Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga, akizungumza na mama huyu mkazi wa kijiji cha Nyakunguru, kilicho jirani na eeno la mgodi wa North Mara, huko Nyamongo wilayani Tarime mkoa wa Mara, wakati alipofanya ziara ya kutembelea maeneo yanayozunguka mgodi huo Jumatatu Mei 5, 2015 ili kufahamu jitihada za mgodi kuendeleza miradi ya kijamii na changamoto ambazo Jamii na Mgodi zinapata kutokana na shughuli za uchimbaji.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga, (Wapili kushoto), akizungumza jambo wakati alipotembelea eneo la ujenzi wa nyumba moja kwa mtindo unaoitwa na wakazi wa Nyamongo “Tegesha”, mita chache kutoka uzio wa mgodi wa North Mara, ili kufahamu jitihada za mgodi kuendeleza miradi ya kijamii na changamoto ambazo Jamii na Mgodi zinapata kutokana na shughuli za uchimbaji. Naibu waziri amesikitishwa na mtindo huo ambapo wananchi hususan wanotoka nje ya eneo la Nyamongo, hujenga majengo haraka haraka eneo la kuzunguka mgodi huo kwa matarajio ya kujipatia malipo makubwa ya fidia kinyume na tathmini iliyofanywa awali.
 Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga, (kushoto), akisalimiana na Meneja Uendelezaji wa kampuni ya Acacia, Asa Mwaipopo, wakati alipofika kwenye kijiji cha Nyakunguru, kilicho jirani na mgodi wa North Mara, Mara ulioko Nyamongo, wilayani Tarime mkoa wa Mara Jumatatu Mei 4, 2015, ili kufahamu jitihada za mgodi kuendeleza miradi ya kijamii na changamoto ambazo Jamii na Mgodi zinapata kutokana na shughuli za uchimbaji  Wanaoshuhudia ni Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Glorious Luoga,(Watatu kulia), Kaimu Meneja Mkuu wa Mgodi huo, Jimmy Ijumba, (Wapili kulia) na Mkuu wa Mahusiano ya Serikali wa kampuni ya Acacia, Alex Lugendo.
 Meneja Uendelezaji wa Mgodi wa dhahabu wa North Mara, Abel Yiga, (kushoto), akimpatia maelezo Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga wakati waziri huyo alipotembelea maeneo yanayozunguka mgodi huo ili kufahamu jitihada za mgodi kuendeleza miradi ya kijamii na changamoto ambazo Jamii na Mgodi zinapata kutokana na shughuli za uchimbaji. Wengine ni Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Glorious Luoga, (Watatu kulia), na kaimu kiongozi wa kitengo cha mahusiano ya kijamii ya mgodi wa North Mara, Zakayo Kalebo. (kushoto)
 Meneja Unedelezaji wa Kampuni ya Acacia, inayomiliki migodi ya Bulyanhulu, Buzwagi na North Mara, Asa Mwaipopo, (katikati), akimpatia maelezo Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga, (kushoto), wakati wa ziara yake ya kutembelea mgodi wa North Mara ili kufahamu jitihada za mgodi kuendeleza miradi ya kijamii na changamoto ambazo Jamii na Mgodi zinapata kutokana na shughuli za uchimbaji. Kulia ni Mkuu wa Mahusiano ya Serikali wa kampuni ya Acacia, Alex Lugendo
 Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga, (kushoto), akisalimiana na Meneja Uendelezaji wa kampuni ya Acacia, Asa Mwaipopo, wakati alipofika kwenye kijiji cha Nyakunguru, kilicho jirani na mgodi wa North Mara, Mara ulioko Nyamongo, wilayani Tarime mkoa wa Mara Jumatatu Mei 4, 2015, ili kufahamu jitihada za mgodi kuendeleza miradi ya kijamii na changamoto ambazo Jamii na Mgodi zinapata kutokana na shughuli za uchimbaji  Wanaoshuhudia ni Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Glorious Luoga,(Watatu kulia), Kaimu Meneja Mkuu wa Mgodi huo, Jimmy Ijumba, (Wapili kulia) na Mkuu wa Mahusiano ya Serikali wa kampuni ya Acacia, Alex Lugendo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 05, 2015

    Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo, hiki ndicho tunachovuna sasa baada ya kupanda kwa muda mrefu ni hali yenye kusikitisha kuona wananchi wameshaamua nawao wale kwa njia ya udanganyifu mala baada ya kujifunza toka kwa wanaowaongoza.....ukiangalia aina hii ya mbegu imeenea sehemu zote nchini watu hawana uzalendo tena kila mtu amekata tamaa na hathamini tena uzalendo.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...