Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi Mhe.George Simbachawene akikata utepe kuzindua rasmi gati ya kisasa katika kisiwa cha Songosongo jana. Wa pili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe.Godfrey Zambi na nyuma ya Mkuu wa mkoa ni Mhandisi Gilbert Mwoga, Mkurugenzi Msaidizi kutoka Ofisi ya Rais Tamisemi.
Na Mathew Kwembe, Lindi
Serikali imesema kuwa halmashauri zinazodaiwa na bodi ya Mikopo ya Serikali za Mitaa na
ambazo zimeshindwa kurejesha malimbikizo ya madeni inayodaiwa na Bodi ya Mikopo ya
Serikali za Mitaa hazitaruhusiwa kukopa katika taasisi nyingine za kifedha hadi zikamilishe
kwanza deni llinalodaiwa na Bodi hiyo.
Agizo hilo limetolewa jana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za
Mitaa, Mhe.George Simbachawene wakati alipotembelea maonyesho ya wakulima ya nane nane
yanayofanyika kitaifa mkoani Lindi.
Waziri Simbachawene alisema kuwa halmashauri zote zinazodaiwa na Bodi ya Mikopo ya
Serikali za Mitaa hataziruhusu kuomba mkopo wa fedha kutoka taasisi nyingine zozote hadi
kwanza zikamilishe deni walilokopa kutoka katika Bodi hiyo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi Mhe.George Simbachawene akiangalia bustani ya mbogamboga inayomilikiwa na Shirika la SUMA JKT.
Waziri Simbachawene alisema kuwa ameamua kufanya hivyo ili kuhakikisha kuwa fedha zote
zilizokopwa na halmashauri kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo
zinarejeshwa ili mfuko huo uwe endelevu na kuzipa fursa halmashauri nyingine kukopa fedha
kutoka kwenye Bodi hiyo.
Aidha Waziri Simbachawene ameitaka Bodi ya Mikopo ya Serikali za Mitaa kuandaa utaratibu
maalum utakaoziwezesha halmashauri zinazokopa fedha kupitia taasisi hiyo zinarejesha fedha
zake moja kwa moja benki bila ya kukumbushwa mara kwa mara.
Hatua hiyo ya Waziri Simbachawene inafuatia maelezo ya Mhasibu wa Bodi hiyo Bwana
Mourice Kobalogira kumweleza Waziri kuwa Halmashauri nyingi zilizokopa fedha kupitia Bodi
hiyo zimekuwa zikikwepa kurejesha fedha kwa visingizio mbalimbali hali inayosababisha
chombo hicho kushindwa kuzikopesha halmashauri nyingine.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi Mhe.George Simbachawene akifurahia baada ya kushuhudia bustani ya mboga mboga aina ya bilinganya ambayo imestawi vyema katika eneo la maonyesho ya Nanenane mkoani Lindi. Bustani hiyo inamilikiwa na Jeshi la Kujenga Taifa kupitia shirika lake la SUMA JKT.
Bwana Kobalogira alimweleza Waziri Simbachawene kuwa hali ya urejeshaji mikopo imekuwa
ya kusua sua mno ambapo hadi kufikia sasa maombi mapya ya halmashauri zinazotaka kukopa
kupitia bodi hiyo yamefikia bilioni 49 lakini Bodi imeweza kutoa mikopo yenye thamani ya
shilingi bilioni tisa tu.
“Tatizo Mhe.Waziri ni kuwa halmashauri hazizingatii urejeshaji kulingana na mikataba yao
waliyoombea mikopo, mfano mtu kama aliomba mkopo kwa ajili ya ujenzi wa kituo kikuu cha
Mabasi, basi fedha za urejeshaji zitoke katika mapato ya stendi, au kama halmashauri iliomba
mkopo kwa ajili ya ujenzi wa soko, fedha za urejeshaji zitokane na mradi huo, lakini
halmashauri nyingi zimekuwa hazifanyi hivyo,” alisema bwana Kobalogira.
Kufuatia hali hiyo, Waziri Simbachawene aliiagiza Bodi hiyo kuhakikisha kuwa inaweka
kipengele katika mkataba wa mkopo utakaozibana halmashauri hizo kurejesha fedha ilizoombea
mkopo kulingana na masharti yaliyowekwa na bodi hiyo, tofauti na ilivyo sasa ambavyo
halmashauri nyingi zilizopewa mkopo zimekuwa zikikwepa kutekeleza suala la marejesho.
Mhasibu kutoka Bodi ya Mikopo ya Serikali za Mitaa Bwana Mourice Kobalogira akimweleza waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi Mhe.George Simbachawene wakati alipotembelea banda la Ofisi katika Maonyesho ya Nane nane yanayofanyika kitaifa mkoani Lindi.
TUNATOA MIKOPO YA HARAKA YA € 15000 Hadi $ 72000 KIASI CHOCHOTE CHA UCHAGUZI WAKO NA 2-4
ReplyDeleteSAA YA HUDUMA YA MAFANIKIO YA KUFANIKIWA NA 2% VIWANGO VYA RIBA KWA BIASHARA
NA BINAFSI
MADHUMUNI SASA TUMIA NA UJUMBE WA BARUA KWA:
philipmorganloanservice00@gmail.com
JAZA NA URUDI
Jina:
Kiasi cha Mkopo:
Muda:
Jinsia:
Nchi:
Lengo:
Namba ya simu ya mkononi:
JIBU LAKO NI LAZIMA MARA MOJA
TUNATOA MIKOPO YA HARAKA YA € 15000 Hadi $ 72000 KIASI CHOCHOTE CHA UCHAGUZI WAKO NA 2-4
ReplyDeleteSAA YA HUDUMA YA MAFANIKIO YA KUFANIKIWA NA 2% VIWANGO VYA RIBA KWA BIASHARA
NA BINAFSI
MADHUMUNI SASA TUMIA NA UJUMBE WA BARUA KWA:
philipmorganloanservice00@gmail.com
JAZA NA URUDI
Jina:
Kiasi cha Mkopo:
Muda:
Jinsia:
Nchi:
Lengo:
Namba ya simu ya mkononi:
JIBU LAKO NI LAZIMA MARA MOJA