Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) kimeshiriki maonesho ya Nane nane yanayofanyika kitaifa viwanja vya Ngongo, Mkoa wa Lindi. 
Maonesho hayo yalifunguliwa rasmi na Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Sospeter Muhongo yakiwa na kauli mbiu “Kilimo, mifugo na uvuvi ni nguzo ya maendeleo. Kijana shiriki kikamilifu. Kupitia maonesha ya Nane Nane mwaka huu AICC pamoja na tawi lake la Dar es Salaam, Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere (JNICC) inapata fursa ya kukutana na wadau wake na wananchi kwa ujumla kuwaelezea juu ya huduma zitolewazo na Shirika hilo. Huduma hizo ni pamoja na utalii wa mikutano, upangishaji wa nyumba za makazi na nafasi za ofisi kwa upande wa Arusha.
Afisa Masoko na Utafiti Mkuu wa AICC Bi.Linda Nyanda akitoa maelezo kuhusiana na huduma zitolewazo na AICC na JNICC kwa Mkuu wa Magereza wa Mkoa wa Lindi SACP Tusekile Mwaisabila (kulia).
Mkurugenzi wa Manispaa ya Lindi Bw.Jomaary M. Saturi akisikiliza kwa makini maelezo toka kwa Mkuu wa Masoko na Utafiti wa AICC Bi.Linda Nyanda, alipotembelea banda la AICC kwenye maonesho ya Nane nane yanayoendelea Mkoani Lindi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...