Na Zephania Mandia, Mwanza

Wananchi wanaoishi katika Kata ya Nyasaka a,b,na c, Wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza, wanakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa kivukio yaani daraja katika Mto Nyakurunduma ambao unatiririsha maji katika Ziwa Victoria jijini Mwanza.

Wananchi hao Wamesema tatizo hilo limekua kero kubwa ya miaka mingi kwani mvua zikinyesha mto huo hufurika kiasi cha kusababisha wananchi kushindwa kuvuka mto huo mara kwa mara na wakati mwingine kwa Wanafunzi kupitwa na masomo, imeelezwa kuwa hivi karibuni wanafunzi watatu na madereva wawili wa pikipiki walisombwa na maji wakati wakivuka katika mto huo na kupoteza maisha.

aidha wananchi hao wamesema walipofikisha taarifa kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, aliwahakikishia tatizo hilo lingefanyiwa kazi baada ya mvua kupungua lakini hadi sasa hakuna kilichofanyika badala yake wananchi hao wamelazimika kujenga daraja la miti ili wapate sehemu ya kuvukia kwani muda wowote mvua zinaweza kuanza tena. 
 Muonekano wa Daraja hilo lililojengwa na Mwananchi wa Kata ya Nyasaka a,b,na c, Wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza.
 Watoto wakivuka.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hapa daraja la uhakika linatakiwa liwe la chuma, mbao au sementi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...