Muwakilishi wa Balozi wa China nchini Tanzania,Gou Haodong akimkabidhi moja ya dawati kati ya 100 yaliyotolewa na Wafanyabiashara wa Karikoo wenye asili ya China ,kwa Mkuu wa Wa Wilaya ya Ilala,Mh Sophia Mjema mapema leo jijini Dar.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala,Mh Sophia Mjema akizungumza kwenye hafla fupi ya kukabidhiwa madawati 200 kutoka kwa Wafanyabiashara wa Kariakoo wenye asili ya China leo jijini Dar,kwa ajili ya shule ya msingi Maghorofani iliyopo Gongolamboto,jijini Dar Es Salaam.Wafanyabiashara hao waliahidi kumkabidhi Mh.DC Mjema Madawati 200 lakini leo wamekabidhi nusu ya madawati hayo (100),huku mengine yakiendelea kutengenezwa.Shule hiyo ya Maghorofani ilikuwa na uhitaji wa madawati 525,yakapatikana madawati 250 na kupungukiwa madawati 275.
Muwakilishi wa Balozi wa China nchini Tanzania,Gou Haodong akizungumza kwa ufupi mbele ya Waalimu,wageni waalikwa mbalimbali (hawapo pichani),kabla ya kukabidhi madawati 100 yaliyotolewa na Wafanyabiashara wa Kariako wenye asili ya China jijini Dar,pichani kulia ni Mkuu wa Wa Wilaya ya Ilala,Mh Sophia Mjema. 
Baadhi ya Wanafunzi wa shule hiyo ya Maghorofani wakiwa wamekalia baadhi ya madawati yaliyotolewa na Wafanyabiashara wa Kariakoo wenye asili ya China jijini Dar. 
Wakiwa katika picha ya pamoja .PICHA NA MICHUZI JR.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Mchango mzuri wa kundeleza jiyihada za kuboresha mazingira ya kusomea nchini.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...