Wakazi wa Kata ya Kibamba wamepiga kura ya siri kuwabaini wahalifu wanaoishi
katika maeneo yao kufuatia tukio la karibuni la uvamizi katika nyumba nne zilizopo Mtaa wa
Muhongoni ambalo limesababisha kifo cha mkazi mmoja wa eneo hilo, aliyejulikana kwa jina la
Upigaji kura huo ulifanyika katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na ofisi ya mwenyekiti wa
serikali ya mtaa huo ambao ulifanyika viwanja vya Ofisi ya Mtendaji wa Kata na kuhudhuriwa na
Kamanda wa Polisi wa Kata ya Kibamba, Pius Lutumo.
Uamuzi wa kupiga kura hiyo umetokana na kuanza kuibuka kwa vitendo vya ujambazi
unaofanywa majumbani na makundi ya vijana, uporaji wakati wa alfajiri na wizi wa mifugo hali
ambayo imesababisha watu kadhaa kujeruhiwa na wengine kupoteza mali zao.
Katika mkutano huo, wakazi hao walikubaliana na kupiga kura za siri ambazo ziliwataja mara
nyingi watuhumiwa wa uhalifu sugu wanne ambao Diwani wa Kata hiyo, alisema hata yeye majina
yao ameyakuta ofisini kwake hivi karibuni alipoingia madarakani hivi karibuni.
Diwani wa kata hiyo, Ernest Mgawe aliwataka wakazi wa kata hiyo kutoa ushirikiano kwa jeshi la
polisi na ofisi yake hasa pale yanapotokea matukio ya uhalifu nna kukamatwa kwa watuhumiwa ili
lengo la kuifanya Kibamba kuwa sehemu salama ya kuishi liweze kufikiwa.
”Tunaomba ushirikiano wenu kwani kuna wakati watu walivamiwa na kujeruhiwa na mmoja kati ya
watuhumiwa sugu ambaye pia leo ametajwa lakini hata hivyo wahanga walipotakiwa kwenda olisi
kutoa maelezo ili mlenga afikishwe maakamanbi hawakuonekana” alisema.
Awali Kamanda wa polisi wilaya ya kipolisi ya ibamba aliwataka wananchi watambue kuwa suala
la ulinzi na usalama ipo miononi mwao kutokana na hali halisi ilivyo hvi sasa na kuwataka
waachane na nadhjaria kuwa polisi ndi walinzi wao na mali zao.
“Hilo mnapaswa kjulitambua na kulingana na sheria ndogo zilizotungwa katika manuspaa ya
ionondoni suala la ulinzi shrikishi sio iyari hasa pa,e wananchi wanapokubaliana upitia mikutano
yao halali kma huo” alisema.
Alibainisha kuwa kura za siri zilizopigwa zitafanyiwakazi na kila mkazi ni lazima ashiriki ulinzi huo
iwe kwa yeye mwenyewe kutoka na kulinda au kuchangia fedha kidogo kwa ajili ya uwezeshaji
wa mpango huo na wale ambao watakaidi watafikishwa mahakamani kwani sheria ipo wazi.
Pia Diwani M,gawe amewapa siku 30 watu wanaomiliki maeneo katka kata hiyo ambayo
hawajayaendeleza hivyo kuwa mapori ambayo sasa yanatumiwa kama maficho ya wahalifu na
baada ya muda hup atawasilisha majina kwa mkuu wa mkoa kwa aili ya hatua zaidi.
Alisema kuna maeneo mengi eneo hilo ambayo wamiliki wake hawayaendelezi na yamegeuka
mapori na ingawa wengine wana hati za kuyamiliki lakini wataomba msaada ofisi ya mkoa kwa
hatua zaidi ili kuwanusuru wananchi na madhila ambayo wanayapata hivi sasa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...