WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO
            (TAARIFA KWA UMMA)
Taarifa inatolewa kwa umma kwamba Bodi ya Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali katika kikao chake cha 38 kilichofanyika tarehe 27 Januari, 2016 iliazimia kufuta usajili wa Shirika la African Poor and Patient Organization (APOPA) kutokana na kukiuka masharti ya Sheria ya NGOs Na. 24 ya mwaka 2002 (kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2005). 
Kwa taarifa hii, shughuli za Shirika tajwa zimekoma kuanzia tarehe ya ttangazo la taarifa hii. Wanachama wa shirika wanaagizwa kusitisha shughuli za shirika na kuzingatia taratibu za ufungaji wa shughuli za Shirika kama zinavyoainishwa katika katiba ya Shirika na Kanuni za Sheria ya NGOs, GN.Na.8 ya Mwaka 2015.

M.S.Katemba
MSAJILI WA NGOs

2 Februari, 2016

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...