Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, John Mngodo, akizungumza na Maafisa wa Jeshi la Polisi, wakati wa mkutano wa Kujitambulisha na kufahamiana na Watendaji wakuu na Maafisa wa Jeshi la Polisi uliofanyika Makao Makuu ya Jeshi hilo, jijini Dar es Salaam leo. Katika hotuba yake, Mngodo alilipongeza jeshi hilo kwa kusimamia Uchaguzi Mkuu kwa amani na utulivu. Kulia kwa Katibu Mkuu ni Inspekta Jenerali wa Jeshi hilo (IGP), Ernest Mangu.
Inspekta Jenerali wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Ernest Mangu (kushoto) akiwaongoza watendaji wakuu na maafisa wa jeshi hilo kuimba wimbo wa maadili wa jeshi hilo wakati wa ziara ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, John Mngodo (wapili kushoto). Ziara hiyo iliyofanyika Makao Makuu ya jeshi hilo jijini Dar es Salaam leo, ilikuwa na lengo la kujitambulisha na kufahamiana na watendaji hao. Watatu kushoto meza kuu ni Naibu IGP, Abdulharam Kaniki, wapili kulia ni Kamishna wa Lojistiki na Fedha wa Jeshi la Polisi Clodwig Mtweve, na kulia ni Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova.
Inspekta Jenerali wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Ernest Mangu (kushoto) akitoa taarifa ya Jeshi hilo wakati wa Ziara ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, John Mngodo, alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi hilo jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujitambulisha na kufahamiana na watendaji wa jeshi hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...