Ofisa Biashara wa Manispaa ya Kinondoni, Ananias Kamundu (wa tatu kushoto), akipata maelezo kuhusu bidhaa za kampuni mpya ya simu za mkononi ya Halotel katika hafla ya uzinduzi rasmi wa kampuni hiyo jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Viettel Tanzania wamiliki wa Halotel, Nguyen Thanh Quang na wageni wengine waalikwa.
Ofisa Biashara wa Manispaa ya Kinondoni, Ananias Kamundu (kushoto), na Mkurugenzi wa kampuni mpya ya simu za mkononi wa Halotel Mkoa wa Kinondoni, Alex Thiem (kulia), wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa kampuni hiyo nchini jijini Dar es Salaam leo. Katikati Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Viettel Tanzania wamiliki wa Halotel, Nguyen Thanh Quang .
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Viettel Tanzania wamiliki wa Halotel, Nguyen Thanh Quang akizungumza katika hafla hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...