DALADALA lenye namba za usajili T274 DEX, lililokuwa likifanya safiri zake kati ya Mbagala RangiTatu kuelekea Temeke jijini Dar es Salaam, limepiga mweleka mita chache tu kutoka kituo cha Daladala Sabasaba-Mbagala mapema leo asubuhi (Agosti 11, 2016) na kujeruhi watu kadhaa.

Mashuhuda wanasema, Daladala hilo lililokuwa katika mwendo kasi, liliserereka na kuacha njia wakati likikaribia kusimama kituoni hapo.
Dereva wa Daladala hilo aliruka na kukimbia, nakuwaacha abiria wakitaharuki kila mmoja akijaribu kukoa maisha yake.

“Unajua mvua hizi zilizonyesha asubuhi zinafanya barabara iteleze na hawa jamaa mwendo wao unajua tena, sasa alijaribu kufunga breki gari likaanza kuserereka na alipojaribu kurudi barabarani likakataa na kutumbukia mtaroni,” anasimulia mmoja wa mashuhuda aliyekuwa eneo la ajali.
Polisi wa usalama barabarani alifika muda mfupi baada ya ajali hiyona taratibu ya kuliondoa gari hilo zilianza.

Abiria wote walitoka salama, wachache walijeruhiwa na baadhi yao walionekana wakilia kutokana na mshtuko wa ajali hiyo ya asubuhi.
 Mtu huyu ambaye haikujulikana maramoja kama ni muhudumu wa daladala hilo au abiria akitoka ndani ya daladala hilo baada ya "kupiga mwereka'
 Mashuhuda kama kawaida yao
HABARI/PICHA NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID
  Mmoja wa abiria aliyenusurika akilia kwa huzuni kutokana na ajali hiyo
 Wapita njia wakimuuliza abiria huyu (aliyekaa), ambaye alikuwa ndani ya daladala hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...