Ili kuwezesha upatikanai rahisi wa huduma za mtandao – Mahoteli, Viwanja vya ndege na maeneo mengine ya mkusanyiko wa watu kumekua na huduma ya Mitandao inatolewa kupitia teknolojia ya “Hotspot – Wi-Fi” ambapo imeendelea kua na umaarufu mkubwa hivi sasa.

Kama ilivyo katika maeneo mengine ya Hili nalo limekua na upande wa pili ambapo kumeibuka wimbi la wahalifu mtandao wanaotumia udhaifu uliyoko kwenye huduma hizi za bure za “Wi-Fi – Hot spot” kudukua  na kuleta madhara kwenye mtandao.

Wahalifu mtandao wamekua wakiweka “Wi-Fi” za bure ambazo si sahihi “Fake” ambapo wanategemea watu wengi watazitumia na baadae kukusanya taarifa zao na kufatilia vinavyosambazwa kwenye mtandao na baadae kupelekea kufanikisha uhalifu mtandao.

Kampuni ya usalama mtandao ya “Avast” hivi karibuni imefanya jaribio la kuangazia uelewa wa watu juu ya huduma hizi za bure za kujipatia mtandao “Free Wi-Fi” ambapo kampuni hiyo iliweka idadi kadhaa ya “Fake Free (Hot spot) Wi-Fi” kwenye mkutano wa Kisiasa nchini Marekani “Republican National Convention”.

---------------------------------------------------
NOTE: "Travellers should be conscious of hackers who will attempt to physically steal laptops, tablets and cell phones from luggage, hotel rooms or coffee shops when they are left unattended"
---------------------------------------------------

Takwimu zlizo kusanywa na Kampuni hiyo zinasema watu zaidi ya 1200, Walitumia huduma hiyo iliyokua imewekwa kwa mtego na asilimia 68.3 walitoa taarifa zao binafsi. Huku ikielezwa mashindano ya Olympik hili pia linategemewa kujitokeza.

Aidha, Takwimu za jaribio hili ziliendelea kueleza – aribio lilifanikiwa kufahamu Asilimia 38.7 walitumia Facebook; asilimia 13.1 walitumia Yahoo Mail, asilimia 17.6 waliperuzi barua pepe zao kupitia  Gmail, na Asilimia 13.8 walitumia programu zyingine za kuwasiliana kama vile  WhatsApp, WeChat pamoa na Skype.

Kiuhalisia kama zoezi hili lingekua limefanywa na wahalifu mtandao, Hakika wangefanikiwa kudukua kila kinachopatikana kwenye mifumo ya washiriki kaika mkutano huo ambapo jaribio hili lilifanywa. Na hii ni hatari zaidi hasa pale unapo tumia kifaa cha ofisi kilichokusanya taarifa muhimu/za siri ambazo hazikutakiwa kuangukia kwenye mikono ya asiye husika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...