DALADALA lenye
namba za usajili T274 DEX, lililokuwa likifanya safiri zake kati ya Mbagala RangiTatu kuelekea Temeke
jijini Dar es Salaam, limepiga mweleka mita chache tu kutoka kituo cha Daladala
Sabasaba-Mbagala mapema leo asubuhi (Agosti 11, 2016) na kujeruhi watu kadhaa.
Mashuhuda
wanasema, Daladala hilo lililokuwa katika mwendo kasi, liliserereka na kuacha
njia wakati likikaribia kusimama kituoni hapo.
Dereva
wa Daladala hilo aliruka na kukimbia, nakuwaacha abiria wakitaharuki kila mmoja
akijaribu kukoa maisha yake.
“Unajua
mvua hizi zilizonyesha asubuhi zinafanya barabara iteleze na hawa jamaa mwendo
wao unajua tena, sasa alijaribu kufunga breki gari likaanza kuserereka na
alipojaribu kurudi barabarani likakataa na kutumbukia mtaroni,” anasimulia
mmoja wa mashuhuda aliyekuwa eneo la ajali.
Polisi
wa usalama barabarani alifika muda mfupi baada ya ajali hiyona taratibu ya
kuliondoa gari hilo zilianza.
Abiria
wote walitoka salama, wachache walijeruhiwa na baadhi yao walionekana wakilia
kutokana na mshtuko wa ajali hiyo ya asubuhi.
Mtu
huyu ambaye haikujulikana maramoja kama ni muhudumu wa daladala hilo au
abiria akitoka ndani ya daladala hilo baada ya "kupiga mwereka'
Mashuhuda kama kawaida yao
HABARI/PICHA
NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID
Mmoja wa abiria aliyenusurika akilia kwa huzuni kutokana na ajali hiyo
Wapita njia wakimuuliza abiria huyu (aliyekaa), ambaye alikuwa ndani ya daladala hilo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...