Mkuu wa Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, Nyabaganga Taraba akizungumza na makundi ya wafugaji wa wilayani humo (hawapo pichani) katika kikao cha kujadili maendeleo ya sekta hiyo na kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili. 

 Tukio hilo limefanyika leo katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu ambapo mkuu huyo wa wilaya aliwataka kushiriki katika shughuli za maendeleo ya wilaya. 

 Taraba alisema kuwa wafugaji wana mchango mkubwa katika maendeleo ya wilaya, mkoa na taifa kwa ujumla hivyo wamuunge mkono ili kuwaletea wananchi maendeleo. 

 Aliwaomba kuchangia shughuli za maendeleo hususan katika utengenezaji wa madawati ili yasambazwe katika shule zilizopo wilayani humo ili watoto wasikae chini. Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa Kishapu ina mnada ambao ni wa pili kwa ukubwa nchini kote hivyo wafugaji wautumie kuleta maendeleo ya wilaya na taifa. 

 Hata hivyo, aliwakumbusha kutumia wataalamu katika kuboresha ufugaji wao uwe wa kisasa zaidi yaani kufuga na siyo kuishi na mifugo kama inavyokuwa siku zote.
Wafugaji wakimsikiliza kwa makini Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Nyabaganga Taraba alipokuwa akizungumza nao katika kikao cha kujadili maendeleo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...