Benki ya CRDB  imekanusha vikali habari iliyoandikwa leo Agosti 18, 2016 na  gazeti moja la kiswahili la kila siku na kunukuliwa na baadhi ya mitandao ya kijamii na  kumnukuu kimakosa Mkurugenzi Mtendaji Dkt. Charles Kimei (pichani) kuwa Benki hiyo  “Sasa imesimamisha mikopo kutokana na "hali tete ya uchumi wa nchi ".

Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB Bi. Tully Esther Mwambapa, amekanusha  vikali habari hiyo ambayo ameitaja kuwa  inalenga kuwatia hofu wateja wao  wapendwa na kuichonganisha Benki ya CRDB na dola.

“Nachukua fursa hii kuwatangazia wateja wetu na watanzania wote kwa ujumla kuwa waipuuze taarifa hii na kuwajulisha kuwa Benki inatoa mikopo kama kawaida na tunawakaribisha kuja kukopa ili kwa pamoja tujenge uchumi wa taifa letu”, amesema Bi. Mwambapa katika taarifa yake kwa vyombo vya habari leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...