BENKI ya Barclays Tanzania wazindua mkopo wa Nyumba kwa wananchi mkopo ambao utaanzia shilingi Milioni 30 hadi Mkopo wa Milioni 500 ambao utakuwa na riba ya asilimia 19.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa za rejareja wa Benki ya Barclays, Oscar Mwafwagasi wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo. Amesema Mkopo huo ni kwa waajiliwa wa kudumu.

Amesema kuwa Mkopo utakopeshwa kwa wazawa wa Tanzania(Raia wa Tanzania) tuu pia unaatakiwa kulipa kuanzia  mwaka wa kwanza wa mkopo hadi miaka 20.
 Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa za rejareja wa Benki ya Barclays, Oscar Mwafwagasi akizungumza wakati wa kuzindua Mikopo ya Nyumba kwa  wananchi hapa nchini ambao utaanzia shilingi Milioni 500 ambao utakuwa na riba ya asilimia 19. Kulia ni Meneja wa Masoko wa benki ya Barclays, Joe Bendera.
Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa za rejareja wa Benki ya Barclays, Oscar Mwafwagasi, Meneja wa Masoko wa benki ya Barclays, Joe Bendera na Mkurugenzi wa biashara na wateja wa rejareja wa benki ya Barclays, Kumar Pather wakisikiliza kwa makini swali kutoka kwa mwandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...