PROGRAMU mpya za utamaduni na ubunifu zinatoa fursa kubwa ya uanzishaji  wa shughuli za kitamaduni zenye kuimarisha sekta ya ubunifu wenye mwelekeo kiuchumi.
Balozi wa Denmark nchini Tanzania,Bw. Johnny Flentoe akizungumza jambo wakati wa uzinduzi wa program mpya ya CKU.
 
Kwa mujibu wa balozi wa Denmark nchini Tanzania,Bw. Johnny Flentoe, amesema kwamba Tanzania inautajiri mkubwa wa kiutamaduni ambao unaweza kutumiwa kuchangia pato la taifa GDP.

 “Bado tasnia ya sanaa na ubunifu ambayo ingeliweza kuchangia katika uchumi na kuwapatia kazi vijana haijatumika ipasavyo. Kutokana na hilo kipaumbele cha programu hii mpya ni kuwezesha vijana kutumia sanaa na ubunifu kukuza ajira,” anasema balozi Johnny Flentoe.
Mshairi Jasper Sabuni akifanya kazi ya 'spoken words' wakati wa uzinduzi wa program mpya ya CKU.

Juni 5, 2015, Ubalozi wa Denmark ukishirikiana na Kituo cha Utamaduni na Maendeleo cha Denmark (CKU) umezindua program mpya ya utamaduni na  maendeleo Tanzania ( Tanzania Culture and Development Programme ).

Programu hiyo imelenga kutengeneza fursa za kiuchumi kupitia jukwaa la sanaa na ubunifu ambapo watanzania watajipambanua kupitia kushiriki shughuli mbalimbali za kitamaduni na kujipatia kipato.
Baadhi ya wadau waliofika kwenye uzinduzi wa program mpya ya CKU Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja
CKU inatekeleza program hiyo kupitia kwa washirika wake likwemo Tamasha la Kimataifa la Filamu (Zanzibar International Film Festival (ZIFF), kupitia mradi wao wa Village Panorama ambao unalenga kuonyesha filamu za kuelimisha maeneo ya vijijini huko Zanzibar.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...