Mwenyekiti wa wasaidizi wa kisheria wilaya ya Monduli Mkoani Arusha, Ibramih Melita akizungumza na wafugaji wa kijiji cha Nanja kwenye mafunzo ya kujengewa uwezo wa kisheria yaliyotolewa na Chama cha wanawake wanasheria nchini (TAWLA) jana.
Askari wa dawati la jinsia na watoto wa Mkoa wa Arusha, Baltazar Kitiku akizungumza na jamii ya wafugaji wa Kijiji Cha Nanja, Kata ya Lepruko Wilayani Monduli Mkoani humo, kuhusiana na kupiga vita unyanyasaji wa kijinsia kwenye mafunzo yaliyotolewa na Chama cha wanawake wanasheria nchini (TAWLA) kwenye maadhimisho yao ya miaka 25.
Jamii ya wafugaji wa Kijiji cha Nanja Kata ya Lepruko Wilayani Monduli Mkoani Arusha, wakiwasikiliza wanasheria wa Chama cha wanawake wanasheria nchini (TAWLA) Tawi la Arusha, ambao wameadhimisha miaka 25 ya kuanzishwa kwa chama hicho kwa kutoa elimu na ushauri wa kisheria jana kwenye vijiji vya Nanja na Meserani (Duka bovu) Wilayani Monduli.
Baadhi ya jamii ya wafugaji wa Kijiji cha Nanja, Kata ya Lepruko Wilayani Monduli Mkoani Arusha, wakiwasikiliza wanasheria wa Chama cha wanawake wanasheria nchini (TAWLA), ambao jana walitoa elimu na ushauri wa kisheria kwenye kijiji hicho.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...