.blogspot.com
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...