NA BASHIR YAKUB -
WAPO mawakala na wapo wanaohitaji kuwa mawakala, Kwa sasa biashara ya uwakala ni kubwa mno, wapo mawakala mitandao ya simu kama tigo, Airtel, voda n.k, mawakala makampuni ya usafirishaji kama mabasi, malori n.k , na makampuni mengine mengi. Mtindo wa biashara ya uwakala umekua sana katika siku za hivi karibuni.
Ni kutokana na ongezeko la makampuni na kukua kwa biashara, Upo umuhimu mkubwa wa kuijua biashara ya uwakala kwa undani hasa katika misingi ya kisheria .
Hii itakusaidia kuzijua haki zako, usipozijua haki zako za kisheria katika biashara kama hii ni vigumu kunufaika. Hii ni kwasabbu hutojua unastahili nini na nini hustahili. Ili kuliepuka hili unajikuta katika ulazima wa kuzijua taratibu za kisheria zinazohusu uwakala. Usiingie katika biashara hii bila kujua japo mambo kidogo ya msingi ya kisheria yanayohusu uwakala.
1.WAKALA NI NANI.
Sura ya 345 kifungu cha 134 cha sheria ya mikataba kinaeleza nini maana ya wakala. Kinasema kuwa wakala ni mtu aliyeajiriwa kufanya kazi au kitu chochote kwa niaba ya mwingine au kumwakilisha mtu mwingine katika shughuli fulani. Kwahiyo wakala ni mtu anayesimama badala ya mtu mwingine.
Huyo mtu mwingine huitwa mhusika mkuu, Kwahiyo wakala hufanya kazi kwa niaba ya mhusika mkuu, Humwakilisha mhusika mkuu.
2. SIFA ZA KUWA WAKALA.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...