Kaimu katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano anayesimamia sekta
Mawasiliano mhandisi Dkt. Maria Sasabo kushoto akizungumza wakati wa hafla ya
kutoa zawadi kwa wanafunzi wa vyuo, sekondari na shule za msingi za jijini Dar
es Salaam walioshinda shindano la uandishi wa insha kuhusu haki ya mtumiaji wa
huduma za mawasiliano, kulia ni Katibu wa Baraza la ushauri la watumiaji wa
huduma za mawasiliano Bi. Mary Shao
Msuya.
Mwenyekiti wa baraza la ushauri la watumiaji wa huduma za
mawasiliano Bw. Stanley Mwabulambo akimkaribisha mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano (Mawasiliano) Mhandisi
Dkt. Maria Sasabo kuzungumza na wanafunzi wa vyuo, sekondari na shule za msingi
za jijini Dar es Salaam walioshinda shindano la uandishi wa insha kuhusu haki
ya mtumiaji wa huduma za mawasiliano
Mshindi wa kwanza wa insha kwa upande wa Shule za
Msingi Jane Michael Andrew kutoka shule ya msingi ya Mbuyuni akipokea
zawadi ya cheti ya mshindi wa kwanza wa insha kutoka kwa Kaimu katibu Mkuu wa
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
(Mawasiliano) mhandisi Dkt. Maria Sasabo.
Mshindi wa kwanza wa insha kwa upande wa vyuo vya elimu ya
juu Bw. Omari Abbas kutoka chuo Kikuu kishiriki cha Ualimu (DUCE) akipokea
zawadi ya cheti kutoka kwa Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano (Mawasiliano) mhandisi Dkt. Maria
Sasabo.
Mshindi wa kwanza wa insha kwa upande wa Shule za sekondari
Bw, Ramadhani Mohamed kutoka Shule ya sekondari ya Kibasila akipokea zawadi ya mshindi wa kwanza wa insha kutoka
kwa Kaimu katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Mawasiliano) mhandisi Dkt. Maria Sasabo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...