Sehemu ya Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani |
NA MWANDISHI MAALUM
SHIRIKA
la Umeme Tanzania (TANESCO) linaendelea kuwatangazia wateja wake wote wa Wilaya
ya Bagamoyo kuwa, kutokana na kukatika kwa waya wa mawasiliano, (Optic Fiber)
kati ya Dar es Salaam na Bagamoyo, Ofisi ya Shirika hilo wilayani Bagamoyo bado
inashindwa kutoa huduma za kupokea malipo na kuuza LUKU kwa muda mpaka hapo
waya huo utakapoungwa.
Kwa mujibu wa taarifa ya Ofisi ya Uhusiano MakaoMakuu yaTANESCO, Kwa sasa Shirika linawaomba wateja wake wanaotaka kununua umeme au kulipia huduma zingine za umeme kutumia njia mbadala ya mitandao ya Simu na makampuni mengine yenye mikataba na TANESCO.
Jitihada zinaendelea ili kuhakikisha mkongo huo wa mawasiliano unaungwa mapema iwezekanavyo.
Uongozi unaomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza.
Kwa mujibu wa taarifa ya Ofisi ya Uhusiano MakaoMakuu yaTANESCO, Kwa sasa Shirika linawaomba wateja wake wanaotaka kununua umeme au kulipia huduma zingine za umeme kutumia njia mbadala ya mitandao ya Simu na makampuni mengine yenye mikataba na TANESCO.
Jitihada zinaendelea ili kuhakikisha mkongo huo wa mawasiliano unaungwa mapema iwezekanavyo.
Uongozi unaomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...