NA  BASHIR  YAKUB -
WAPO mawakala  na  wapo  wanaohitaji  kuwa  mawakala, Kwa  sasa biashara  ya  uwakala  ni  kubwa mno, wapo mawakala   mitandao  ya  simu kama tigo, Airtel, voda n.k, mawakala makampuni  ya  usafirishaji  kama mabasi,  malori n.k , na  makampuni  mengine  mengi. Mtindo  wa  biashara  ya  uwakala  umekua  sana  katika  siku  za  hivi  karibuni. 

Ni  kutokana  na  ongezeko  la  makampuni  na   kukua  kwa  biashara, Upo  umuhimu  mkubwa  wa  kuijua  biashara  ya  uwakala  kwa  undani   hasa  katika  misingi  ya  kisheria .

 Hii  itakusaidia  kuzijua  haki  zako, usipozijua  haki  zako  za  kisheria  katika  biashara  kama  hii   ni  vigumu  kunufaika. Hii  ni  kwasabbu   hutojua  unastahili  nini  na  nini  hustahili.  Ili kuliepuka hili  unajikuta katika  ulazima  wa  kuzijua  taratibu  za  kisheria  zinazohusu  uwakala. Usiingie  katika  biashara  hii  bila  kujua  japo  mambo  kidogo ya  msingi  ya kisheria  yanayohusu  uwakala.

1.WAKALA   NI  NANI.
Sura  ya  345  kifungu  cha 134  cha  sheria ya   mikataba  kinaeleza  nini  maana  ya  wakala.  Kinasema  kuwa  wakala  ni mtu   aliyeajiriwa  kufanya  kazi  au  kitu  chochote  kwa  niaba  ya  mwingine au  kumwakilisha  mtu  mwingine  katika  shughuli  fulani.  Kwahiyo  wakala  ni  mtu  anayesimama  badala  ya  mtu mwingine. 

Huyo  mtu  mwingine  huitwa  mhusika  mkuu, Kwahiyo  wakala  hufanya kazi kwa  niaba  ya  mhusika  mkuu, Humwakilisha  mhusika mkuu.

2.   SIFA  ZA  KUWA  WAKALA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...