IKIWA ni sehemu ya mkakati wa kupambana na ujangili pamoja na kutangaza utalii wa ndani kampuni za Uhifadhi za Friedkin Conservation Fund (FCF) na African Wildlife Trust (AWT) zimeamua kudhamini Rock City Marathon inayotarajiwa kufanyika Septemba 25 kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana kuhusiana na udhamini huo wa miaka mitatu, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hizo Bw Pratik Patel alisema kampuni mzake zitatumia mbio hizo kuzindua kampeni yao inayofahamika “*Okoa Wanyama Wetu*; *Kataa Ujangili”*

“Tutatumia Rock City Marathon kutangaza kampeni yetu ya kupinga ujangili
itakayofanyika katika baadhi ya majiji ulimwenguni.,’’ alibainisha Pratik. Alisema kampeni hiyo ya “*Okoa Wanyama Wetu*; *Kataa Ujangili”* itaanza nanmatembezi yatakayofanyika Septemba 24 mwaka huu jijini Arusha, Moshi na Dar es Salaam yakifuatiwa na mbio hizo Septemba 25, Uwanja wa CCM Kirumba.

“Tuliamua kudhamini Rock City Maratahon kwa kuwa lengo la mbio hizi ni
kutangaza utalii wa ndani na sisi tuliona kwamba huo utalii unaotangazwa
ili uwe na tija zaidi unategemea uwepo wa maliasili. Na ni wazi kwamba
uwepo wa maliasili hizi unategemea sana jitihada za kweli katika uhifadhi
wake! Na hapo ndipo hasa utatukuta sisi ,’’ alisema.

Wakizungumza kwenye uzinduzi wa mbio hizo jijini Mwanza hivi karibuni, Mkuu wa mkoa huo John Mongella na Mkuu wa mkoa wa Simiyu ambae pia ni Rais wa chama cha riadha Tanzania (RT) Anthony Mtaka walipongeza wadhamini wa mbio hizo zikiwemo kampuni za Friedkin Conservation Fund (FCF) na African Wildlife Trust (AWT) kwa kuunga mkono jitahada za serikali  katika kutangaza utalii wa ndani pamoja na kupambana na ujangili hapa nchini.

Pamoja na pongezi hizo pia viongozi hao wa walikuwa wa kwanza kujisajili
kushiriki Rock City Marathon huku wakiahidi kuhakikisha kwamba mbio
zinapata washiriki wa kutosha sambamba na wadhamini kutoka mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Mbali na kampuni za Freidkin Conservation Fund na African Wildlife
Trust,wadhamini wengine wa mbio hizo ni pamoja na  Mwanza Hotel, Nyanza Bottlers Limited, Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Real PR
Solutions na kampuni ya Fabec.

Akizungumzia mbio hizo Mratibu kutoka kampuni ya Capital Plus Bw Mathew Kasonta alisema Rock City Marathon zitahusisha makundi matano yaani mbio za kilomita 21 kwa wanaume na wanawake, kilomita 5 kwa ngazi ya ‘corporate’, kilomita 3 kwa ajili ya walemavu na zile za wazee umri zaidi miaka 55 na kuendelea pamoja na kilomita 2 kwa ajili ya watoto umri kati ya miaka 7 hadi 19.

Pia litoa wito kwa wakazi wa jiji la Mwanza na mikoa jirani kujisajili kwa
kuchukua fomu katika vituo kadhaa vikiwemo Ofisi za michezo wilaya zote za
mkoa wa Mwanza, Ofisi zote za riadha mikoa ya Geita, Simiyu na
Shinyanga,   Uwanja wa Nyamagana,  Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino  Mwanza, Kituo cha michezo Malya na Shule ya Kimataifa ya Isamilo,

“Kwa upande wa Dar es Salaam Fomu za ushiriki pia zinapatikana katika ofisi za Kampuni ya Capital Plus International zilizopo ghorofa ya tatu jengo la ATC, jijini Dar es, Salaam na vituo vingine vitaendelea kutangazwa hivi
karibuni,” alihitimisha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...