Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete (pichani) amewataka wananchi wote wenye haki ya kupiga kura kuhakikisha wanaheshimu maagizo ya Tume ya Uchaguzi ya kuwataka waondoke katika vituo vya kupigia kura mara baada ya kumaliza zoezi la upigaji kura.
Rais Kikwete Amesema kuwa wenye jukumu la kukaa kituoni ni Mawakala wa wagombea na sio wapiga kura wote kama inavyodaiwa na baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa.
Rais Kikwete ametoa kauli hiyo leo mjini Dodoma wakati wa kilele cha Mwenge wa Uhuru kilchoenda sanjari na kumbukumbu ya miaka 16 ya kifo cha Baba wa Tiafa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
“Mlinzi wa uhakika wa kura ni wakala kwani ndiye anayekuwepo wakati wote katika chumba cha kupigia na kuhesabia kura…ni jambo la kushangaza kuona baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa wakiwahamasisha wafuasi wako kubaki vituo mita 100…wanalinda nini? wakati kuna Mawakala ndani” alihoji Rais Kikwete.
Amesema kuwa ikiwa wapiga kura wengi watabaki vituoni kwa madai ya kulinda kura upo uwezekano mkubwa wa kutokea fujo ambazo zitasababisha baadhi ya watu kuogopa kupiga kura na hivyo kukosa haki yao ya msingi ya kuwachagua viongozi wanaowataka.
Rais Kikwete amesema kuwa ni vema wananchi wenye sifa za kupiga kura kuondoka kwenye vituo mara baada ya zoezi hilo , vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa yoyote atakaye kaidi agizo la Tume ya Tiafa ya Uchaguzi.
Amesema kuwa watu wenye nia ya kufanya hivyo wasiilazimishe Serikali ifikie uamuzi wa kuchukua hatua kwa kuwa wanaofanya hiyo wana nia ovu na nchi hii.
Amesesisitiza kuwa nia yao ovu haitafanikiwa kwani Serikali imejipanga vizuri ili kuhakikisha kila mwananchi wenye sifa ya kupiga kura anafanya hivyo bila bughuza yoyote.
Aidha , Rais Kikwete amewaonya wananchi wote wanaonunua na kuuza vitambulisho vya kupigia kura kuacha tabia hiyo la sivyo dhidi yao zitachukuliwa.
Amesema kuwa ni vema kila mwananch akatunza vizuri kitambulisho chake ili siku ya kupiga kura aende katika kituo cha kupigia kura ili kutekeza haki yake ya kidemokrasia.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa Ndugu Juma Khatib Chum akimkabidhi Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete mwenge wa uhuru wakati wa sherehe za kilele cha Mbio za Mwenge zilizofanyika katika Uwanja wa Michezi wa Jamhuri mjini Dodoma leo
Mwenge wa Uhuru unaratarajiwa kuzinduliwa mwakani mkoani Morogoro na kilele chake kitakuwa mkoani Simiyu.
Wakati huo huo....
Imetolewa na Premi Kibanga,
Dodoma
Mwenge wa Uhuru unaratarajiwa kuzinduliwa mwakani mkoani Morogoro na kilele chake kitakuwa mkoani Simiyu.
Wakati huo huo....
Katika Kilele cha mbio za mwenge wa uhuru , kumbukumbu ya Baba wa
Taifa , Mwalimu JULIUS Nyerere na wiki ya vijana Kitaifa, Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika hotuba yake
amezungumzia idadi ya watu waliojiandikisha kupiga kura.
Kwa uhakika amesema kuwa idadi ya wapiga kura ni 22,751, 292 kwa upande wa
Bara na 503,193 wa Zanzibar . Hii ndiyo idadi kamili ambayo imo kwenye hotuba ya
Mheshimiwa Rais na hii ndiyo idadi kamili kama ilivyotolewa na Tume ya Uchaguzi
Tanzania .
Asanteni
Mwandishi wa Habari wa Rais, Msaidizi
13 Oct, 2015
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...