Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi Mhe.George Simbachawene akikata utepe kuzindua rasmi gati ya kisasa katika kisiwa cha Songosongo jana. Wa pili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe.Godfrey Zambi na nyuma ya Mkuu wa mkoa ni Mhandisi Gilbert Mwoga, Mkurugenzi Msaidizi kutoka Ofisi ya Rais Tamisemi.

Na Mathew Kwembe, Lindi

Serikali imesema kuwa halmashauri zinazodaiwa na bodi ya Mikopo ya Serikali za Mitaa na ambazo zimeshindwa kurejesha malimbikizo ya madeni inayodaiwa na Bodi ya Mikopo ya Serikali za Mitaa hazitaruhusiwa kukopa katika taasisi nyingine za kifedha hadi zikamilishe kwanza deni llinalodaiwa na Bodi hiyo.

Agizo hilo limetolewa jana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe.George Simbachawene wakati alipotembelea maonyesho ya wakulima ya nane nane yanayofanyika kitaifa mkoani Lindi.

Waziri Simbachawene alisema kuwa halmashauri zote zinazodaiwa na Bodi ya Mikopo ya Serikali za Mitaa hataziruhusu kuomba mkopo wa fedha kutoka taasisi nyingine zozote hadi kwanza zikamilishe deni walilokopa kutoka katika Bodi hiyo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi Mhe.George Simbachawene akiangalia bustani ya mbogamboga inayomilikiwa na Shirika la SUMA JKT.

Waziri Simbachawene alisema kuwa ameamua kufanya hivyo ili kuhakikisha kuwa fedha zote zilizokopwa na halmashauri kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo zinarejeshwa ili mfuko huo uwe endelevu na kuzipa fursa halmashauri nyingine kukopa fedha kutoka kwenye Bodi hiyo.

Aidha Waziri Simbachawene ameitaka Bodi ya Mikopo ya Serikali za Mitaa kuandaa utaratibu maalum utakaoziwezesha halmashauri zinazokopa fedha kupitia taasisi hiyo zinarejesha fedha zake moja kwa moja benki bila ya kukumbushwa mara kwa mara.

Hatua hiyo ya Waziri Simbachawene inafuatia maelezo ya Mhasibu wa Bodi hiyo Bwana Mourice Kobalogira kumweleza Waziri kuwa Halmashauri nyingi zilizokopa fedha kupitia Bodi hiyo zimekuwa zikikwepa kurejesha fedha kwa visingizio mbalimbali hali inayosababisha chombo hicho kushindwa kuzikopesha halmashauri nyingine.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi Mhe.George Simbachawene akifurahia baada ya kushuhudia bustani ya mboga mboga aina ya bilinganya ambayo imestawi vyema katika eneo la maonyesho ya Nanenane mkoani Lindi. Bustani hiyo inamilikiwa na Jeshi la Kujenga Taifa kupitia shirika lake la SUMA JKT.

Bwana Kobalogira alimweleza Waziri Simbachawene kuwa hali ya urejeshaji mikopo imekuwa ya kusua sua mno ambapo hadi kufikia sasa maombi mapya ya halmashauri zinazotaka kukopa kupitia bodi hiyo yamefikia bilioni 49 lakini Bodi imeweza kutoa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni tisa tu.

“Tatizo Mhe.Waziri ni kuwa halmashauri hazizingatii urejeshaji kulingana na mikataba yao waliyoombea mikopo, mfano mtu kama aliomba mkopo kwa ajili ya ujenzi wa kituo kikuu cha Mabasi, basi fedha za urejeshaji zitoke katika mapato ya stendi, au kama halmashauri iliomba mkopo kwa ajili ya ujenzi wa soko, fedha za urejeshaji zitokane na mradi huo, lakini halmashauri nyingi zimekuwa hazifanyi hivyo,” alisema bwana Kobalogira.

Kufuatia hali hiyo, Waziri Simbachawene aliiagiza Bodi hiyo kuhakikisha kuwa inaweka kipengele katika mkataba wa mkopo utakaozibana halmashauri hizo kurejesha fedha ilizoombea mkopo kulingana na masharti yaliyowekwa na bodi hiyo, tofauti na ilivyo sasa ambavyo halmashauri nyingi zilizopewa mkopo zimekuwa zikikwepa kutekeleza suala la marejesho.
Mhasibu kutoka Bodi ya Mikopo ya Serikali za Mitaa Bwana Mourice Kobalogira akimweleza waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi Mhe.George Simbachawene wakati alipotembelea banda la Ofisi katika Maonyesho ya Nane nane yanayofanyika kitaifa mkoani Lindi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. TUNATOA MIKOPO YA HARAKA YA € 15000 Hadi $ 72000 KIASI CHOCHOTE CHA UCHAGUZI WAKO NA 2-4
    SAA YA HUDUMA YA MAFANIKIO YA KUFANIKIWA NA 2% VIWANGO VYA RIBA KWA BIASHARA
    NA BINAFSI
    MADHUMUNI SASA TUMIA NA UJUMBE WA BARUA KWA:
    philipmorganloanservice00@gmail.com

    JAZA NA URUDI

    Jina:
    Kiasi cha Mkopo:
    Muda:
    Jinsia:
    Nchi:
    Lengo:
    Namba ya simu ya mkononi:

    JIBU LAKO NI LAZIMA MARA MOJA

    ReplyDelete
  2. TUNATOA MIKOPO YA HARAKA YA € 15000 Hadi $ 72000 KIASI CHOCHOTE CHA UCHAGUZI WAKO NA 2-4
    SAA YA HUDUMA YA MAFANIKIO YA KUFANIKIWA NA 2% VIWANGO VYA RIBA KWA BIASHARA
    NA BINAFSI
    MADHUMUNI SASA TUMIA NA UJUMBE WA BARUA KWA:
    philipmorganloanservice00@gmail.com

    JAZA NA URUDI

    Jina:
    Kiasi cha Mkopo:
    Muda:
    Jinsia:
    Nchi:
    Lengo:
    Namba ya simu ya mkononi:

    JIBU LAKO NI LAZIMA MARA MOJA

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...