Ndege aina ya Super Bat DA-50
us.
Imetengenezwa Ufaransa na kampuni ya Delair
Tech. Hii ni kubwa kidogo, ina uwezo mkubwa na inatumia viwango vya satelaiti
za kijeshi vya mawasiliano kutumana kupokeataarifa pamoja na namna ya kuongozwa
kwake.
Superbat DA 50 – Imejaribiwa Mkomazi.
Na Daniel Mbega, Mkomazi
Ni majira
ya saa tatu asubuhi Jumatano, Septemba 16, 2015 wakati tunawasili kwenye uwanja
mdogo wa ndege (air strip) katika eneo la Kisima ndani ya Hifadhi ya Taifa ya
Mkomazi inayotenganisha mikoa ya Kilimanjaro na Tanga.
Uwanja unaonekana
mweupe, hakuna ndege! Nikashangaa kwa sababu wenyeji wetu kampuni ya Bathawk
Recon wametuambia tunakuja kushuhudia uzinduzi wa ndege maalum zinazopambana na
ujangili.
Kilichoonekana
mbele yetu ni hema kubwa ambalo mbele yake kulionekana minara midogo
iliyosimikwa kama fimbo. Kwenye banda kubwa ikaonekana ndege ndogo aina ya Twin
otter. Nikadhani ndiyo inayozinduliwa, lakini Idrisa Jaffary, mwenyei wetu
tuliyekuwa naye kwenye gari akasema, hapa siyo hiyo.
Mshangao ukanipata
baada ya gari kusimama wakati nilipokiona kifaa mfano wa ndege kikiwa
kimeegeshwa kwenye bomba maalum kana kwamba ndege inataka kupaa.
Kama nisingekuwa
nazifahamu ndege hizi maarufu kama drones,
ningeweza kusema kwamba huo ni mdoli ambao mwanangu angefurahia kama
ningempelekea akauchezea.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...