Benki ya CRDB imekanusha vikali habari iliyoandikwa leo
Agosti 18, 2016 na gazeti moja la
kiswahili la kila siku na kunukuliwa na baadhi ya mitandao ya kijamii na kumnukuu kimakosa Mkurugenzi Mtendaji Dkt. Charles Kimei (pichani) kuwa Benki hiyo “Sasa imesimamisha mikopo kutokana na
"hali tete ya uchumi wa nchi ".
Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja
wa Benki ya CRDB Bi. Tully Esther Mwambapa, amekanusha vikali habari hiyo ambayo ameitaja kuwa inalenga
kuwatia hofu wateja wao wapendwa na
kuichonganisha Benki ya CRDB na dola.
“Nachukua fursa hii kuwatangazia wateja wetu na
watanzania wote kwa ujumla kuwa waipuuze taarifa hii na kuwajulisha kuwa Benki
inatoa mikopo kama kawaida na tunawakaribisha kuja kukopa ili kwa pamoja
tujenge uchumi wa taifa letu”, amesema Bi. Mwambapa katika taarifa
yake kwa vyombo vya habari leo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...