Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC),Jaji Mstaafu,Damian Lubuva akizungumza na makundi maalum (hawapo pichani)jinsi watashiriki upigaji wa kura Oktoba 25 iliyofanyika Ukumbi wa New Afrika Hoteli jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Chama Shirikisho la Watu wenye Ulemavu Mkoa wa Pwani Adam Shaban akizungumza juu jinsi ushiriki katika upigaji kura Oktoba 25 katika mkutanao uliotishwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) uliofanyika leo katika Hoteli ya New Afrika jijini Dar es Slaam.
Sehemu ya washiriki wa makundi maalum katika mkutano wa NEC juu ya ushiriki wa watu wenye ulemavu katika upigaji kura oktoba 25 uliofanyika leo Hoteli ya New Afrika jijini Dar es Salaam.
Na Chalila
Kibuda ,Globu ya Jamii
TUME ya
Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema vyama vya siasa vitangaze sera zao kwa wananchi
na sio kuingilia masuala ya utawala wa tume hiyo.
Hayo
ameyasema leo,Mwenyekiti wa tume hiyo,Jaji Mstaafu,Damian Lubuva wakati
alipokutana na makundi maalum jinsi watavyoshiriki uchaguzi mkuu unaotarajiwa
kufanyika Oktoba 25 mwaka huu,amesema tume inafanya kazi kwa mujibu wa sheria
hivyo vyama vya siasa viachie tume ifanya
kazi yake.
Lubuva
amesema kuwa vyama vimekuwa vikishughulika na watu hivyo tume itavichukulia
hatua za kisheria kutokana na
kukiuka kwa maadili ya uchaguzi.
Amesema
mabadiliko ya uteuzi baadhi ya watendaji NEC ni suala kawaida kutokana watu
kujaza nafasi zilizoachwa wazi.
Lubuva
amesema Tume haiko tayari kuingiliwa katika masuala yao ya kiutawala kutokana
na kile kinachofanyika kiko katika sheria.
Amesema
matokeo yatatolewa katika kila vituo na kwa mwaka watatumia siku tatu katika
uchaguzi kwa matokeo yote.
Lubuva
amesema wakati uchaguzi visionekane vikundi vyovyote katika eneo la kituo cha
kupigia kura vikisubiri matokeo.
Shukrani Michuzi na Timu yako kwa kuielimisha jamii
ReplyDelete