Na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.
Baraza la Michezo la Taifa (BMT) limesogeza mbele siku ya kufanya uchaguzi wa Chama cha Mchezo wa Vinyoya Tanzania (TBA) ambapo unatarajiwa kufanyika Juni 10
mwaka huu katika ukumbi wa Baraza hilo.
mwaka huu katika ukumbi wa Baraza hilo.
Hayo yamesemwa na Afisa habari Baraza la Michezo la Taifa (BMT) Najaha Bakari wakati akizungumza na Mwandishi wetu kwa Njia ya simu.
Pia Najaha amesema kuwa Baraza hilo linaongeza muda wa kuchukua na kurudisha fomu za Uchaguzi wa Viongozi wa Chama cha Mchezo wa Vinyoya Tanzania (TBA) hadi Juni 5 mwaka huu.
Amesema kuwa Fomu zinapatikana ofisi za Baraza la Michezo na kwenye tovuti ya Baraza, gharama ya fomu ni shilingi elfu 10,000/=,Amesema kuwa nafasi ya Mwenyekiti nafasi 1,Makamu Mwenyekiti nafasi 1,Katibu Mkuu nafasi 1,Katibu Mkuu Msaidizi nafasi 1,Mweka Hazina nafasi 1,Mweka Hazina Msaidizi nafasi 1na Wajumbe nafasi tano wakuchaguliwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...