Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) linashiriki kwenye maonesho ya nanenane ambayo yanafanyika kitaifa katika viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi.

Katika maonesho hayo NSSF inatoa huduma mbalimali zikiwemo kutoa taarifa za michango za wanachama, kuandikisha wanachama wapya na kutoa kadi mpya kwa wanachama wa zamani, kutoa maelezo juu ya uuzaji wa nyumba za mtoni kijichi phase 3 na Viwanja vya Kiluvya na pia kutoa elimu ya mafao na huduma mbalimbali zitolewazo na NSSF.

NSSF inapenda kuwakaribisha wananchi wa Lindi na Mtwara kutembelea banda lao lililopo kwenye viwanja hivyo vya Ngongo.
Afisa wa NSSF mkoa wa Lindi, Saad Juma akitoa maelezo kwa wananchi wa Mkoa wa Lindi waliotembelea banda la NSSF kwenye maonesho ya Nanenane mkoani humo.
Afisa Matekelezo wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), mkoa wa Lindi, Adam Mbena akimwandikisha kujiunga na NSSF mmoja wa wakazi wa Lindi aliyetembelea kwenye maonesho ya Nanenane.
Afisa Mifumo ya Kompyuta Rukia Penza akimuelezea mwanachama taarifa yake ya Michango alipotembelea banda la NSSF kwenye maonesho ya nanenane Lindi.
Afisa Masoko Muandamizi Amina Mmbaga akiwapa maelezo wakazi wa Lindi waliotembelea banda la NSSF kwenye maonesho ya nanenane anayoendelea mkoani Lindi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...